Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

11. Mavuno ya Kiroho

"Miezi sita! Sio nafasi ya kutosha kuwafikia watu nusu bilioni, au sivyo?"

Yohana Doorman alikuwa akiongea na Raymie Straight huku wakipaa kutoka London hadi Afrika ya Kusini.

Lakini kichwa cha Reymie kilijaa mawazo mengine tofauti na hayo kwa wakati huo

Mamake-- Irene jinsi alivyokuwa akimuita-- hakuchukulia kuondoka kwake vyema. Hakufikiria kwamba yu tayari kwa jukumu kama hilo; lakini Rayford.(Raymie alifurahi kuwaona wazazi wake kama ndugu na dada katika Yesu.) Rayford alikuwa amemtetea Raymie, huku akimjulisha Irene jinsi kijana huyo alikuwa amekomaa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.

Raymie alimkasirikia Irene. Alijua kwamba alimdhania kuwa yule kijana mdogo, Lakini alifurahia kwamba babake alimuamini hata akiwa mchanga, na alitaka kutimiza jukumu hilo.

Hapa hivi yeye akiwa na umri wa miaka kumi na mitano na mshahuri mkuu wa wale mahakimu kumi na mbili duniani. Nani angaliamini kwamba kijana mpotovu kabla ya kuangamia kwa Amerika angaliweza kuwa na cheo mashuhuri kama mkuu wa kikundi kikubwa cha kidini duniani.!

Maneno ya Rayford yalimrudia. "Waweza kutimiza, Raymie, mradi tu unaelewa na kukumbuka kila hatua ya jinsi usivyoweza kutimiza. Sio bila msaada wa Mungu."

"Unisaidie nikumbuke hayo," aliomba kwa mara ya miamoja tangu aanze kujianda kusafiri pamoja na Yohana.

Yohana Doorman hakujaliwa kupata watoto. Hata alikuwa hajawai kuoa. Lakini alimpenda Raymie, na kuonyesha mapenzi na dhihirisho la kushahuri kijana. Hiyo ndio iliyokuwa sababu kwa Rayford kumuachilia Raymie awe pamoja na Yohana. Kwa pamoja Raymie na Yohana walikuwa na jukumu la kutafuta wafuasi 12,000 halisi katika mataifa yaliyo fanya Afrika Kusini na Afrika ya Magharibi.

Wazo la Yohana lilikuwa ndani ya akili ya Raymie, na mara moja Raymie aliitikia.

"Ndio. Ni kazi kubwa sana, ama sivyo?" alisema. "Lakini kumbuka kwamba twaweza kufanya? Tunaweza fanya iwapo tutakumbuka kwamba hatuwezi kufanya bila usaidizi wa Mwenyezi Mungu."

Yohana alitikisa kichwa kukubali, na kunyamaza kimya ili kutafakari kuhusu hayo ambayo Raymie alikuwa amesema, na kisha kuendelea;

"Niko na wazo fulani, Raymie," alisema, huku akitoa kijitabu kidogo kutoka kwa mfuko wa shati. "Nataka kupata wazo lako hapa".

Jambo moja lililo mfurahisha Raymie ni kwamba Yohana alimchukulia tu kama mtu mzima, hasa kwa mambo ya kiroho. Yohana alikuwa mtu wa kuisikiza wote, alimchukulia Raymie jinsi alivyowaona wanachama wengine wa makabila kumi na mbili, na hasa kama ndugu katika roho.

Yohana alikuwa na mipanga ya kuanda kambi nne kule Johannesburg kama alivyomueleza Raymie, moja kwa watafsiri, nyingine kwa waalimu, moja ya shughuli za uchapishaji na kueneza, na ya mwisho ya usimamizi na mawasiliano ambapo yeye na Raymie watafanya kazi.

"Hiyo ni sawa sana kwangu," Raymie alisema.

"Lakini itatuchukua kama miezi sita hivi kufundisha wafanyikazi wetu," aliyekuwa mfaasi wa Mashahidi wa Yehova alilalamika. "Na tutahitaji mamia ya watu kama hao kabla ya kumaliza."

