Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

KITABU CHA PILI

9.Kuanza kuhesabu

"Lingine tena!" Rayford alijiongelesha alipokuwa ameketi kwenye dawati lake usiku mmoja Januari.

Ilikuwa yapata miezi kumi na minane tangu Straits kujiunga na Jesans. Hali ya Rayford kuwa makini katika utabiri wa Bibilia, na mori yake katika kufundisha, ilipelekea kupanda daraja na kuwa kiongozi katika jamii. Alijiuliza iwapo angalikuwa na furaha jinsi hii angaliendelea kuwa rubani. Maisha yalikuwa matamu na ya kupendeza tangu alipochukua uamuzi na kumpatia Mwenyezi Mungu chochote alichokuwa nacho.

Cheo cha Rayford katika jamii kilipelekea kujitoa mhanga kwa Neville, aliyefurahia kufanya kazi pamoja na Rayford kwa kutumia kifaa alichopenda.tarakilishi. Neville alionekana kama kijana barubaru, na Maria asiye na uzoefu wa kusema mengi, alifurahi kuona mumewe akibadilika hivo.

Wote wawili walikuwa wamefanya kazi kwa pamoja zaidi ya mwaka mmoja, huku Rayford akiandika makala kuhusu mambo ya kila aina (na hasa kuhusu jinsi kila aina ya makala yalivyolingana na matukio ya wakati fulani duniani), na Neville kuanda mtandao kwenye tuvuti ili watu waweze kupata yale makala aliyoanda Rayford. Kwa wakati fulani Rayford angalitayarisha majarida manne au matano kwa siku moja. Kichochezi kilitokana na kule kujihusisha moja kwa moja na Jesans, na kutoka kwa fikira au mazungumzo waliyokuwa nayo mitaani.

Neville alianda kitabu cha wageni, msukumo wa mtandao na kifuatilizi katika ukurasa wao kwenye tuvuti. Halikadhalika aliweka utaratibu wa mafunzo, ambao ulinuiwa kuwataini wasomaji moja kwa moja kutoka kwa jarida moja hadi lingine. Neville alihakikisha kwamba ukurasa wao ulipata uwakilishi katika pembe zote za dunia na mitambo yote ya kupeperusha ujumbe wa tuvuti, na pia kukusanya anwani nyingi za barua pepe kutoka kwa jarida la mtandao ambalo lilichapishwa kila mwezi na Chloe pamoja na Reinhard. Dhamira ya jarida hilo lilikuwa kuwachochea wasomaji wengi kuutembelea ukurasa wao kwenye mtandao.

"Tazama hili" Rayford alisema baada ya kumaliza kusoma jarida lililokuwa mkononi mwake. Alipinduka kwenye kiti na kupitishia Irene. "Barua sita katika anuani, na wote kuonekana kuwa na uaminifu. Je itakuwa furaha kupata angalau mshiriki mmoja kutoka kwa hawa wote?"

Rayford alianza kutaambua ukweli wa dhana ya kundi hilo kwamba Mungu alikuwa anakusudia kupinga watu kujiunga nao. Walikuwa hawajapata mfuasi tangu ajiunge nao, na alijaribu kila awezalo kutambua shida. Angalau mara moja kwa mwezi walipata barua kutoka kwa mtu aliyesoma majarida yao au kutembelea ukurasa wao kwenye tuvuti. Lakini hawakupata kusikia lolote kutoka kwa watu hawa tena. Kupata watu sita kwa siku moja wakitaka maelezo zaidi lilikuwa tukio lisilo la kawaida.

Irene alisoma barua hizo na kisha kuongea. "Yaonekana kuwa mambo makuu, au sivyo? kuna mpango upi kuhusu barua hizi?"

"Neville na maria wataondoka wiki ijayo. Nitajaribu kuwaleta wote sita hapa Jumatatu. Kisha sitajibu swali hilo mara kwa mara."

"Wafikiri ni bora kuwaleta hapa?" Irene aliuliza. Azimio la kundi halikuwa kutoa anwani ya Neville kabla ya kumuarifu.

"Nina wazo kuhusu hili," Rayford alisema. Natumai kuna ulinganifu na mazungumzo ya Yerusalemi."

