Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

23. Mpasuko

Ilikuwa ni Alhamisi asubuhi kabla ya Rayford kufika Yerusalemi. Alikuwa amechukua muda mrefu kuweza kujipenyeza kutoka Uropa hadi Mashariki ya Kati. Alisikia kuhusu kutekwa kwa Chaim akiwa safarini. Rayford alielekea moja kwa moja hadi alikokuwa akizuiliwa Chaim katika makazi ya Mtawala, alipofika mji mtakatifu.

Katika safari yake kutoka Uropa, ni watu wawili tu ndio waliomtambua, na hawakuwasilisha malalamishi au uzushi wowote. Lakini hakuwa ameingia Yerusalemi kwa muda usozidi nusu saa, ndiposa watu walianza kunyosha vidole na kunong'onezana. Alipoingia umati wa watu ulimfuata, kuona kitakachotokea. Mtu alipigia waandishi wa habari sumu na neno hilo kufikia ikulu, mahali palipodhaniwa kwamba Rayford anaelekea.

Jambo la ajabu ni kwamba hakuna aliyemuongelesha, kumshika au hata kumkaribia Rayford. Kulikuwa na kitu katika mwenendo wake kilichowafanya watu kumuondokea.

Alipofika mbele ya ukumbi mkubwa unaoelekea kwenye ikulu, alilakiwa na kikundi kikubwa cha waandishi wa habari na majemadari. Kamera ziling'aa na kuwaka huku Dangchao akitoka nje kuelekea kwenye jukwa lile akiwa pamoja na walinzi wake. Majasusi wengine wa umoja wa Mataifa walikuwa wametapakaa kila mahali kushuhudia.

"Karibu! Karibu!" alipaaza sauti Dangcha ili asikike na umati.

"Nimekuja kumchukua Chaim Rosenberg!" Rayford alisema kwa sauti. "Mlete hapa nje!"

"Yumo humu ndani. Tafadhali karibu ndani!" Dangchao alisema huku akisonga kumkaribia Rayford.

Rayford alikaa pale chini ya sakafu, alipokuwa akiketi, kulitokea mtetemeko uliotingisha eneo lile. Yeyote aliyekuwa amesimama alianguka ila tu Dangchao, aliyejikakamua na kuyumbayumba kisha kusimama. Majasusi walianguka kutoka kwa kuta za zilizokuwa katika eneo hilo, na wengi wao wakajeruhiwa. Wengine waliokota silaha zao na kusimama.

"Mlete Chaim hapa," Rayford alirudia huku akinyosha kidole kwenye sakafu kando na alipokuwa ameketi. "Hivi sasa!"

Mtetemeko mwingine uliwaangusha wote waliokuwa wamesimama. Wakati huu Dangchao alianguka vile vile. Kamera za waandishi wa habari waliokuwa werevu na kubaki pale chini zilimnasa katibu mkuu akianguka mbele ya Shahidi wa Magharibi. Rayford alikaa kwa utulivu huku miguu yake aliyokunja ikiwa mbele.

"Sawa basi! Sawa basi!" Dangchao alisema, huku akijaribu kusimama na kumtazama Rayford.

"Mleteni yule mateka!" alimuamuru mmoja wa walinzi wake, na yule mtu akaenda kwa haraka.

"Usijali utapata fursa yako,"Rayford alisema. Hivi karibuni. Lakini kwa sasa utapata matatizo usipomleta Chaim kwangu."

"Mpige risasi!" Dangchao alipaza sauti, kadiri alivyoweza. Lakini wakati huo, Rayford alipumua tu, na miale ya moto mkali ikatoka kumuelekea Dangchao. Waliomuasi Yesu walikimbia lakini hawakukosa miali hiyo, miali ile iligawanyika katika ndimi na kuelekea kila upande. Huku ikienda mbio kuliko mtu yeyote, ndimi zile za moto ziliwafikia kila mmoja wa askari aliyekuwa na bunduki iliyomuelekea Rayford. Wote waliteketea kabla ya kudhubutu kulenga bunduki zao.

"Haupaswi kunifanya nitende hayo," Rayford alimuambia Dangchao kwa upole.

