Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

6. Kuhesabu Gharama

Rayford aliangalia juu ya gari la Leyland Dal. Lilikuwa limejaa, Watu wanne kwenye sebule, lakini sio msongamano kama alivyotarajia. Daftari ilijumuisha vifaa vya mbao. Kulikuwa na mahali pa kila mmoja kulala na pia kuketi. Kila kitu kilikuwa kimewekwa vyema. Kusonga au kupita katika sehemu moja hadi nyingine ndani ya gari hilo haikuwa rahisi, hasa iwapo mmoja alikuwa akipika au kuosha vyombo katika eneo ndogo la jikoni.

Karibu na Rayford, upande wa nyuma wa gari hili, alikuwa ameketi kijana mwenye umri wa chini kwenye kundi hilo aliye na miaka 24 kwa jina la Martin. Jamii ya Martin ilitoka nchi ya Czech. Upande mwingine kinyume na Rayford, kulikuwepo Reinhard na Francisco. Reinhard alikuwa na miaka 32, ilihali Fransisco alikuwa na umri wa miaka 28. Mama ya Frans alitoka Argentina. Wote watatu hawakuwa wamefuzu taaluma yoyote licha ya kuelewa lugha nyingi lwa ufasaha. Kwa pamoja walikuwa wametafsiri Kuangamia kwa amerika kwa lugha ya Kifaransa, Kijerumani, Kiispania, Czech, Kirusi na hata Kipolishi.

"Je, kwa wiki moja mnapata vingapi," Rayford aliuliza, huku ameshika nakala moja ya kitabu kilichomvutia.

"Maelfu katika wiki nzuri", Martin alijibu. Martin alikuwa mkuu wa takrimu. Yeye ndiye aliyetayarisha makadirio ya kifedha kwaniaba ya kundi hilo.

"Hiyo ni 1000,000 kwa mwaka," Rayford alisema.

"Mwaka bora," Martin alimjulisha.

"Chochote. Jambo ni hata mwaka mbaya, mtapata wanachama wengine. mbona nyinyi ni watatu?"

"Sababu mbili," Fransisco alijibu, aliyeonekana mwenye uwezo na mali kuliko wale mamishionari wengine wawili. Mikono yake ilichezacheza, na kutingisha kichwa kana kwamba kichwa kilivuta kamba mkononi. Kutikisa kwa kichwa ilikuwa ishara ya kutoka kwa wazo fulani hadi lingine.

"Tunayo hubiri.hasa, watu hawasikii. Wajua, wanataka wahubiri kuwabembeeeleza." Alikariri na kulivuta neno kuwabembeleza. "Tunaongea juu ya kifo hapa. kutuandama sote. Namaanisha kutoa kila kitu kwa Mungu! Nani anataka kusikia hayo?"

"Sababu gani nyingine inayowafanya watu wasijiunge nanyi?" Rayford aliuliza.

Reinhard alijibu. "Twatumai kwamba Mungu amatuficha chini ya waumini wa hakika. Hao pia wanajificha tusiwaone. Siku moja tutakuja pamoja. Kwa sasa, tunajaribiwa kuona kama tutadanganya au kubadili ujumbe wetu."

"Mmoja akipanda mmea, mwingine hunyunyiza." Fransisco alirudia. "Mavuno yatawadia. Hakuna wasiwasi. Kwa sasa wanasoma. Wanafikiria. Na lo, wanazungumza juu ya hayo. Watu hutueleza.kil siku!"

Rayford alitamani mawazo ya watatu hawa; lakini hakuamini kwamba wengine hawakujiunga nao licha ya utabiri wao kuhusu Amerika kuonekana na kutimia. Na akasema hivyo.

"Kwa haraka watu husahau," Reinhard alieleza. Wanapuuza pia. Ikiwa wanasema kwamba kitabu chetu kiliandikwa baada ya shambulio."

