Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

24. Yerusalemi Mpya

Mwanya uliokuwa juu ya wateule ulizidi kupanuka na Rayford kujihisi akiukaribia kwa kasi sana. Huku mamilioni ya wateule kutoka kote ulimwenguni wakisonga kuelekea katikati ya kio, wale (kama Rayford na Chaim) walio wasili kwanza walichukuliwa kupitia kwa mwanya ule. Rayford alitazama chini na kuona mawingu chini yake. Lazima wako maili nyingi kuelekea juu, na bado wanaendelea.

Hata baada ya kupita mwanya ule, waliendelea kuelekea juu kwa kasi, wakiwacha nafasi kwa wingu lililokuwa na malaika na wateule wengine wakiwafata nyuma.

Ndani ya chombo kile, Rayford hakuhisi mvuto wa chini au juu. Ulikuwa ni kama ulimwengu mwingine, bila kuwepo uzani. Hatukuwepo na upungufu wa hewa safi, iwapo miili yao ilikuwa ikitumia hewa.

Kwa ghafla Rayford alijihisi mwenye hatia. Alikasirishwa na mji ule kiasi cha kumsahau Yesu, yule ambaye aliwezesha haya yote.

"Usiwache hilo likakusumbue!" mtu akasema au kitu. Ilikuwa kama kwamba sauti ilifanyikia kichwani mwake. Hata hivyo, Rayford alitazama kando na kuona malaika akitabasamu. "Utakuwa na wakati wa kutosha kukutana na Bwana ana kwa ana," alifikiri alisikia malaika akisema.hata ingawa hakuona mdomo wake ukiashiria.

"Waweza.?" Rayford alianza. Lakini jawabu lilimrudia hata kabla ya kumaliza swali.

"Hiyo ndiyo sababu niko hapa. Ni jukumu langu kuwaonyesha hapa, na kujibu maswali yenu."

Wale watu wawili (kwani malaika walionekana kama watu isipokuwa kwa hali yao ya unyenyekevu na uerevu pamoja na mavazi) walikuwa pia wakisonga kwa kasi kupita ule mji mkubwa waliokuwa wameingia tu. Umati ulikuwa ukipunguka, na ikaonekana kwamba kila mteule alikuwa na malaika wake wa kumuongoza.

Fikira za Rayford zilijaa mshangao jinsi vile alivyokuwa amefufuka, kuingia katika chombo kile, kushuhudia kurudi kwa Yesu, na jinsi taratibu za kisayansi zilivunjwa huku akionekana kama kijana.

"Ni takribani maili elfu moja na mia tano juu", malaika alisema huku akisoma akili ya mwanagenzi wake. Akili ya Rayford ilikuwa imejaa maelezo kuhusu alipokuwa na kilichokuwa kikiendelea kwa haraka.

"Mamilioni ya wateule wamefufuka kutoka kote duniani na kuletwa kwa kasi. Yesu yu pale ili wote wamuone kabla ya kuingia Yerusalemi mpya. Ndio Yerusalemi mpya. hilo ndilo jina la mji huu. Sote tumekuwa tukifanya bidii kuona wakati huu.

"Wakati kila mtu atakuwa ameingia ndani, kufikia jioni Israeli, tutakusanyika kushuhudia arusi. La hatutakuwa na giza hapa. Uwepo wa Bwana huangaza mji huu milele. Hakuna kulala, sherehe yaweza kuendelea kwa wiki kadhaa kulingana na saa za dunia, bila kuchoka.

"Umati? haitakuwa shida. Utamsikia vizuri tu jinsi unavyonisikia. Tutakuwepo na vio iwapo utahitaji kumuona, lakini sio mwili wake tunaoabudu, ni ukweli wake na nguvu. Tumeandaa vyakula vya kutosha na nyimbo nzuri pamoja na kucheza. Sherehe kuu, haujui jinsi sisi huku juu tulikuwa tukisubiri wakati huu"

"Hii ni raha tupu!" Rayford alishangaa, kwa furaha kwamba malaika wake alikuwa amemueleza machache kuhusu yale aliyokuwa akifikiri.