"Mipango yako ni ipi?" Dangchao aliuliza, huku akiwa na wasiwasi. "Iwapo utanihakikishia kwamba hautawacha mji huu nitamuachilia rafiki yako ili muende naye."

"Utamuachilia rafiki yangu bila masharti," Rayford alimjibu kwa upole. "Lakini iwapo itakuridhisha.hatuna mpango waa kuondoka mjini kwa siku kumi zijazo."

Hapo ndipo Chaim alitokea na yule askari.

Dangchao hakuwa na lingine ila kusalimu amri ya wale Mashahidi wawili; lakini baadaye siku ile wale waganguzi wake walifanya isikike kama kwamba wale wanaume wawili walikuwa wamewachiliwa kwa dhamana wakingojea kutolewa kwa hukumu. Kulikuwa na manung'uniko mbona kumwachilia gaidi aliyekuwa na uwezo wa kuteka nyara ndege na mshukiwa wa mauaji kuwachiliwa warandarande hivyo; lakini Dangchao alisisitiza kwamba kila kitu kiko sawa. Kwa hakika ilikuwa. ila tu hakuwa ni yeye aliyekuwa akiendesha hali hiyo ya usawa.

Siku sita zilizofuata, Cham na Rayfoord walichukua muda mwingii karibu na Hekalu la Mlima, walipokuwa na fursa ya kuhutubia umati wa watu. Ilikuwa ni mwanzo wa mwezi wa Desemba, na hali ya hewa ilikuwa na baridi; Lakini wale Mashahidi wawili waliendelea kulala mitaani, huku wakilala kwa zamu. Walikuwa wamekusanya vipande vya nguo na kuni za kutosha, na viungo vingine kuwakinga kutokana na baridi. Waliwasha moto usiku kucha karibu na eneo walilo lala. Yeyote ambaye hakulala, alitengeza moto na kuwahutubia watu.

Usiku kucha watu walikuja kuwaona na kusikiza waliyokuwa wakisema kukashifu Dangchao na wale waliokuwa wakimuabudu. Mara mbili mtu alijaribu kuwaingilia, na mara mbili mshambulizi alikuwa ameangamizwa kwa moto. Ujumbe ulisambaa kupitia vyombo vya habari na haraka zaidi kupitia kwa wale waliokuja kushuhudia; kiasi kwamba umati haukudhubutu kuuliza maswali kuhusu Mitume wawili baadaye.hadi jioni ya Jumatano.

Rayford na Chaim walikuwa hawajapata kuwasiliana na wenzao watakatifu tangu waingie Yerusalemi siku kumi zilizopita. Hawakula sana lakini waliomba sana mara kwa mara siku zile za mwisho. Wakristo wote walifahamu kwamba nyakati za mwisho wa Chaim na Rayford zimewadia. Kulikuwa na vifo na kurudi nyuma miongoni mwa wafuasi wao kipindi hicho cha siku kumi.

Irene na Elaine walikuwa wamenaswa na mamlaka na kisha kuuawa wiki moja baada ya Rayford kuondoka London. Watakatifu fulani pale Yerusalemi walikuwa wamewaeleza wakati wa wiki ile ya mwisho. Ujumbe kuhusu mauaji ya Irene ulimuongezea Rayford uchovu; lakini hakukoma kuhubiri.

Matayo alikuwa amebaki kuwatunza wafuasi wa Makabila Kumi na Mbili na Msukumo wa Mahangaiko baada ya kupotea kwa Irene na Elaine; lakini fikira kuu ilikuwa ni kwamba mambo yanaenda mrama. Tulibakia tu na siku nne tangu muda uliosubiriwa kurudi kwa Yesu kufika.Iwapo hesabu yao ilikuwa sahihi, na wengi walihofu iwapo watadumu zile siku na viongozi wao.

Basi, Jumatano jioni ya ile wiki ya mwisho, mmoja kati ya wale askari wawili wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakiwachunga wale Mashahidi Wawili, kwa kimchezo tu alichora mduara kwa Rayford akitumia mtutu wa bunduki, kwa mzaha tu. Alikuwa amesimama mahali Rayford hakuwa anamuona, na Chaim alikuwa amelala kando ya moto. Hapo tu ndipo yule mwenzake alimfikia ghafla na kumshtua huku bunduki ikifyatuka, na kumpiga Rayford kichwani. Rayford alianguka chini.