"Lakini ndani ya mioyo yao wanajua!" Fransisco alieleza. "Wanajua basi! Ukweli umo kwenye vitabu, kupita kama bomu lililotunguliwa. Siku moja uwazi utajitokeza.Na kisha. Ka-PWA!" Alipiga makofi kutoa hiyo sauti na kisha kubeba mkono juu ya hewa kama roketi. Nyuso zote tatu ziliangalia kwa kukubali yale aliyoyasema Fransisco.

"Hatuongezeki kwa idadi; lakini ukweli unadhihirika," Kufanikiwa mbele ya Mungu ni bora kuliko kufanikiwa tu."

"Lazima uelewe," aliendelea Reinhard, "Sisi huamini tunapozungumzia juu ya mbingu na Mungu, na kuhusu kurudi kwa Yesu. Imani hii hubadili fikira zetu kuhusu vitu vingine. Tunaishi katika ulimwengu mpya. milele. Imani yetu sio ile imani ya kanisa."

Hayo ni mawazo makuu! Rayford hakuamini kwamba watu wa ajabu watatu wanaoishi kwa umasikini wangali mshawishi. Ili hali walikuwa wakifanya hivyo. Ukweli ni kwamba hangaliwapatia nafasi ya pili pasipo shambulio la Amerika. Gharama gani hii juu ya Mwenyezi Mungu kwake kusikiza kwa makini! Watu wengi kote ulimwenguni walikuwa wakitafakari kuhusu uchumi na wala sio hali ya kiroho inavyozidi kudidimia nchini Amerika.

Rayford alibakia akiongea kwa muda. Aliwatumbuiza kwa chakula moto ndani ya mkahawa wa kituo cha Heston. Kwa wakati huo alifahamu kwamba watatu hao waliegeza gari lao usiku katika vituo vya kurekebisha magari, kutokana na hali isiyo ya wasiwasi au hata kushukiwa hata kwa saa 24 kuliko kuegesha kando ya barabara. Kuegesha katika sehemu kama hizi ilikuwa ni hakikisho la kupata vyumba. Wakati wa mchana waliuza makala yao kwenye vituo vya biashara, kama walivyofanya katika barabara ya Hounslow hapo awali.

"Hatuishi mahali pamoja kwa siku mbili mfululizo," Martin alieleza. "Sio rahisi kugundua kwamba tuko hapo."

Siku iliyofuatia, Jumapili, Jesans walikutana na Rayford katika ukumbi wa Ruislip, siku yao ya kupumzika. Rayford alijuunga nao kisha kutoa mafundisho ya Bibilia na maankuli ya mchana yaliyotayarishwa na Francisco.

"Niwache kazi yangu ili niwe mkristo kamili?" aliuliza walipokuwa wanakula.

"Unachotakiwa kufanya ni kumuamini Yesu," Reinhard alisema.

"Lakini uliniambia kwamba ni kutoa yote uliyonayo, na kumtumikia muda wote!" Rayford alikuwa akirejelea mafundisho ya mlango wa kumi nanne katika kitabu cha Luka.

"Kwa hivyo fanya alivyosema," Reinhard alijibu. "Lakini usifanye tu kwasababu alisema."

"Lakini nini kuhusu familia yangu?"

"Nini kuwahusu?" Reinhard aliuliza kwa upole akikodoa macho kuonyesha hali ya kusisitiza.

"Siwezi kuwaacha"

"Kwa hivyo kuja pamoja nao."

"Unajua siwezi kufanya hivyo. Chloe ameshikwa kule Chicago, na sijui mahali alipo Irene na Raymie. Wanaweza kuwa wameuawa." Reinhard hakupinga hayo, kwani jesans walimpa muda na kumsikiza Rayford na vilevile kumhadithia kuwahusu. lakini alitaka kumuonyesha Rayford jinsi asivyo na uwezo.

Kwa mara nyingine Furaha ya Fransisco ilizidi ile ya Reinhard. Ona? unashikilia kitu usicho nacho!" alisema. "Wachilia! ukiwachilia Mungu atakuonyesha cha kufanya. Lakini huwezi kufikiria hayo kabla ya kuwachilia kwanza".