Rayford alikuwa akiongea juu ya mpango wa Umoja wa mataifa kujenga hekalu kwa wayahudi kule Yerusalemi. Dunia ilikuwa imeanza kujiendeleza baada ya kuangamia kwa Amerika, na sasa ulikuwa wakati wa watu kutafakari na kufikiri juu ya mambo mengine. Mazungumzo yalikuwa yakiendelea kule Israel yapata wiki mbili au tatu zilizopita. Katibu mkuu Dangchao alikuwa huko kwa siku tatu zilizopita, na hata Baba mtakatifu alihudhuria.

Waarabu walikaidi na kusema kwamba kutazuka vita iwapo mtu angaligusa mnara wa mwamba, hekalu lao la msikiti. Lilikuwa limejengwa yapata karne nyingi zilizopita, hasa katika eneo la hekalu la Solomon, mahali ambapo tangu jadi wayahudi walimtolea Mungu dhabihu. Lakini Dangchao alikuwa na mbinu ya kuwabembeleza. Mbinu hiyo ilijumuisha ujenzi wa hekalu la kiyahudi upande mmoja wa mnara wa mwamba na ule upande wa pili kujenge hekalu la Kikristo. Msikiti uliopewa heshima hizo hautashikwa. Baba mtakatifu mteule Pope Pius XIII, alikuwa amedokeza kwamba angalitoka Vatican na kuchukua nafasi ya makao mapya kule Yerusalemi, eneo lisilo mbali na hekalu mpya, na pia kama ishara ya kuonyesha hali ya kujitoa kwa Vatican kwenye kumbukumbu ya ushirikiano wa kidini.

Waislamu hawakufurahia uamuzi huo, Lakini kulikuwa na kitu ndani ya Dangchao kwamba hatakubali La kama jawabu.

Iwapo watu walidhani kwamba Amerika ilikuwa na upendeleo kwa wayahudi, Waamerika walionekana kuwa na matumaini kulingana na Dangchao. Idadi ya walinzi kutoka Umoja wa Mataifa ilikuwa imeongezeka katika mji mtakatifu. Na Waislamu walifahamu jambo hili kama onyo kuhusu yale Dangchao angalifanya endapo hawangekubali "mtaji" wa hekalu.

"Mazungumzo Yerusalemi? Sikumbuki ni lini tumekosa kusikia kwamba aina fulani ya mazungumzo yanaendelea kule Mashariki ya Kati. Sasa katika miaka hii yote tulitazamia kuona ukweli halisi wa mambo. Iwapo Dangchao angaliwachilia, hilo litakuwa dhibitisho kwamba kuhusu yale niliyokuwa nikifikiri

Rayford alikuwa akifikiri ya kwamba Dangchao alikuwa kama ilivyotabiriwa kuwa mtu asiyependa Kristo. Jambo kama hilo halikuwa kwenye fikira ya uma, kwasababu lolote alilofanya Dangchao lilikuwa kwa maslahi ya binadamu. Ilikuwa tu ni ufahamu wa Bibilia kulingana na Rayford, ndiposa akahisi kuna tukio lisilo la kawaida kutokana na ujasiri wa Dangchao. Shida moja ilikuwa jina lake. Kulingana na utabiri wa Bibilia (Ufunuo wa Yohana 13:17-18), suluhisho la idadi ya herufi za jina la mtawala wa mwisho duniani litakuwa jumla 666. Haijulikani mbinu au mtindo aliotumia Rayford (Kigriki, kihibrania, Kilatino au hata Kichina iliyo lugha ya Dangchao) idadi ya herufi zote kwa pamoja zilipungua.

Herufi za kiRoma zilikuwa X, D na C, kwa jumla zikiwa 610. Herufi I, V na L zilihitajika kuongeza 56* iliyokuwa imekosea. Katika Kigriki na Kihibrania aidha idadi ya herufi hizo ilikuwa chache. Rayford hakuwa na la kufanya kuyahusu hayo. Hata hivyo kulikuwa na mambo mengine mengi yaliyoashiria kwamba Xu Dangchao alikuwa miongoni mwa wale waliotabiriwa kuwa wakaidi wa Ukristo, na walio mkana Yesu.

Uwezo na kufaulu kwa Dangchao kuuteka ulimwengu kupitia Umoja wa Mataifa, kilikuwa ni kidokezo cha nguvu alizokuwa nazo, lakini Rayford alipaswa kukiri kwamba Umoja wa Mataifa haukuwa utawala rasmi wa dunia. Kila Taifa lilijitawala kulingana na maadili yao.

