Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

7. Wakimbizi

Licha ya uchovu na kisunzi na shida nyingine za safari, Irene Straight aliweza kuendesha kwa muda bora kuelekea kaskazini alipokuwa amewacha wanakambi wengine Kaskazini mwa Dakota. Aliendesha mbio usiku kucha na kuwasili mchana siku ya Jumamosi.

Mamlaka ya nchi ya Canada ilikuwa ikichukua maelezo kutoka kwa wakimbizi waliokuwa wakija na kuwaelekeza kwenye kambi. Tom na Betty na wajukuu walidhibitishwa kuhitaji matibabu ya dharura kuliko Irene na Reymie, hivyo basi waliingia kwenye basi na kuelekea Regina ili kupata kutunzwa vyema.

Usafiri ndani ya nchi uliwekewa vikwazo kote nchini Canada. Irene hakuwa na fedha, ombi lake kuenda Toronto lilikataliwa. Kulingana na mamlaka, Toronto ilikuwa imepata wakimbizi wengi kupita kiasi. Irene na Reymie walielekezwa katika kampi iliyokuwa katika barabara kuu ya kuelekeaRegina na Winnipeg. (Waliweza kuwacha Lincoln kwenye mpaka). Kampi hii ilikuwa kati ya zile nyingi zilizokuwa zikitengwa kutoka kwa mashamba kila mahali kusini mwa Canada.

Irene na Reymie walipaswa kungojea hapo hadi tuwe na utulivu Toronto, au hadi watakapochukuliwa kwa ndege nje ya Saskatchewan. Wote walikuwa wakipoteza nywele na kukosa maji kutokana na kutapika, lakini hawakua wagonjwa kama watu wengi kwenye kambi. Kambi ya wakimbizi ilikuwa na maelfu ya mahema ya futi kumi na mbili mraba, kila hema likiwa na watu wanane. Kila baada ya mahema manne kulikuwa na chumba cha kuogea. Ndoo kwenye vyumba ilitumiwa kama choo wakati vyumba hivyo vilikuwa vikitumiwa kwa wingi au wakati wa hali mbaya ya hewa. Eneo la shamba palikuwa mahali pa kuchukiza kutokana kiasi kikubwa cha mvua ya hapo awali na pia kutokana na msongamano wa watu wanaotembea kupitia hapo.

Wakimbizi walishahuriwa kubaki ndani ya kambi kuzuia maafa. Wahudumu wasio na ujuzi walileta madawa mara mbili kwa siku. Dawa hizo zilikuwa pamoja na zile za kisunzi, kuendesha. Halikadhalika maji na chakula. Visa vya dharura vya magonjwa ndivyo vilivyoripotiwa kwa wauguzi waliohitimu. Katika eneo lililotumiwa kama zahanati, tulikuwa na madaktari wawili na wauguzi wachache. Maisha yalikuwa magumu kwenye kambi hiyo licha ya uvumi kwamba hiyo ndiyo ilikuwa kambi nzuri kushinda nyingine yeyote.

Shirika la ndege la Pan-continental lilijulishwa kuhusu hali ya Reymie na Irene na Pan-con kupitisha ujumbe kupitia kwa Rayford. Jamii hiyo haikuwa na la kufanya ila kungojearuhusa ya kwenda kuungana na jamii.

Kwa sasa Irene na Reymie walisadiki kwamba wanapata chakula bora na maji safi, na pia kambi bora iliyo na mahali pa kupumzikia, kulala na kuwa na matumaini. Hapakuwepo na uwezekano waRayford kuwasiliana nao moja kwa moja, na kwamba simu za dharura za kuenda nje ndizo zilizokubaliwa ndani ya kambi.

Kwa wakati fulani, Reymie alikuwa akifikiri kuhusu hali ya maisha. Maisha yalikuwa mabaya hata kushinda gereza au korokoro mbovu Kaskazini mwa Amerika. Lakini kwwa muda wa wiki mbili alikuwa mgonjwa kufanya lolote ila kuguna kwa maumivu. Hadi tu alipopata nguvu ndipo alipoanza kulalamika. Irene alikimia na kunyamaza kuhusu shida zake, huku akimjulisha mara kwa mara jinsi walivyonusurika. Lakini Reymie alikuwa akijaribu kuvunja tabia za kitambo. Ilikuwa kama kwamba roho yake ilikuwa ikingoja Irene kupata nguvu na busara ya kuimiliki. Ni wazi kwamba katika ulimwengu yale yanayopuuzwa ndio husababisha maafa. Kwa jumla, Raymie alilazimishwa kukua katika muda mfupi, na kwa haraka alikuwa akijaribu kuishi katika hali hiyo mpya ya kuwa mtu mzima mwenye utu-bora.