"Tunaelewa kutaka kwenu kutoa shukrani," Malaika alisema Sisi pia tunahitaji hilo Utafurahia nyimbo hizo! Itakuwa ni furaha kuu ya kutukuza katika historia. Kwa hakika itakuwa ya kupendeza na kuvutia!"

Rayford alijisikia mwenye hamu ya kumkumbatia malaika, na kisha malaika kwa furaha alimkumbatia. "Niite Bob" alisema. Na Rayford kushanga kwa jina hilo lisiloonekana kama lakimalaika.

"Wafikiri ni la kawaida sana?" Bob aliuliza. "Kwa hakika majina hayana maana hapa juu. Watu hawawezi kupotea, na watu hufahamu wanapoelezwa kivyao-- kama ninavyofanya--- lakini Bob litafaa iwapo utaona haja ya kutumia jina."

Ahsante Bob Rayford alijibu. Na fikira zake zikamgeukia Irene.

"Yuko hapa," Bob alimhakikishia. "Utamuona baadaye. Lakini utampenda kila mmoja hapa jinsi unavyompenda. Na Bwana. mbona, atakuwa kipenzi cha wote!"

Rayford aliona ukweli ndani mwa yote aliyosema Bob. Duniani alikuwa na mapenzi kwa Irene; alikuwa jukumu lake. Lakini hapa.kila mmoja aliishi kumfurahisha Mungu. Sherehe ya harusi kama walivyosema ilikuwa ni kuwaunganisha na Mungu. Raha aliyoona Rayford tangu kuinuka kutoka pale Hekalu la Mlima ilikuwa ni raha ambayo alikuwa hajapata kuona akiwa kule duniani, ikiwemo ngono. Hakumkosa hata Irene, au kuwa na hamu ya kumuona. Alijua kwamba wako pamoja. sio tu na kila mmoja, lakini na wateule wote. Walikuwa kitu kimoja katika kumuabudu Mungu. Walikuwa wameingia katika ndoa mpya--harusi na Mungu.

Fikira za Rayford zilichukua mkondo mwingine, na mara moja Bob akabadili sawa naye.

"Kule duniani?" Bob aliuliza. Wamehangaika, siwezi kukueleza hayo!" alisema kwa kicheko. "Ol Dangchao anawaambia tu hii ni nyota ya wageni wanaokuja kuharibu dunia. Kwa kiwango ni kweli. Lakini hawezi kudhubutu kumtaja Mungu. Kama angaliweza, basi wangaliona adhabu ya kutupiga vita na labda wangaliungama.

"Israeli imepitia kwenye maafa kwa wakati huu. Karibu 7,000 wamekufa kutokana na mtetemeko. Lakini Dangchao hajaguswa. Hafikiri juu ya yote ila yeye binafsi. Sasa hivi analia na kuomba majeshi kutoka pembe zote za dunia. Manuwari, ndege za kivita, makombora, na chochote kinachoweza kulipua kile kio"

"Wanaweza.?

"La. Hakuna nafasi. Haingesababisha lolote laiti wakidhubutu. Kio hiki sio kinga, Mungu ndiye. Tuliweka tu pale. Sawa na mawe ya dhahabu na mawe mengine yanayong'aa kila mahali hapa. Yanavutia, au sio?"

Majengo yale ya kupendeza katika Yerusalemi Mpya yalikuwa yameongeza raha aliyohisi Rayford. Kulikuwa na manukato yaliyo toa harufu nzuri, na aina ya mlio wa mziki wa kupendeza uliokuwa ukichezwa kichwani mwake. Maji masafi yalipita kwenye mji ule, maji hayo hayakuwa yamezuiliwa na ukingo wa mto, yalikuwa yamejishikilia tuu yenyewe, Rayford alinyosha mkono kuyagusa, kwa hakika yalikuwa baridi bila kitu kilichofunika kama alivyodhani.

Kulikuwepo sehemu zilizokuwa na mimea kama jangwa. lakini haikuwa jangwa. Ungalitembea juu chini ya vichaka, na maua ya kuendeza. Mimea ilionekana kukosa shina, hata ingawa tulikuwa na mimea ya kutambaa iliyokuwa na maua ya kupendeza.