Reinhard kwa siri alimuashiria Fransisco kuondoka, na kuwacha kundi katika hali mbaya ya kimya kwa muda. Walikula bila kuongea huku Rayford akiwaza sana ndani ya akili yake. Fikira zake hazikuhusu wageni hawa. Fikira yake ilikuwa kuhusu Muumba wake.

Iwapo Mungu wetu ni Mwaminifu, aliwaza, basi Mungu anahaki ya kuwaamuru watu kuwacha familia zao, kazi, utajiri wao ili kudhihirisha imani yao kwake. Lazima ilikuwa imani kama hiyo iliyotoa uhuru kwa Reinhard, Fransisco na Martin kufanya yale waliyokuwa wakifanya. Idadi yao haitawai kuongezeka iwapo wenzake hawangali fanya uamuzi kama wake. Rayford aliona kwamba mazungumzo ya imani kuhusu Yesu yaliyopuuzwa na wafaasi sio imani tena. Lakini angalifanya nini kuhusu jambo hilo?

Tukio la hali lilikuwa limechukua nyumba na jamii yake. Kilichobaki ni kazi yake. Hata ingawa kazi ilikuwa kwa minajili ya jamii yake, na wazo la kujipatia nyumba mpya siku moja.

"Ewe Mwenyezi Mungu," aliomba. "Siwezi kumuacha Chloe. Yeye ananitegemea."

"Mungu anajua kilicho na muhimu kwako," Reinhard alisema kwa lahaja yake, kama kwamba alikuwa akisoma akili ya Rayford. "Ni bora kumchukulia kwa fikira nzito badala ya kupuuza maneno yake."

Jasho lilimtiririka Rayford. Alikuwa amesimama kando ya ukingo wa jukwa la maamuzi ya mwenyezi Mungu kama alivyofahamu. Aliendelea kuomba kwa kisiri. "Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie. Sitaki kufanya jambo la kishenzi. Kuna mengi mbele yangu. Na je, kuhusu Chloe?"

Reinhard alinena tena kama kwamba anasoma fikira zake. "Hatuna uwezo lakini tunafikiria tunao," alisema. "Kwa dakika Mungu anaweza kuchukua. Na kwa dakika anaweza kupeana. Iwapo unatumai mema basi wachilia! Wachia Mwenyezi Mungu atoeuamuzi kuhusu yaliyo bora kwako na kwa watu uwapendao."

Akili nyepesi ya Rayford Strait iliweza kukadiri ukweli wa yale yaliyosemwa na Reinhard. Alikuwa ameeleza utawala wa Canada yale aliyofahamu kuhusu familia yake. Licha ya hayo hakuwa na uwezo. Mambo muhimu yalikuwa madaraka, heshima na pesa pamoja na uhuru wa kuenda Uingereza na Canada kwa ajili ya kazi yake. Mengi ya kuacha, hata hivyo ni bure ikiwa ni mipango ya Maulana. Matukio ya siku chache zilizopita yalikuwa yamemshtua. kumuezesha kuona jinsi maisha yalivyo ya kutisha na vile ndoto zilivyo tamu. Iwapo angali sema laa kwa Maulana, ni sawa na kusema hapana kwa maisha ya milele. Rayford alikuwa ameonyeshwa ukweli wa kiroho na watu hawa, kwa hali ambayo alikuwa hajapata kuona. lilikuwa jukumu lake kutekeleza.

Hata ingawa yote hayo yalitokea baada ya shambulizi la mabomu, Rayford hakuwa amelia mara moja. Labda ilikuwa kujinyima, au kujihusisha kwa uangalifu na matukio yaliyokuwa yakitukia. Lakini machozi yalimlengalenga, ukweli wa Mungu katika maisha yake ulipomjia. Alijikaza kufuata na kutekeleza aliyofikiria kwenye akili.