Jamii ya watu wanane katika kila hema waliongea na kufanya kazi ndogondogo kwa wale waliokuwa na nguvu. Mengi ya mazungumzo yalikuwa kuhusu kile walichofikiria juu ya yale yaliyotokea, na muelekeo na madhara kwa jamii zao. Kila mmoja alikuwa na huzuni na maombolezi kwa kupoteza rafiki mpendwa au jamaa yake, hata hivyo wengi walidhani kwamba baadhi ya jamaa zao walinusurika shambulizi

Mtandao wa habari na mawasiliano katika U.S. ulikuwa umeharibiwa muda mfupi baada ya shambulizi.

Licha ya kukosa magazeti katika kambi, wahudumu fulani walipata habari au ujumbe kutoka nyumbani, na kuwaarifu wakimbizi waliporejea kwenye kambi. Kutoka hapo ujumbe wa mdomo ulienea kwa haraka.

Wakaazi walijua kwamba Umoja wa Mataifa ulikuwa umeanda jinsi ya kutunza misaada. Katika majuma machache yajayo, manusura wa Amerika wataanza kusambazwa kote ulimwenguni kutoka kambi za Canada na Mexico na sehemu za Amerika. mahali pa kuchukuliwa kwa ndege katika sehemu zilizo na uwezo wa ndege kutua.

Hali ya anga ilikuwa shuari, kwa upepo wenye utaratibu uliopita juu ya Atlantic. Upepo ulisukumwa kusini mwa nje ya Canada baada ya shambulizi. Hata hivyo viwango vya miali ya jua vilikuwa juu hasa kusini mwa Canada, juu kuliko ilivyotarajiwa. watu wa Canada walihimizwa kubakia nyumbani. Ulimwengu kwa jumla na visiwa vya Caribbean na sehemu za Mexico hazikuadhiriwa kwa miali hiyo.

Nchi ya Urusi ilichukulia hali ya vita hivi kama kwamba havikutokea. Baada ya wanamgambo wake kulipua makombora kwenye kambi za kijeshi na sehemu nyingine muhimu za umeme na mawasiliano, walirudi kwenye maskani yao. Kutokea hapo Russia ilitoa misaada kwa manusura kama taifa lengine lolote.

US. na Uingereza walikuwa wametimuliwa kutoka kwa umoja wa mataifa siku chache baada ya shambulizi. Amerika ilitimuliwa kwa kuangamizwa ilihali maelezo kuhusu Uingereza kutimuliwa hayakutolewa. Licha ya malalamishi kutoka Uingereza, hatukuwa na pingamizi kutoka kwa jamii nyingine za umoja huu. Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Xu Dangchao, kwa kuungwa mkono na Russia na China katibu huyu aliweza kusuluhisha kwa wepesi. Kutimuliwa kutoka kwa uanachama haukufuata na kuwekewa vikwazo. Hata hivyo watu wa Uingereza walipuuza na kuendelea kusaidia Amerka. Uingereza haikutaka kubishana kutokana na tofauti ya mawazo.

Kupotea kwa nafasi ya kibiashara na Amerika ilikuwa tisho kwa mataifa mengi maskini, lakini Umoja wa Mataifa ulianzisha juhudi za kutaka kuchukua sehemu zilizomilikiwa na Amerika na kuanza kutayarisha mashamba ili kukidhi uhaba wa chakula. Katibu wa Umaja wa Mataifa bwana Dangchao aliahidi kwamba atasaidia mataifa yanayostawi, na ajabu ni kwamba Banki kuu duniani iliunga mkono azimio hilo.

Mkutano mkuu ulipangiwa kufanyika kuhusu hali ya uchumi wa dunia. Mojawapo ya maswala ya kujadiliwa ilikuwa ni matumizi ya sarafu moja.