Lakini Dangchao alikuwa amebuni jeshi la umoja wa mataifa lililosambazwa pembe nyingi za dunia kwa kisingizio cha kudumisha amani. Kutokana na kuwepo kwa jeshi hilo, dunia nzima ilipata amani, au hata umoja, yapata mwaka mmoja na nusu tangu kuanguka kwa Amerika.

---------------------------------------------------------------

*Herufi I, V, X, L, C na D (Herufi za kiRoma zinazowakilisha 1, 5, 10, 50, 100, na 500) lazima zionekane mara moja (na iwe mara moja), na herufi M (1,000) haipaswi kuonekana katika jina lolote linalotarajiwa kufikia 666 katika kiRoma.

Fahamu: Majina yote yaliyotumiwa katika riwaya hii sio ya kweli. Kuna uwezekano kwamba mtawala asiyetambua Yesu atakuwa na jina lililo na idadi ya 666 katika herufi za Kilatino, Kigriki na Kihebrania.

Iwapo Katibu Mkuu Dangchao angalifaulu kupata hekalu kwaniaba ya Wayahudi, Rayford hangalishawishika tu kwamba huyu ni mpiga Kristo vita, bali angaliweza kuhesabu siku zilizosalia kabla ya kurudi kwa Yesu Kristo.

Rayford hakulala mapema siku hiyo, huku akisoma zile barua sita na kufikiri juu ya ule mkutano wa Jumatatu. Alikataa kula siku ya Jumamosi na Jumapili, na kukaa pekee yake chumbani mwake au kuzunguka nje. Alimuambia Irene machache kumuarifu kwamba mambo sio mabaya, kati yao wawili au kati ya Rayford na Mungu. Hali yake hiyo ya unyenyekevu ilikuwa katika ile hatua ya kusubiri au kutarajia mipango ya Mungu.

Alipowapigia simu wale watu waliotaka maelezo kamili, aliwapata kama waliotayari kupokea na kujitolea. Yohana Doorman na Dada Maria Teresa walikuwa na kazi zilizowawezesha kupata fursa ya kuhudhuria. Matayo Baker na Sheila Armitage hawakuwa na ujira. Wale wengine wawili walisema kwamba wataomba ruhusa ili waweze kuhudhuria mkutano huo Jumatatu.

Yohana Doorman aliyekuwa na umri wa miaka 42 alikuwa mfuasi wa Mashahidi wa Yehova, na alipata uguso kutokana na mafundisho na utabiri wa wale Jesans, hivyo basi kuvutiwa. Jesans walihubbiri kwamba serikali zote zina ukaidi, na kwamba Mwenyezi Mungu anatafuta watu wanaotii na kulitimiza neno lake na wala sio siasa. Doorman alikuwa Mpasifisti. Alikuwa amehudumu kama mmishonari katoka bara lake la Afrika na kwa wakati fulani kutiwa mbaroni kwasababu ya imani yake. Alikuwa hajaoa na wakati mwingi alifanya kazi za mkono ili kupata fursa zaidi kutumikia kanisa.

Dada Maria Teresa alikuwa na umri wa miaka 56, mtawa wa kikatoliki na mshiriki wa Wanadada katika Yesu. Aliishi na kufanya kazi ya jamii na wahamiaji katika vitongoji vya mji wa London. Alivutiwa na maisha ya kujitolea ya Jesans, na dhamira ya kujenga jamii iliyojumuisha waliooa na wale ambao hawajaoa.

Matayo Baker alikuwa mbatizaji wa umri wa miaka 40, aliyejishughulisha kwa kutembelea Hospitali magereza na miji. Alifurahishwa na msimamo wa Jesans kuhusu maisha na hasa kuhusu ndoa na talaka. Bibi yake alimtalaki baada ya miaka miwili ya kuoana, kutokana na tofauti za kidini.

Sheila Armitage alikuwa mfuasi wa dhehebu la marafiki na mwenye umri wa miaka 70 na halikadhalika msagaji, na aliyevutiwa sana na Jesans kutokana na moyo wao wa heshima na kushirikiana na imani tofauti za watu, na hasa kuwa muaminifu kwa Mwenyezi Mungu sio sawa na kuwa mwaminifu kwa dhehebu fulani.