Fikira na mawazo yalimpelekea kukata tamaa ya kuwacha kazi. Je atoe ilani? Akose tu kufika kazini? Aligundua kwamba alikuwa ametoaa uamuzi kufanya. Yote ili kumfuata Mwenyezi Mungu. Swali kuu ni vipi. na lini.

Rayford aliinua kichwa chake na kutabasamu, huku machozi ya furaha yakimtoka. Wenzake walielewa maana ya machozi hayo, na hasa tabasamu iliyofuatia. Fransisco aliyeketi ule upande mwingine wa Rayford, aliruka na kumsalimia. Salamu hizo zilipelekea kukumbatiana. Martin na Rainhard walingojea zamu yao kwa furaha na machozi.

Rayford alipiga simu kazini siku ya Jumatatu ili kuwaarifu. Alijulishwa kwamba Jeshi la Uingereza halingalimruhusu kuwacha kazi. Ni miezi mingi kabla ya mashirika ya ndege kurejelea safari zao, kwa sasa kila rubani na ndege walitumiwa kwa kikamilifu katika juhudi za kunusuru.

Wote wanne walijadili swala hilo na kuamua kwamba hali ya Rayford ilikuwa sawa na utumwa. hasa kwa wakati. Alikuwa ameapa kujiuzulu kwa ajili ya kazi ya Mungu, na huku hali ya wakati imemrejeshea kazi. Angalingojea hadi pale anaporuhusiwa kujiuzulu, kwa sasa angetumia uwezo wake kuomba msaada kwa ajili ya jamii yake. Akiwa London ataishi na ndugu zake wa kikristo na kuwasaidia kueneza injili kwa kuuza majarida kando ya njia.

Majuma machache yajayo, katikati ya fikira zao kuhusushida ya Amerika, Wahudumu wa Pan-Con waliona ubadilifu wa Rayford Strait. Rayford Strait alikuwa ameokoka na kujiunga na wafaasi wa Kristo. Kujitolea mhanga katikaToronto kulikuwa kwa haki, lakini London angalikutana na wanaume walio kwenye gari aina ya Daf katika uwanja wa ndege, na kurudi kwa wakati kuchukua ndege. Hali yake ya kawaida ilikuwa imempotea, na kwamba uvumi ulienea kwamba yeye anarandaranda mitaani huku akiomba.

Zion Ben-Jonah Aandika

G.K Chesterton aliwai sema, "Sio kwamba Ukristo umejaribiwa na kupatikana umeshindika. Ni ile tuu watu walijua sio rahisi na kutojaribu."

Shida katika Kanisa la kisasa ni kwamba watu wachache wamekuwa wakijaribu (lakini changamoto kwa wengi) kufuata sheria za Kristo kwa wafuasi wake. Kuna wahubiri wengi walio tayari kutueleza yale tunayotaka kusikia, yale tusiyochukua muda kusikiza kutoka kwa Bwana wetu. Iwapo maana ya Ukristo ni kumfuata Kristo, basi hatuwezi kufurahi kusema kwamba Kanisa ni la kikristo, licha ya kujihusisha na mengi kuhusu dini au dhehebu hili.

Chukua muda kupitia katika sura ya kumi na nne ya kitabu cha Luka mstari wa 25 hadi 35. Labda Yesu hakutaka tuelewe sura hiyo kwa juu tu. na labda pia alinuia hivyo. Mengi yako juu yetu lazima tuombe kwa wingi na kwa kujitolea kabla ya kutupilia mbali sura hizi.

Tunapowadia katika kutambua miujiza ya maisha yamilele na yale maisha yanayowakilishwa, utapata hakikisho kwamba tutadanganya kuhusu maagizo hayo na pia kupata kuyajua.

Siku moja Mwenyezi Mungu atakuuliza kulaza maisha yako kwake. Je, ni gharama kwako kutoa familia yako kwake, kazi, na utajiri iwapo anauliza hayo sasa?