Mawe ya dhahabu aliyosema Bob yalikuwa kando ya sehemu za kupitia. Mijengo aliyokuwa akiona haikuwa "nyumba" kama zile za ardhi. Hapakuwepo haja ya kuta au sakafu, kwani watu hawakuwa na lakuficha na aliweza kuwaona wenzao kutoka juu, kando chini na kokote pale. Sehemu ambazo zilipitisha mwangaza nusu ndizo zilizotumiwa kugawanya sehemu za mji ule, ili kinachoendelea sehemu moja kisije kuadhiri ule upande mwingine. Mawe mazuri na mimea ya kuvutia ndio iliyogawa sehemu hizo.

Iwapo kulikuwepo na lolote lililo wasumbua wateule katika Yerusalemi mpya, ulikuwa ni wakati au saa. Haungali zungumza kuhusu "usiku" au "kesho", au siku ngapi kabla ya kitu fulani kutendeka, kwa sababu hatukuwepo na usiku, aidha watu hawakulala.

Lakini wangalichukua muda kujiburudisha katika bustani za maua, na kisha kuingiwa tu na uzuri wa mazingira yale.

Kulingana na siku za dunia, sherehe ya arusi ilichukua majuma kadhaa. Rayford alikutana na Irene, Elaine, Chloe, . hasa wale Jesans wote na mahakimu kumi na mbili. Walijadili kuhusu yaliyotukia walipokuwa mbali mbali, msisimuko wao ulikuwa juu ya kufufuka, na kilichofanyika, na yale ambayo walikuwa wamejifunza katika Yerusalemi Mpya.

"Tunaenda kuutawala ulimwengu baada ya `vita'kukamilika," Raymie alisema. Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mbili, na ataendelea kuzeeka katika Yerusalemi Mpya hadi atakapofikia thelathini. "Jukumu hili" alisema. "Litatolewa baada ya sherehe."

Rayford aliwatayarisha kwamba hawatakuwa na majukumu mengi au magumu kama waliyokuwa nayo kule duniani miaka saba ile ya mwisho. "Imeonekana kwamba sisi huonekana wachovu tunapoongoza, na Mungu hutambua vipawa vya wale wenye imani miongoni mwa wafuasi wake. Twataraji kuona baadhi ya wenzetu wachanga wakipewa mamlaka," alisema.

Neville alikuwa kule pia, na alikuwa na ujumbe wa kufurahisha aliopokea kutoka kwa malaika wake.

"Mnafahamu jinsi tulivyoweza kutuma barua-pepe bila kuunganishwa au kuwepo kwa tuvuti?" alisema. Hakika ilikuwa ikitayarishwa kupitia chumba fulani hapa juu. Mahali hapa paweza kubadilika. Ilikuwa kule nje kwa wakati ule ili kuweza kutoa kiunganishi kwenye mtandao na kutayarisha barua zetu. Hiyo ndiyo sababu hatkupata kulipa kodi baada ya kuharibiwa kwa Web Wonders.

"Jambo lingine! walikuwa ni watu hawa ndio walioyeyusha Web Wonders na wala sio Dangchao, ili orodha na anwani zetu zisiweze kutambuliwa na dangchao na wenzake.

"Nimekuwa nikijifunza jinsi mambo yanavyofanyika huku juu. Sio uganga au kitu kama hicho. Kuna mengi na fizikia ambayo watu wa dunia hawajavumbua. Vitu kama kuepuka mvuto wa ardhi, na jinsi ya kusoma akili. Hata miili yetu mpya inafanya tu kazi kama ile ya awali ilivyofanya. Aina mpya. Haihitaji kulala, haitazeeka, na ina kinga dhidi ya maradhi. Tutaendelea kula na kunywa, lakini nguvu zaidi inatoka kwa Mungu. Inatufikia kupitia mwangaza unaofikia sehemu hii. Nje ya eneo hili tungalizeeka, kama mtu mwingine yeyote.

"Kuna mengi tu ya kujifunza," alieleza

"Sio ajabu?"