Mike Anastopoulos alikuwa mwanagenzi wa umri wa miaka 36 kutoka Uturuki, aliyekuwa akisomea shahada ya uzamili katika Chuo kikuu katika taaluma ya mambo ya kale. Yeye hakuwa mfuasi wa dhehebu au dini yoyote na alijiita Mbinadamu. Mike alivvutiwa na ushirika wa Jesans hasa kuhusu msimamo wao juu ya uchumi, na hasa maisha nje ya uchumi na kisiasa.

Hatimaye tulikuwa na Luis Rafael, mwenye umri wa miaka 29 Mpentekosti kutoka Brazil. Hapo awali alikuwa amejiunga na ushirika fulani wa kipentekosti ulio kuwa na mafundisho ya kutatanisha kuhusu jinzia. Luis alifurahia mafundisho ya jamii kuhusu Bibilia na imani, lakini alichukizwa na baadhi ya mafundisho yao. Alivutiwa na Jesans kutokana na jinsi walivyotafsiri mafundisho ya Yesu Kristo, na jinsi walivyochukulia maadili hayo kama njia ya kukadiri mafundisho mengine.

Rayford alisoma barua hizo zote, na kurudia mara kadhaa Ijumaa usiku, na kujadili mambo fulani yaliyomvutia kuhusu kila mmoja kupitia kwa simu alizowapigia Jumamosi. Wote sita walionekana kama waliokuwa na kiu cha kutaka kufahamu mengi zaidi, hata hivyo kulikuwa na hali ya kuasi miongoni mwa wote hao. Alimuomba Mwenyezi Mungu kumpatia hekima na ujasiri kukumbana na hali yeyote ya uasi atakapo kutana nao Jumatatu.

***

Luis Rafael ndiye aliyekuwa wa kwanza kuwasili siku ya Jumatatu asubuhi. Rayford ndio mwanzo tu alikuwa akimjulisha kwa Irene, ndiposa kengele ililia mara nyingine.na mara nyingine. Saa nne kamili, watu hao sita walikuwa wameketi kwenye sebule ya neville.

"Wacha tuone.Tutanzia wapi?" Rayford alisema. "Na iwapo wewe utaanza, kwa kuuliza swali ulilo nalo, nasi tujaribu tuwezavyo kujibu." Alimtazama Irene kana kwamba anatafuta uungaji mkono.

Mike Anastopoulus, mkufunzi wa mambo ya kale, alitazama na kufahamu kwamba wenzake wote kwa kiwango fulani walikuwa wafuasi wa madhehebu fulani. Yeye ndiye aliyeongea kwanza. "Ni lazima tuamini kwamba Mungu yu pamoja nasi katika kikao hiki?"

"Itategemea na vile unavyomaanisha kumuamini Mungu," Rayford alijibu. Hapo aliona Matayo na Luis wakiingilia mara moja, wawili hao walikuwa waingilisti wa kikristo kwenye chumba hicho. Walisonga na kusikiza kwa makini yale Rayford alitaka kusema.

"Mafunzo ya kidini hayatatuponya." "Imani ndiyo itatuponya kwa kuamini Mwenyezi Mungu tunayemtambua. Ukimuita wa upendo au wa kweli, lolote utakalo, lakini ni Mungu."

Mike alionekana kufurahia jawabu hilo, lakini Matayo na Luis walitazamana kwa shaka kabla Luis kuinua mkono ili aongee.

"Sikubali," alisema. "Iwapo mtu ni mnyoofu na muaminifu, basi lazima aweze kumuamini Mungu."

Yohana Doorman alifikia kibeti chake na kuchomoa toleo la gazeti, na kumpatia Mike. "Yahova Mungu anataka kila mtu kumtambua kwa jina lake," alisema. "Kuna makala fulani katika jarida hili ambayo yatakusaidia."

"Je, hilo ni jarida la Amkeni?" Matayo aliuliza. "Je, wewe ni mfuasi wa Mashahidi wa Yehova?"