"Umemua!" Yule mlinzi mwingine alisema. "Tazama umemuua!" Na kisha kumuona Chaim akitaka kuamuka. "Harakisha! mpige huyo mwingine kabla ya yeye kukuchoma!"

"Ni yeye au mimi, au sio?" askari yule alisema huku akilenga bunduki kwa mara nyingine. Na Chaim halikadhalika alianguka karibu na Rayford. Alikuwa ameuawa kwa kupigwa risasi kichwani.

Rayford alikuwa amekamilisha hotuba yake kwa umati mdogo kabla ya kupigwa risasi, na umati ulikuwa unaondoka tu wakati wa kupigwa risasi. Wale wachache waliobaki pale na kuona Rayford akianguka kisha Chaim, hawakuamini macho yao. Baada ya miaka mitatu na nusu bila mafanikio wakiwindwa na utawala, na kisha baada ya kushindwa kuwaangamiza, askari mmoja alifaulu kuwaua wote, kwa ajali, kisha kwa sekunde na risasi mbili tu!"

Wale askari wawili walikimbia kudhibitisha kwamba, kweli walikuwa wameua wale Mashahidi Wawili, na kisha kuwaarifu wakubwa wao. Ambalanzi ya kijeshi ilikuja mbio kuokota miili ile pamoja na askari wale, na ujumbe kuenea duniani kupitia kwa vyombo vya habari kwamba ulimwengu ulikuwa umeokoka; wale Wakimbizi Wawili (kama alivyozoea kuwaitaPius) walikuwa wamekufa.

Dangchao alikuwa ameamka akihutubia waandishi wa habari huku akipanga mipango mingine. Asubuhi ile alizindua kijengo cha kikatili kilichokuwa kimezingira miili ile ya Mashahidi Wawili. Walikuwa wamerejeshwa mahali walipouawa. Vigae vya moto vilikuwa vingali pale, na vile vifaa walivyookota kuwapa joto vilikuwa vimetapaka pale. Watu walikaribishwa kujionea wenyewe. Wale askari waliotekeleza mauaji yale walitumiwa kuzuia na kuongoza umati wa watu.

Dangchao aliamua kuweka miili hiyo hapo nje ili wakristo wasilete hadithi nyingine ya kufufuka, kama walivyofanya na Yesu wao. Alitaka pia watu kujionea kwamba ni wale Mashahidi wawili waliouawa, na hakika walikuwa wamekufa.

Alisonga hatua mbele zaidi, Krismasi ilikuwa wiki chache tu ili iweze kuadhimishwa., hata ingawa ilikuwa imebadilishwa jina na kuitwa Winterfest, miaka iliyo tangulia, alihisi kwamba huu ulikuwa wakati bora kubali tarehe ya maadhimisho. Alitangaza kwamba siku inayofuata, Ijuma, itakuwa ni tarehe mpya ya kuadhimisha Winterfest. Maduka yote yatakuwa wazi, Ijuma hiyo, katika pilkapilka na heka heka za ununuzi wa mwisho; lakini afisi na maeneo yasiyo ya dharura yatafungwa Alhamisi na Ijuma. Hii ilitoa fursa kwa watu kununua zawadi, vyakula, vinywaji, na siku mbili za kusherehekea. Maduka ya jumla yalipata na kushuhudia wateja wengi sana katika siku hizo mbili kuliko walivyopata kuona. Kila mmoja alifurahi.

Watu waliamini kwamba kizazi cha binadamu kilikuwa kimebadili mkondo. Amani na maendeleo yangalirejelewa! Hivyo basi walinunua vitu na kusherehekea ushindi wa binadumu juu ya "Wageni".

Sherehe zilianza siku ile na kuendelea siku mbili zilizofuata. Jumamosi jioni maduka yote yalipokuwa yamefunga na wafanyikazi kuruhusiwa kuenda kusherehekea, ulimwengu mzima ulikuwa katika maafa ya ulevi.

