Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

12. Hekalu

Mike na Martin walikuwa na jukumu la kutunza tabaka la Judah, lililojumuisha eneo la mashariki ya kati na Afrika ya masharika. Hekalu la Yerusalemi lilipokaribia kukamilika, wote wawili walitayarisha safari isiyo ya kawaida mbali na tarakilishi zao huko Ankara ili kutembelea kundi ndogo la wafanyi kazi wa mji mtakatifu. Lengo na dhamira ya safari hiyo lilikuwa kujionea yale yaliyokuwa yakiendelea. Talanta na hekima ya Mike kuhusu utaalam wake wa mambo ya jadi yalimfanya kufurahia mitindo ya ujenzi.

Baba mtakatifu alikuwa ametaka kuhamia Yerusalemi, jumba la kifahari lilikuwa linaandaliwa kwa heshima yake karibu naHekalu la Mlima. Jambo hili lilichukuliwa na wanavyuo kuwa sawa na kujiunga na ukristo kwa Constantino. Kwa kutangaza ukristo kama dini yake na katiba ya utawala, na yeye mwenyewe kama mkuu wa dini, Constatino alikuwa amewashawishi wakristo wa hapo awali kutoka kwa makundi yao hadi upande wake, mahali wamedumu mpaka hivi sasa. Kwa kutumia maarifa hayo, Baba mtakatifu alikuwa ameanza kuwachukulia wayahudi na waislamu kama "ndugu" (iwapo walitaka au la) na kwa kufanya hivyo alikuwa amejitwika kama mkuu wa dini hizo tatu.

Wayahudi walitaka hekalu ili kuepuka kushirikishwa na mpango wa Rome, na kuwepo wanajeshi wengi wa Umoja wa Mataifa kule Yerusalemi kwa wakati huo kuliwachaWaislamu wakiwa na njia mbili tu, kufuat yale "ndugu" zake wawili walikuwa wameafikiana.

Miaka 2000 ilifanya mji wa Vatican kuwa mtakatifu kama vile Baba Mtakatifu, katika hali ya utakatifu, Yerusalemi inashinda mji wa Roma. Vicar wa Kristo alipaswa kufanya uamuzi wa kuishi katika mji ulio mtakatifu zaidi kuliko miji mingine.

Januari ya mwaka huo maafikiano yalikuwepo kujenga hekalu mbili. Sasa miezi saba baadaye mijengo ilikuwa iankaribia kukamilika. Mike na Martin walidhuru eneo hili kukagua mradi huo.

Mnara wa mwamba, mahali yaaminika kwamba Muhammed alipaa mbinguni, uliwachwa pasipo kuguswa. Hii iliwezekana kwa sababu hekalu la Kiyahudi liliwekwa upande wa Mashariki-Magharibi (wala sio Kusini Kaskazini) mbali na mnara uliokuwa yadi kadha kutoka kwa Msikiti. Langu kuingia hekalu lililinganishwa na Lango la Dhahabu la ukuta wa Mashariki. Kwa kufuta mtindo wa Hekalu la awali (lakini kufanya "refu" kuliko ilivyokuwa), Hekalu jipya liliingia upande wa Kaskazini kwenye sehemu iliyokuwa ukumbi wa wageni waliotembelea Mnara wa Mwamba.

Kulikuwepo Basilika ya Kikatoliki iliyojulikana kama Cathedral ya Ibaada Takatifu, iliyokuwa upande wa Kusini mwa Hekalu la Mlima. Kwa nje lilionekana kama pacha la Hekalu la Kiyahudi, lakini kulikuwa na mpangilio tofauti humo ndani, ili kuchukua mamia ya waumini na kwaya nzima. Mahali pa "Utakatifu kwa Watakatifu" palijumuisha kwenye mpangilio wa Kiyahudi, kulikuwepo hema takatifu la Kikatoliki kwa shughuli ya kutoa sacramenti.

Upande ule wa mbele ulikuwa umepanuliwa ili kutoa nafasi pana ya Hekalu Msikiti na Kanisa kuu la jimbo la askofu. Wakristo wale wawili hawakuwa na budi kukiri kwamba kuwepo mnara ule katikati ya majengo mapya meupe yaliyo fanana kilikuwa kielelezo chema cha ujenzi.

Wakuu wa madhehebu mbalimbali walifurahi na kuongea kuhusu jinsi Yerusalemi ("Mji wa amani") ulikuwa tayari kukaa kama jina lake. Hekalu zilizofanana zilikuwa dhihirisho la wazi kwamba amani kote ulimwenguni ilikuwa mbioni.

Sehemu zilizoandaliwa awali, kana kwamba hazikutokea mahali, zilipunguza muda wa ujenzi. Hatukuwepo na kungojea kwa vifaa vya ujenzi, kwani kila kitu kilikuwa kimenunuliwa hapo awali.