"Uh-oh," alidhani Rayford. Hili ndilo jambo ambalo alitaka kuepuka. Mashahidi wa Yehova wamekatiliwa kote ulimwenguni na madhehebu yote ya Kikristo. Msisimuko uliokuwa kwenye chumba kile ungewezesha mambo makuu ya Mwenyezi Mungu kujitokeza, bora tu kutakuwepo na masikizano. Kwa sasa mwelekeo uliokuwa unaanza kuchukuliwa ulikuwa ule Rayford ameshuhudia kati ya madhehebu mbalimbali. Yeye aliamini kwamba Mwenyezi Mungu angalitenda miujiza, lakini mambo hayakuwa hivyo.

"Ndio mimi ni shahidi wa Yehova," alijibu Yohana Doorman, kwa madaha huku akishika kidevu chake kwa majivuno.

"Na wewe Je?" Matayo Baker alisema, akielekeza swali kwa Dada Maria Teresa. "Kutokana na mavazi yako, nakuchukulia kama mfuasi wa kikatoliki. Je nyinyi humuabudu Maria?"

"Naam, Mimi." Maneno yalimpotea Dada Maria.

"Waona kinachotendeka hapa?" Mike aliingilia kati, huku akinyosha kidole kumuelekezea Matayo. "Hii ndio sababu sikupata nafasi kwa dini au dhehebu lolote. Hakuna lolote ila malumbano na kushutumiana. Chukua gazeti lako. Sina haja." Alirudisha jarida la Amkeni kwa Yohana Doorman.

"Labda sote tuweze." Sheila alianza, huku akitarajia kuwatuliza; lakini alikatizwa, huku Mike akiendelea:

"Sikuja hapa kusikiza yale mtakayo sema hapa. Nilikuja kusikiza yale waliyonayo Jesans!"

"Haijalishi kile wanachoabudu Jesans," Luis alisema kwa sauti, huku akiruka juu.

"Jambo muhimu ni yale mafundisho ya Bibilia."

"Na iwapo siamini maadili ya Bibilia?" Mike aliuliza.

"Basi labda hauko nasi hapa!" Matayo alijibu, huku akiruka tena huku akielekea upande wa Mike akiongea.

Sheila kwa haraka alisimama kati ya wanaume hao wawili akinyosha mikono yake kana kwamba anaongoza wana ndondi. "Mbona tusikae chini na ."

Lakini Luis alipaza sauti kumshinda Sheila. "Katika kitabu cha Matendo 4:12 Bibilia inatuarifu, "Kwa hakika hakuna wokovu kwa lolote lile; kwani hakuna mahali popote isipokuwa mbinguni."

"IMETOSHA!"

Kulikuwa na hali ya kutoelewana kufuatia mjadala huo. Wale walio kuwa hapo hawakupata kuelewana iwapo Rayford anggali toa maoni yake.

"Ulikuwa kama mlipuko," Luis alisema hapo baadaye, "ila tu ilitoka kinywani mwake."

Lolote au chochote kile kiliwapelekea watu kukimbia ndani ya chumba na kumuelekezea mwenziwe. Dada Maria ndiye aliyeketi peke yake, alikuwa tayari amesongesha kiti chake. Irene aliyekuwa amesimama nyuma ya Rayford ndiye aliye epuka. Wengi wao walijeruhiwa. Mwangaza ulifuatia mlipuko. Kila mmoja kwenye chumba hakuweza kuona kwa muda.

Rayford alipigwa na butwa kama wale wengine. Lakini akaanza kunena-- kwa nguvu asizopata kuwa nazo mbeleni. Ilimuogopesha, lakini ingalimuogopesha zaidi laiti asingalizungumza, kwasababu alielewa kwamba yote yaliyotoka kinywani mwake hayakuwa maneno yake. Yalikuwa maneno ya Mwenyezi Mungu.

Alipoanza kuongea, chumba kilinyamaza na kutulia. Watu walisikiza kwa makini kuliko walivyowai kumskiza mtu yeyote hapo awali.

"Hamjafika hapa leo kwasababu maadili na imani yenu ni sawa na kweli. Mungu amewaleta hapa; na amefanya hivyo kwasababu nyinyi wote ni waaminifu. Kwa miaka elfu mbili amevumilia, na hata kushuhudia mgawanyiko ambao umedumu kati yenu na waumini wengine. Wengi wenu mmehubiri mahubiri yenu yasiyotosheleza, huku mkitumai kwamba mmetoa picha nzima, ilihali mlikuwa na sehemu tu. Kwa kupuuza mmebuni makundi na mkawa wabinafsi kwa kupuuza. Mkawa watu wa kuwatazama wafuasi wa madhehebu mengine kama walio chini yenu na wasiofaa.