Lakini jumapili asubuhi kitu cha ajabu kilitendeka Mashariki ya Kati. Ukanda mzima wa maili kumi na tano kuelekea Baghdad, Cairo na Ankara), watu walipotazama juu, waliloona ni kama kio juu kabisa ya ardhi, kio kilichotambaa kila pembe za dunia. Mwangaza ulipenya ndani ya kio kile na kuwafanya kuona vitu vikisonga upande ule mwingine.

Ndege zilizokuwa zikiendeshwa juu ya futi 25,000 zililazimika kutua au kurudi zilipokaribia Mashariki ya Kati.

Dangchao alikutana na washahuri wake waliomuarifu kwamba ilikuwa ni nyota iliyokuwa ya kigeni. Swali kuu lilikuwa iwapo wale walinzi waliokuwa wakiitunza nyota ya kigeni ile walikuwa wazuri. Dangchao alibahatisha kilichokuwa kule juu na kuwaonya wachukue tahadhari.

Kisha, mchana, kulikuwa na mabadiliko katika Hekalu la Mlima. Mtu mmoja alisema aliona mkono mmoja wa wale Mashahidi ukisonga. Dangchao alishangaa na kukimbia katika eneo lile, kwa pamoja na umati uliojumuisha waandishi wa habari.

Kila mmoja aliyekuwa pale alitazama kwa dakika tano bila kuona dalili yoyote. Walipokuwa tayari kufutilia mbali habari ile kama fikira ya uongo, walioana mwili wa Chaim ukitetemeka.

"Uliona hilo?" Mtu alisema. Kwa hakika Dangchao alikuwa ameona, na kushikwa na hofu.

"Mpige risasi!" alipaaza sauti huku akinyosha kidole kueleka kwa Chaim.

"Lakini tayari amekufa!" mlinzi wake alisema. Yeye pia alikuwa ameogopa. Alikuwa amesikia yale yaliyowafika wote wale waliojaribu kuwalenga Mashahidi wawili.

"Sijali kama amekufa au la. Mpige risasi!" Dangchao alisema kwa hasira. Alinyakua ile bunduki kutoka kwa mkono wa yule mlinzi, katika juhudi za kutekeleza mwenyewe. Aliielekeza kwenye kichwa cha Chaim na kufinya ili kuwachilia risasi. Lakini alipokuwa akifanya hivyo, alipata msukumo kutoka kwa ardhi na risasi zake kuelekea upande mwingine. Alirusha mikono (na bunduki) juu hewani ili kupata kusimama wima. Mahali pale pakaanza kutingika na ile miili pia ikatetemeka.

Mtetemeko wa ardhi! Dangchao alifikiri. Kumbe ni hiyo miili ile haikutingika! ilikuwa ni ardhi iliyozitingisha.

Lakini baada ya muda mchache, mikono na miguu ya Rayford na Chaim ilianza kunyooka. Miili yao ikajipinda, na mikono yao kuinuliwa ili waweze kuamuka. wima kwa miguu yao. Walikuwa wameinama huku wakifungua macho yao na kutazama wapotevu.

Lile kovu la risasi lilipotea mara moja mbele ya macho ya Dangchao. Nywele zao ziliimarika huku mvi ukipotea mikunjo usoni ilipotea, na walionekana kama waliokuwa chini ya umri wa miaka thelathini. Matambara ya nguo walizokuwa nazo ilitoka na kuwacha kanzu safi nyeupe.

Wale wanaume walisimama wima huku sauti ikisikika kutoka mahali wasipoona na kusema: "Kujeni huku juu!" kila mmoja alitazama juu na, chini ya kile kio kilichokaribia juu ya Hekalu la Mlima, mlango wa mduara ulifunguka. Lakini "moshi" ulipokaribia, ulitawanyika na kuwa mamilioni ya viumbe wadogo walio na mavazi meupe. Katikati yao kulikuwepo na mmoja aliyeng'aa kiasi cha kusababisha upovu. Wale viumbe wengine walimzingira huku akikaribia chini.

Chaim na Rayford walianza kupaa ili kuwalaki viumbe wale, walipokuwa wakipaa, walishuhudia wengine wengi kutoka katika ardhi wakipaa na kuzingira Kiumbe Kilichokuwa na Mwangaza.