Kila mtakatifu alipata furaha kutoka kwa jambo fulani. Maria alifurahi kuona mabadiliko baina ya wenzake, kwamba walikuwa wachanga na wenye afya. Alifurahia kumsikiza Neville aliyekuwa akipata maelezo ya ajabu ya Fizikia. Kuwatazama tu Maria Teresa na Sheila Armitage waliokuwa na umri wa miaka thelathini, kulimvutia sana. Na sasa nguvu maradufu!. Alitaka kuongea na kila mmoja kutaka kufahamu aliyotendewa na Mungu.

Fran Luis, Mike na Martin walijikuta wakicheza kufuatia ujuzi wao mpya wa kuruka. Walikuwa kama watoto,, hata ingawa walionywa dhidi ya kuruka ovyo.

Matayo Baker na Yohana Doorman walichukua muda mwingi kwenye makavazi wakitazama kanda zilizo rekodiwa kuhusu maisha yao na ya wengine. Waliweza kuelewa kiroho kilichotendeka wakati fulani katika maisha yao. Wangalifahamu wakati walipoomba na kubwenyeza mahali ili kuona kilichowapelekea kuomba. Walifurahi sana jinsi Mungu na malaika waliweza kuunda orodha ya kila mmoja na matendo yake.

Reinhard alifurahia tu kuzunguka katika bustani akitazama maua na mimea ya kupendeza, na viumbe kama wanyama waliokuwa hapo.

Kulikuwepo angalau kitu cha kumffurahisha kila mmoja na kumfanya kuwa na la kufanya na kufurahia hata zaidi ya miaka elfu moja, kilichokuwa kipindi watakacho tawala ulimwengu. Yatakayotukia baada ya miaka hiyo elfu moja lilikuwa jambo la kujali wakati utakapo karibia. Lakini kwa sasa kila mmoja kwa kuongozwa na malaika na Yesu, atapewa jukumu wakati wa kutawala ulimwengu kwa miaka hiyo elfu moja.

Huku wakisherehekea, Mungu alikuwa akiwaadhibu waliokuwa chini ya ardhi. Yale maafa na mahangaiko waliyopitia wateule hayakuwa lolote ukilinganisha na yale yaliyokuwa yakishuhudiwa kule chini. Majeshi ya Dunia yalikuwa yakijiandaa kwa vita kati yao na Yerusalemi Mpya. Dangchao alipanga kulenga makombora kupitia mwanya walioingilia wateule. Lakini wateule kwa pamoja na malaika walikuwa tayari kuzuia shambulizi.shambulizi linalojulikana sana kama Vita vya Magedoni.

Zion Ben-Jonah Aandika

Ufunuo wa Yohana 21, unaeleza zaidi kuhusu Yerusalemi mpya inapofikia ulimwengu (yaani baada ya vita vya Magedoni).

Hatujaeleza kuhusu yale majitu yanayoambatana na mitungi ile `saba' ya adhabu. Waweza kujisomea katika Ufunuo wa Yohana 16. Hata hivyo kutokana na yote Mungu anayodhihirisha, ulimwengu hauko tayari kuungama. Licha ya hayo ulimwengu unazidi kuwa na ukatili na kumuasi Mungu. Wanaungana na kumpiga vita Mwenyezi Mungu. (tazama sura inayofuatia.)

Bibilia inatuarifu kwamba hatutakuwa na ndoa mbinguni. (Matayo 22:30, Mariko 12:25 na Luka 20:34) Hii ni ngumu sana kwa baadhi ya watu kuelewa, kwani ndoa ndiyo huonekana kuwa karibu sawa na mbingu (hata hivyo wengine husema ni karibu sana na jehanamu aidha!) Lakini kama tusivyoelewa jinsi Mungu alivyotenda Mengi (kwa mfano kuumba), hatuwezi kuelewa raha na uzuri aliopangia waja wake wanaomuamini.

Bibilia inatuarifu kwamba Mungu atatoa mwangaza katika Yerusalemi Mpya. Kuonekana kwa Yesu akiwahubiria mamilioni ya watu hakuwezi kufanyiwa taswira kwa urahisi. Lakini kwa kuungana na Mwangaza wa Bwana (Uwepo wa roho mtakatifu) na malaika, Yesu ataweza kutimiza haja za waaminifu pasipo matatizo yoyote.