"Mungu aliwaacha katika njia hiyo yenu ya kupuuza, ili kujaribu unyenyekevu wenu mbele Yake. Alitaka kuona iwapo mtaweza kutii yale mliyokuwa mkifundisha na kuhubiri, hata ikiwa yalinuiwa kuwatenganisha na jamii au marafiki. Mko hapa hivi leo kwa kufaulu majaribio hayo."

Rayford akapaaza sauti yake tena. "Lakini SASA. sasa, ni wakati wa kukua!" Wale waliokuwemo walisonga nyuma huku wakitarajia mlipuko mwingine.

Lakini haukutokea. Sauti ya Rayford ilipungua badala yake.

"Tafadhali muniamini. Njia ya kipekee ya kuitikia ukweli ni kwa neema ya Mungu. Amewateua nyinyi kwa ajili ya uwazi wenu-- sio kwasababu ya taaluma ya kidini.au kwa kuikosa." Alimtazama Mike alipokuwa akisema maneno hayo ya mwisho.

Rayford alichukua kifurushi cha vijitabu vitatu vilivyofungwa na kuwapitishia wote sita. Muda wa mwaka mmoja uliopita, alikuwa amefanya bidii kutayarisha yote yaliyokuwemo.

"Kuna makala ya kila aina kuhusu mambo tofauti kwenye nakala hii," alisema. "Mtapata baadhi ya kushangaza. Yatakuwa changamoto ya maadili na imani zenu.

"Ndugu na dada," alisema kwa kutua na kutabasamu, "Ni wakati wa kutafakari na kuchambua maswala ya kindani na ukweli ambao hamjawai kupata. Ni wakati wa kudhihirisha kujitolea kwenu na imani yenu kwa kusikiza kila mmoja wenu na kuweka kando tofauti zenu."

Rayford alijaribu kutoa taswira ya mambo aliyokuwa akitaraji.

"Muafaka wa makubaliano unatiwa sahihi kule Yerusalemi leo," alisema. "Kabla kufika alasiri hivi leo , ujenzi wa hekalu jipya utaanza kule Yerusalemi. Lakini muafaka mkuu wa makubaliano umeafikiwa kule mbinguni. Mungu atajenga Hekalu lake, amini musiamini atawatumia nyinyi hapa kujenga hekalu hilo. Tumeingia kipindi au awamu ya mwisho wa miaka saba ya historia ya ujenzi wa kanisa. Mambo makuu yanatukia tu katika kipindi cha miaka mitatu na nusu ijayo, ni jukumu letu kuanda dunia kwa wakati huo."

Rayford alitulia, ilikuwacha uzito wa masimulizi hayo kuwaingia. Kisha akaendelea.

"Kifo cha Yesu kiliadhimisha mwisho wa madhehebu. Mungu kwa miaka elfu mbili amekuwa akimchunguza mtu kivyake, akijaribu kujenga imani inayo zidi mkusanyiko au ufuasi wa dhehebu.

"Sasa hivi atajumuisha maadili mema na vipande vya ukweli na uaminifu kujenga kanisa lake, na wala sio lako".

Mike mwanaharakati za kibinadamu alifurahi kumsikia Rayford akiongea juu ya utu na tabia; lakini alikuwa akijaribu kupambanua kwamba yote yalikuwa yakitoka kwa Mungu-- wa kweli na wa Kikristo. Maneno kama "Kanisa" na "Yesu" yalikuwa magumu sana kwake kusadiki. Mike hakufurahia mazungumzo ya kuanda kundi lingine.

Katika njia moja au nyingine, kila mmoja katika kundi hilo alikuwa anaona uzito fulani. Walikuwa wamewekwa kwa pamoja na watu waliodhani kwa wakati mmoja kama adui. Lakini uwepo wa Mungu uliwashahuri kwamba Rayford hakuwa kama guru aliyetaka kubuni dhehebu.

Rayford aliendelea; "Hivi sasa, katika sehemu nyingine ya dunia kuna mkutano kama huu unaoendelea kama huu. Kuna watu wengine sita kama nyinyi. Mmoja ni Mhindi, mwingine Muislamu, na mwingine Muyahudi." Yale Rayford alikuwa akisimulia hayakutoka kinywani mwake kama hapo awali, bali yalitoka kwa Mwenyezi Mungu.