Wale wengine walikuwa wanang'ara na mavazi ya ufufuo, lakini kulikuwa na wachache walio tambuliwa kutokana na nguo zao za kawaida. Hawa walikuwa ni watakatifu waliokuwa hai. Hao pia walikuwa na sura mpya ya ujana. Kovu na aina yeyote ya ulemavu ilipotea. Yeyote aliyekuwa kati ya umati huo alihisi furaha na kujisikia mwenye afya, na habari njema ilikuwa ni kwamba hakuna aliyekosa mkono.

Chini ya ardhi, mtetemeko ulizidi, sasa kwa kasi muno. Mji mzima wa Yerusalemi ulikuwa ukitingizika. Majengo yalianza kuanguka. Kutoka juu walipokuwa wateule ilionekana kama kwamba mji wote ulikuwa ukianguka polepole. Lakini pale chini kulikuwa na garika ya vio, chuma, matofali, vigae na aina nyingi ya vifusi kutoka kwa majengo yaliyokuwa yakiwaangukia wakaazi. Watu waliokuwa wangali wanasherehekea walinaswa na kuangukiwa na majengo kote Yerusalemi.

Wateule walikuwa kule juu pasipo hewa ya kutosha na hali ya baridi, lakini hakuna hata mmoja aliyehitaji kifaa cha kufunika mapua au mwili, walikuwa salama, bila mahangaiko.

Viumbe vyote vilikuwa vikizingira Kile Kiumbe Cha Mwangaza. Rayford na wateule wengine waliozingira Kiumbe kile walifahamu ni nani. Alikuwa ni Mwokozi wao. Alikuwa ni Yesu wao!

Mtu mmoja alianza kuimba na wale wengine wakajiunga. Kila mtu alikuwa akiimba kwa lugha yake, lakini walihisi kwamba walikuwa wanaimba maneno sawa. Yalikuwa ni maneno na nyimbo kutoka kwa Nyimbo za Hallelluya za Handels Masia "Mfalme wa wafalme! Bwana wa mabwana! atatawala milele na milele!"

Walikariri na mara kwa mara; na kila mara sauti iliongezeka, hadi ilipodhaniwa kwamba dunia nzima ingalisikia Hii ilikuwa ndipo! Huu ulikuwa ni wakati ulio tazamiwa na kusubiriwa. Ilikuwa ni kilele cha mipango ya Mungu kwa viumbe wake.

Alikuwa amerudi, kwa hakika. kuhukumu ulimwengu!

Zion Ben-Jonah Aandika

Kuna kitu kuhusu kurudi kwa Yesu kinachoonekana kama sio kweli kwa ulimwengu huu wa sasa. Na hakika sio cha kuaminika kama miiko na hekaya zingine (Ikiwemo jinsi viumbe walivyoumbika) vile binadamu alivyoumbika. Bila hicho, maisha hayatakuwa na dhamani-- ajali tu katika supu ya kiuongo kijulikanacho kama ulimwengu.

Lakini mbona tusiamini Bibilia inavyotueleza kuhusu kurudi kwa Yesu, juu ya maelezo mengine kuhusu maisha na uhai? Kila kitu kinaeleza Bibilia kama kitabu cha historia kinachoweza kuaminika; na kizazi cha binadamu kufaidika zaidi kuliko kitabu chochote kuwai kuandikwa Twapaswa kutenda mema kinavyoeleza huku tukingoja kurudi kwa Yesu.

Tukio hilo kubwa limeelezwa katika njia tofauti na waandishi. Paulo anatabiri kuhusu Mpasuko katika Wakorinzo wa I 15:32-58. Anaanza kwa kusema, "Iwapo maiti hawatafufuka, basi tule na kunywa kwani kesho tutakufa." Na kumaliza kwa maneno haya ya kutia moyo: "Mjue kwamba kazi mnayo fanyia Bwana sio ya bure." Hivyo basi kuna sababu ya kuishi. Yeye atarudi. Tutainuka tena.

Ufunuo wa Yohana 11:7-13 inaongea kuhusu kufa na kufufuka kwa wale Mashahidi wawili, na pia mtetemeeko wa ardhi uliokumba Yerusalemi wakati huo. Huu mlio wa saba (mwisho) wa tarumbeta unaadhimisha mwanzo wa adhabu ya Mungu, au kufunua kwa ndoo ya saba.