"Unakumbuka yale Baba. Yaani, yale Rayford alisema kutuhusu kama mahakimu?" Raymie aliuliza.

"Nafikiri inamaana kwamba sio lazima kumfundisha kila mtu. Mungu atawafundisha iwapotutakuwa huko."

Raymie alipeana mkoba aliokuwa ameshikilia. Ndani kulikuwa na mafunzo aliyotumia kila moja ya makundi sita.

"Hapa ndani kuna majarida mbalimbali kuhusu mafundisho na juu ya kusikiza kila mmoja. Unakumbuka jinsi wale jamaa walivyojifunza wenyewe ulipowacha dini? Twapasa kuwacha wafanye hivyo kadhalika."

Yohana hakutaka kusema lolote kumuudhi Raymie, ila tu angaliweza kukariri "Kishindo kikuu" cha Rayford, lile kundi lililokuja kwenye sebule ya Neville lilikuwa na kishindo, alikuwa na shaka kuhusu uwezo wake kuwasihi watu "kukoma kuwa wafuasi wa dini" kama vile Raymie alieleza. Yeye pia alisema maombi yake kwa kimya.

Iwapo watahitaji mapumziko au kuhitajika mahali popote, kulikuwa na watu wengi kwenye kundi waliokuwa na uwezo wa kutafsiri hata kwa lugha za kienyeji.

Musa aliyeteuliwa kama mhasibu wa kundi, alikubali kutafuta na hatimaye kukodi nyumba tatu zaidi, na kutuma maombi ya kuletewa nakala za kingereza mara moja, huku Alama katika lugha zingine zikitayarishwa.

Ringo alichomoa kitabu kilichokuwa na orodha ya anwani zilizotayarishwa na kundi hilo kabla ya kuwasili kwa Yohana na Raymie. Yeye pamoja na Sylvia mkewe, walichukua jukumu la kuwakaribisha walioleta anwani zao katika kituo cha elimu (mara tu watakapopata kituo) na kuanza kujifunza na kuishi maisha ya makabila kumi na mbili.

Sylvia aliwaarifu kwamba mwanamke aliyetoka alitisha kuvuruga na kuhangaisha kundi. Aliuliza jinsi ya kuepuka majaribio na janga iwapo wanachama watakao hasi na kukaidi na kuwageukia.

"Isipokuwa wakuu au wasimamizi wa kundi, hakuna yeyote anayepaswa kufahamu mambo yanayoendelea katika kundi lingine," Abdullah alisema. Tunaweza fanya kazi katika vitengo. Kwa wakuu na wanachama, majina mengine yatatumiwa. Hivyo hata iwapo watadhulumiwa hawataweza kutoa maelezo."

Kwa mara nyingine Yohana na Raymie walitazamana jinsi walivyokuwa vichochezi katika mfumo uliokuwa ukiendelea kwa njia yake. hasa, kwa njia ya Mwenyezi Mungu.

Baada ya wiki mbili, sehemu zote nne za utendaji zilikuwa mbioni. Wanne zaidi walikuwa wameenda katika kituo cha elimu, mahali Ringo na Sylvia walikuwa wakufunzi washikilizi. Mmoja kati ya wanafunzi alielewa lugha mojawapo ya kienyeji na wale wengine hawakujua, hivyobasi kuteuliwa kama mmoja wa wale watafsiri punde tu atakapo maliza mafunzo hayo.

Mwishoni mwa juma la pili, kanda na majarida yaliyotolewa na kuandikwa na Rayford yalikuwa yakitolewa katika idara ya tafsiri. Muda huo ndio ombi la kwanza la makala yaliwasilishwa kwenye idara ya ugawaji. Ombi lingine la makala katika lugha ya Kiafrikana, lilitolewa, na lilikuwa tayari kusambazwa wiki inayofuatia. Musa alikuwa akijianda kununua Magari yenye nguvu ili kuweza kufikia sehemu za barabara mbovu na njia zisizopitika kwa urahisi. punde tu yale makundi ya kufanya kazi hiyo yatahitimu.

