Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

10. Makabila Kumi na Mbili

Majadiliano yaliendelea siku nzima. Kila mmoja kati ya watu hao sita waliokuwa kwenye sebule ya Neville walikuwa wameona mengi ya kusimulia. Mwisho wa siku walikuwa wameanza kuhisi uzito wa jaribio hili. Dini yao, kazi na familia zao yalikuwa sio muhimu, kila mara imani yao ilipoimarika na kujifunza mengi kuhusu Mungu.

Irene alileta chakula siku nzima, na pia kuhakikisha malazi yote yatakuwepo endapo hao wote wataamua kulala kwa Neville hadi pale watafahamu hatima yao kulingana na mipango ya Mungu. Majadiliano yaliendelea hata usiku wa manane. Waliweza kujilaza kwenye sakafu ili kupumzika na kuendeleza mjadala.

Siku chache zilizopita kulikuwa na mabadiliko kutokana na uamuzi wa wale waliotoa maisha yao na kumkubali Yesu Kristo. Mike alilazimika kukiri sio tu kuwepo kwa Mwenyezi Mungu bali pia yale Mwenyezi Mungu alikuwa amemtendea maishani mwake. Hata ingawa Sheila alikuwa hajashiriki kwenye tabia ya usagaji kwa miaka mingi, alikuwa ametetea tabia ya ushoga kwa maisha yake yote. Sasa alipaswa kukubali kwamba hali yake ya kukaidi na kuunga mkono tabia potovu haikuwa tofauti na yale aliyokuwa akipinga.

Mwishoni mwa juma, kundi hili jipya lilianza kupata miujiza ya kupendana na kuishi vyema, na kuanza kujadili hatua itakayofuata.

Barua pepe na mawasiliano kupitia kwenye tuvuti yaliongezeka. Jambo la ajabu lilikuwa kwamba nusu yake ilitoka Uingereza, na nyingine kutoka Afrika, Amerika ya Kusini, Uropa na mashariki ya kati, wote waliandika wakiuliza jinsi ya kupatana na Jesans, na pia kuungama na kutii mafundisho ya Yesu kama mbinu moja ya kubadili tabia.

Wale Jesans wa kiasili walirudi kutoka shughuli ya kueneza neno, nao Neville na Maria wakarudi kwa wakati huo. Wote hao walijiunga na kusherehekea tukio liliokuwa limetukia.

Kutokana na uzoefu wao kuishi ndani ya imani, Rayford alimpatia kila mmoja wa Jesans mhudumu wa kusaidia mmoja wa mahakimu jinsi ya kujitoa mhanga, kwa kiroho na kimwili katika nchi ya utumwa. Wiki tatu baadaye, kila mmoja wa wale waliookoka aliuza mali yake, na kutoa mali kwa jamii kwa kiwango ambacho walikuwa hawajawai kutoa. Kutoka kwa fedha hizo, tiketi za nauli ya ndege na Tarakilishi zilinunuliwa kwa hawa mamishonari wapya.

Watafutaji wa kweli wa wokovu walikuwa wakisubiri kuwalaki katika sehemu sita tofauti. Luis na Fran walienda Sao paulo, Brazil. Mike na Martin wakaelekea Ankara, Uturuki. Chloe na dada Teresa wakachukua magari kwenye feri kuelekea Ufaransa, na kisha Roma.

Sheila aliwai kuishi Moscow alipokuwa mdogo, kwa hivyo yeye na Reinhard (aliyefahamu Urusi) walijitolea kwenda Urusi. Na hata Raymie aliyekuwa mdogo na miaka kumi na mitano, aliambiwa amsaidie Yohana Doorman kule Johannesburg. Matayo Baker alibaki London kufanya kazi kwa pamoja na Rayford na Irene.

Jamii ndogo hiyo ilikuwa ikikua. "Inatendeka, sivyo?" Fran alisema aliposikia kuhusu wanachama sita. "Inakuja pamoja. Ahsante, Yesuu!" Na Fran aliwashukuru na kuwapungia wale wanaune aliokuwa akisafiri nao. Chloe, Reymie na wengine walitazama huku wakicheka.

Rayford alihutubia umati wa jamii hiyo iliyokuwa ikikua kabla hawajaelekea sehemu zao, mwezi mmoja tangu wakutane:

"Nyinyi wote mtawahudumia takribani watu nusu billioni" alisema. "Muda wenu ni miezi sita kutambua wale waumini 12,000 wenye imani kutoka kwa kabila mtakazo hudumu. Mtahitajika kuwafunza jinsi nilivyowafundisha. Vijitabu na makala hayo yatawasaidia, lakini yatahitajika kutafsiriwa katika lugha za huko na kuchapishwa tena haraka iwezekanavyo. Mtapata majaribio sawa nayale ambayo mmepitia muda wa wiki chache zilizopita. Muombe ujasiri, hekima na uvumilivu kwani mtahitaji hayo yote.

"Lakini msife moyo. Mungu yu pamoja nanyi!"

Licha ya yale wanayotarajia kukumbana nayo walijiona wakiwa na ujasiri kama ule wa Rayford. Mungu hakika alikuwa pamoja nao, na hilo ndio jambo kuu.

Zion Ben-Jonah Aandika

Ni hali ya kitamaduni kufikiria kwamba makabila kumi na mbila yaliotajwa kwenye kitabu cha Ufunuo wa Yohana ni ya kiyahudi. Lakini tunasahau kwamba wale wayahudi tunaojua kwa sasa lilikuwa kabila moja (ukoo wa Judah). Tabaka nyingine za Israeli ziliangamizwa hata kabla ya kuzaliwa kwa Yesu. (Hata yale majina ya makabila hayo kwenye Ufunuo wa Yohana ni tofauti na yale majina ya makabila kumi na mbili katika agano la kale. Hebu linganisha kitabu cha pili katika agano la kale (Kutoka) 1:2-7 na Ufunuo wa Yohana 7:4-8, utaona kwamba tabaka la Dan limeondolewa na mahali pake kuchukuliwa na kabila la Manasseh.)

Yale makabila kumi na mbili ya unabii yanawakilisha "Watu wa Mungu". Watu wake kwa vyovyote sio wale waliomkana Mwanawe Yesu. Watu wake ni wale waliomkubali Mwanawe. wale wanaomfuta Yesu (Mwanakondoo) kwa utaratibu popote anapowaelekeza, jinsi Bibilia inavyosema. (Ufunguo 14:3-4)

Mawazo ya kikaidi katika taasisi ya jamii wayahudi ni mfano wa hali ya kototii na kupuuza yale mafundisho na dhamira ya Mwokozi Yesu. Lengo la Mwenyezi Mungu sio kujenga na kuendeleza taifa la ukoo na damu ya Abrahamu, bali ni kujenga na kuendeleza taifa lililo na imani kama ya Abrahamu.

Kitabu cha Ufunuo wa Yohana kimemfananisha Yesu mara kwa mara kama "Mwana Kondoo", ili kutoa taswira ya wafuasi wake wanaofuata Kanisa lililojengwa kwa mkono (Matendo 7:48) ilikuwatoa kafara wanakondoo wengine. Wayahudi wa kiroho hawana haja kuhonyesha kanisa, bali wale wa kimwili hawana matarajio ya juu.