"Iwapo unafikiri kuna tofauti za kuepuka, fikiri jinsi inavyoweza kuwa. Lakini Mungu anawataka ninyi watu sita kwa pamoja na wale sita walio mahali kwengine, kuendeleza kanisa lake hasa nyakati hizi za mwisho. Nyinyi mtakuwa mahakimu wa nyakati hizi za mwisho. Lakini mwapaswa kuepuka tofauti mlizo nazo.

"Mpango wa Mwenyezi Mungu hapo awali ulikuwa kwa watu wake kuwa na makabila au koo kumi na mbili, na mahakimu kumi na mbili kusuluhisha matatizo yaliyotokea kati ya koo hizo. Sio wafalme. Sio utawala wa kihimla, Lakini mahakimu wa koo. watu kama Samweli, na Gideon, na Debora." Aliwatazama Sheila na Dada Maria Teresa alipotaja Debora.

"Kazi yenu itakuwa kuwasaidia wale wanaoamini kutoka maeneo yenu kufahamu mema na mabaya. Hamtaweza kufaulu kutekeleza hayo kabla ya kuzika tofauti zenu, na vilevile kufahamu upungufu wenu wa kuelewa."

Rayford alihisi upako kutoka kwa Mungu ukididimia na kujihisi tu kama wale wengine.

"Ndugu na Dada sina majibu yote. Yale niliyotayarisha kwenye makala hayo ni muongozo tu. Lakini muhimu zaidi ni kwenu kuelewa na kujifunza kufanya yale Mungu anataka iwapo hata wewe mwenyewe hutaki. Lazima mtazame mbele na sio tu madhehebu yenu. Kuna mengi ya kujifunza kwa muda mchache."

"Tutajaribu kujadiliana tena, wakati huu naomba msikize kwa makini, na kuomba na kufikiri kabla ya kuongea. Nyinyi wote mnaweza kueleza mliyo nayo, lakini hayawezi kuwa mengi mnavyofikiri."

Mazingira katika chumba yalikuwa yamebadilika. Kila mmoja alikuwa mpole. kwa kunyenyekea na kufuata ukweli aliosema Rayford, na uwepo wa Mwenyezi Mungu kwenye chumba hicho. Kwa utaratibu walianza kuondoa tofauti na uhasama baina yao; lakini mara hii kwa uoga. Iwapo hali ya utatanishi ilitaka kutokea, waliomba ili kupata hekima.

Hivyo basi, nusu ya kabila kumi na mbili kutoka Magharibi ilikuwa imebuniwa kama walivyojiita.

Zion Ben-Jonah Aandika

Mtume wa Kihibrania, Danieli alitabiri kuhusu "Watu wa Mungu" miaka 453 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu. (Danieli 9:24-26) Alisema kwamba imebakia miaka 490 kwa watu wa Mungu, lakini Masia "atakatwa" miaka saba tu kabla ya kukamilika miaka 490, mnamo mwaka wa 30A.D (Tazama Armagedon ya Kwanza" sura ya 6, wiki sabwini" kwa maelezo zaidi kuhusu fungu la maneno haya.)

Kusulubishwa kwa Yesu kuliadhimisha mwisho wa makundi ya madhehebu na dini. Mungu amekuwa akimhudumia mtu na kumtunza kivyake yapata miaka elfu mbili sasa. Mipango ya kuendeleza "Kanisa au dhehebu" fulani yameisha na sasa kuna "ufalme wa mbinguni" ambao Yesu alisema hauonekani. (Luka 17:20)

Lakini Danieli alitabiri kwamba watu wa Mungu wataonekana tena kufuatia "maelewano" yaliyoafikiwa miaka saba kabla ya "kumalizika" kwa vitu (Danieli 9:27) Unabii huu umeandikwa kama kwamba ni makubaliano mawili yaliyo sambamba. Moja ni kati ya Kristo na wafuasi wake na nyingine kati ya waasi wa Kristo na Kanisa.

Maafikiano yatapelekea kutoa kwa kafara mara nyingine (kwa sasa hakuna) Hekalu Yerusalemi. hasa kwa miaka tatu na nusu ya makubaliano. Na pia kuleta pamoja "makabila" kumi na mbili ya wafuasi wa Kikristo.