Jambo moja au mradi wa umoja wa mataifa ambalo halikushughulikiwa kama mambo ya fedha na siasa ilikuwa jumuia ya madhehebu. Dunia nzima watu walitaka hakikisho kwamba janga la USA lisirudiwe tena. Wakuu wa madhehebu walishanga kuona tofauti zilizowagawanya hapo awali zikitokea. Hao pia walitaka kujumuishwa katika kuleta amani duniani na umoja.Umoja baina yao na pia umoja wa kitaifa. Wakati wa dhiki au shida, watu wengi hukimbilia vituo vya dini kwa msaada: hivyo basi ni muhimu kwa serikali, kanisa, sinagoji na misikiti kutoa ishara ya umoja na matumai.

Hatukua na ujumbe au risala kutoka kwa rais Fitzhug, ambaye kwamba yeye na familia yake pamoja na wasaidizi wake walikuwa wametekwa nyara ndani ya Ikulu ya White House kutokana na shambulio. Matumaini yao kama manusura yalizidi kudidimia, licha ya kuwepo vyumba na njia za kuepukia mikasa. Tulikuwa na njia ya kuapisha rais mwengine. Hata hivyo wale ambao walihitimu kama vile makamu wa rais na wagombeaji wengine walikuwa wametoweka au kufa, na pia na idadi kubwa ya maseneta na wajumbe wa bunge la chini. Wachache waliokuwa hai walikuwa wakimbizi. Kwa hakika, Amerika ilikuwa imeangamizwa kama taifa huru.

Taifa hili lilikuwa imara kutokana na kuunga mkono Israeli. Taifa hilo ndogo la Israeli lililozungukwa na mataifa ya kiarabu lilikuwa na wasiwasi kutokana na tukio hili. Lakini Dangchao alishangaza ulimwengu na kupata sifa na heshima kwa kuendesha mazungumzo ya amani kati ya Israeli na nchi za Kiarabu. Iliaminika kwamba uwezo wa wayahudi katika Banki ya Dunia ndio chanzo cha kufaulu kwa Dangchao. Alipata mabilioni ya dola kutoka kwa Banki ya dunia ili kusaidia mataifa maskini.

Jambo la kutisha kwa mamilioni ya Waamerika walikuwa wakijaribu kuepuka kifo na janga lililokumba taifa hili. Maelfu ya watu waliendelea kufa kila siku kutokana na yale majeraha na shida nyinginezo kutokana na mlipuko. Wengi walikufa kwa kukosa madawa, aidha waliwachwa mahali hadi pale watakapo kata roho. Wale manusura waliobebwa kwa gari walikufa wangali njiani au hata kwa kufikishwa hospitalini au kwenye kambi. Mazishi halikuwa jambo la kawaida. Kuchoma maiti ilikuwa rahisi na haraka, na kwa kiasi kikubwa maiti iliwachwa kuoza, na magonjwa kusambaa.

Kwa watu kama Chloe, waliokuwa wakingoja msaada kuwafikia, hatari ya kupata kipindupindu iliongezeka.

Zion Ben-Jonah aandika

Alama mbili zatumiwa kuashiria Amerika katika unabii wa Bibilia. Kahaba aliyejulikana kama Babeli, na mabawa ya mwewe na kiwiliwili cha simba (Simba akiwa ni Uingereza.) (Tazama maelezo baada ya sura ya 2)

Kitabu cha Danieli 7:, mabawa ya mwewe yamenyanyuliwa, na simba (yaani Uingereza) sio "jitu" (au babe la dunia) hatimaye. Katika Ufunuo wa Yohana 17:16-18, na Ufunuo wa Yohana 18 kwa jumla, tunasoma juu ya kuanguka kwa Babeli na jinsi kulivyoadhiri wafalme, mabepari na manuari duniani.

Kumbuka kwamba neno "Babeli" halimaanishi tu Amerika. Ni ishara ya utawala wote wa binadamu. Hivyo basi jina litapitishwa kwa taifa lenye uwezo mkubwa wa kifedha katika mpangilio mpya.

Kuibuka kwa dini au dhehebu moja duniani hakuwezi kusaidiwa na Umoja wa Mataifa. mazungumuzo kuhusu dhehebu la dunia yamekuwa yakiendelea; lakini shida na majanga hufanya watu kufikiria juu ya jambo hili.

Ubeberu na ubabe wa Amerika pamoja na Israeli huelezwa kwa wingi (hata kwenye kanisa), kwa kufahamu kwamba ni wateule wa mungu (Licha ya kukata na kumkana Mtume wa Mungu Yesu Kristo!). Hata hivyo, kivutia cha Israeli katika viwango vya serikali ni kupata uwezo wa kumiliki banki kuu ya dunia.