Katika kipindi cha juma kadha, utaratibu huo utaendelezwa mahali kama vile Accra, Capetown, Harare, Monrovia, Kinshasa na Lagos.

Ilikuwa jukumu la Raymie kupokea na kujibu barua, tayari alikuwa akipokea barua kutoka Afrika Kusini hasa wale waliofahamu kuhusu mtandao wa Jesan, na waliotaka kujifunza mbinu zao.

Lilikuwa pia jukumu la Raymie kumfahamisha Rayford kule Uingereza kuhusu matukio na yale yalio kuwa ya kiendelea. Wale wanagenzi wake pia walikuwa na jukumu la kuhakikisha kwamba Irene alitulia na maslahi yake kutunzwa.

Yale yaliyokuwa yakifanyika kule Johannesburg hayakuwa sawa na yale yaliyokuwa yakitukia katika miji mingine mahali mahakimu wa kikabila walikuwa wamewasili. Rayford alikuwa amewasiliana na wahudumu wenzake katika mashariki ya mbali, mtu aliyejulikana kama Chaim Rosenberg, aliyekuwa mkaazi wa Sydney, Australia. Chaim alikuwa na umri wa miaka sitini, naye pia alikuwa ameteua na kuanzisha mahakimu sita. Jukumu lao lilikuewa kusimamia Asia kubwa na vitongoji vya Asia. Mahakimu wa mashariki walikuwa Sydney, Tokyo, New Delhi, Karachi, Beijing na Hong Kong.

Katika miezi sita iliyofuatia , uanachama katika makundi ya makabila hayo uliongezeka kwa takriban mara tatu kila mwezi. Walifanya kazi kwa utaratibu, ili wasiweze kuzua taharuki. Dunia nzima ilikuwa imeja kasumba ya filosofia ya upendo na amani kwa wakati huo, kiasi kwamba hawakuwa wakiona au kuhisi yale yaliyokuwa yakitokea kufuatia kazi ya makabila kumi na mbili. Hata katika mataifa ambayo kazi ya umishonari ilikuwa imepigwa marufuku, kulikuwa na machache yaliyofanywa kuwasimamisha walipoweka mabango usiku wa manane, au walipochukua jukumu lakuwaarifu waumini yale Mwenyezi Mungu alikuwa akitenda.

Hata ingawa milango ilikuwa wazi, ni wachache waliokuwa wakipitia. Waliweza kupata mtu mmoja kati ya 50,000 aliyekaribia viwango vyao. Yale waliyokuwa wakipambana ni kupata kundi la kiroho litakalo kuwa na uwezo wa kutoa mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa dunia, katika yale yatakayo tukia kuwa kipindi cha giza katika historia ya dunia.

Zion Ben-Jonah Aandika

Makadirio ya Rayford yalikuwa kulingana na fungu la maneno katika kitabu cha Danieli, kwenye Agano la kale. Mtu anaweza kubashiri kipindi cha miaka saba katika makubaliano yatakayopelekeahali ya kutoa dhabihu kurudia Yerusalemi na "Kumalizana" (au mwisho). Mwengine anaweza kubashiri kipindi cha siku 2300 kutoka ule wakati wa kuanza kutoa dhabihu hadi pale sehemu ya utakaso itakapo safishwa.

Tofauti kati ya tarakimu hizi mbili (siku 2520 na siku 2300) ni muda unaoweza kuchukuliwa kujenga Hekalu. (Tazama jedwali.)

img2.png

Danieli 9:24-27 imeandikwa kwa mbinu ambayo waweza kudhani inaarifu maagano mawili sambamba, moja kati ya mfalme wa dunia na wafuasi wake na nyingine Mfalme wa amani na wafuasi wake. Moja itapelekea kujenga hekalu, na nyingine kujenga roho kimiujiza.

Lakini kati ya hayo yote jambo la ajabu hutokea kati ya miaka ya mwisho saba, na kusababisha "mkumbo wa ukiwa" na kuharibu aina yote ya "hekalu"