Ulimwengu wa kawaida haukujali kuhusu hekalu hilo; lakini baadhi yao ilikuwa ishara ya mambo makuu. Yakustaajabisha zaidi, miongoni mwa watu hawa alikuwemo Katibu Mkuu Xu Dangchao, mtu asiye na haja au kuwa na uhusiano na dhehebu lolote. Alikuwa amekatiza mashahuri mbambali na shughuli zake ili kufika Yerusalemi wakati makubaliano yalikuwa yakiafikiwa kuhusu mradi wa hekalu.

Mike na Martin walipokuwa Yerusalemi, habari kutoka kwa jarida la Time Magazine (Sasa hivi kule Hong Kong) kuhusu chimbuko na uzao wa Dangchao. Habari hiyo hata hivyo haikupewa uzito, aidha haikutoa maelezo kuhusu kiini cha Dangchao kuvutiwa na Hekalu , jambo ambalo Mike alitaka kuelewa.

Ilionekana kwamba licha ya Dangchao kuzaliwa na kukua kule Tibet, wazazi wake walitokea jimbo la mkoa wa Kaifang nchini China. Xu lilikuwa mojawapo ya majina saba ya Kichina yaliyo chukuliwa na baadhi ya Wayahudi waliokuwa wakitangatanga kule China yapata miaka elfu moja iliyopita. Wale Wayahudi walikuwa wameona na wanawake wa China kwa miaka mingi, kiasi kwamba sura ya uzao wao ilikuwa sawa na ile ya China na majirani. Hata hivyo, uzao na elimu yake kule China ni ya hali ya juu, haikusahauliwa kwamba mababu wa Xu kutoka Kaifeng walikuwa Wayahudi.

Wachache, kutoka uzao wa Juda walibaki. Lakini babake Dangchao aliwacha kumbukumbu. Alimbatiza mwanawe kwa jina la Levi Xu Dangchao.

Matumizi ya jina la tatu nchini China haikuwa ajabu, lakini jina la tatu la Kiyahudi halikuwa jambo la kawaida.nje ya jimbo la Kaifeng. Xu Dangchao katika ujana wake aliwacha kutumia jina la Kiyahudi alipo toka Tibet kuelekea Uingereza kusoma katika Chuo Kikuu cha Oxford; na swala la kuwa na jina lingine halikuibuka hadi hivi sasa.

Makala hayo yalieleza kwamba chimbuko la uzao wa Dangchao kutoka kwa Wayahudi ndicho kiini cha kutaka Hekalu kujengwa Yerusalemi. Ilibainisha wazi kwamba alikuwa akitoa heshima kwa mababu wake, jambo lililo gusa mioyo ya wengi. Lakini hilo halikutoa maelezo au sababu ya kutaka Kanisa la Jimbo kuu la askofu kujengwa karibu na Hekalu la Mlima.

Mike alihisi kitu fulani kuhusu, jina la tatu la Xu Dangchao, na katika Hekalu tatu. Alipomaliza kusoma alienda kutazama kwa makini majina kamili ya Dangchao, na kuanza kuhesabu na kukadiri jumla ya herufi zilizomo nadani.

"Hapo ndipo!" alimuambia Martin, aliyekuwa amesoma kwa pamoja naye yale makala. "Idadi ya herufi zilizokosea kwenye majina yake sasa zimeleta idadi kamili!"

Mike alikuwa akiongea kuhusu herufi ya L, V, na I kwenye jina Levi. Kuwakilisha 50, 5, na 1 katika herufi za kiRoma. Kwa pamoja na herufi za kiRoma X, D, na C kutoka kwa Xu Dangchao, zinazowakilisha 10, 500, na 100 katika kiRoma, idadi ya herufi hizo kwa kujumlishwa ilikuwa 666, idadi iliyotabiriwa kuhusu kiongozi wa mwisho wa ulimwengu. asiyemuamini Yesu. Mike alijua kwamba Rayford alikuwa akitafakari kuhusu maana ya jina la Dangchao, na hivyo basi kumpatia nakala hiyo.

Rayford alimjibu kwa utabiri wa Makabila kumi na mbili: "katika muda usiozidi miaka mitatu," alisema, "Dangchao atasimamisha kafara, naye mwenyewe atachukua mamlaka ya Hekalu. Ndiposa anataka kujua utaratibu wa ujenzi. Siku moja yatakuwa makazi yake rasmi ya utawala, na kuulazimisha ulimwengu mzima kumsujudu na kumuabudu."

Hapo awali, Rayford alikuwa ameandika kuhusu yale aliyofikiri kuhusu Hekalu zile.

"Hekalu hizo, kama vile Dangchao, ni sanamu," alisema. Yawakilisha ujinga wa Mwanadamu kwamba amani itakuja kupitia mikono yao wenyewe, na wala sio kunyenyekea na kumuamini Mungu.

"Itaonekana kama isiyo na madhara kwa watu ambao hawajapata kumtambua Yesu. Mengi ya makanisa yanadumu nyakati za Agano la Kale, siku ambazo wat waliamini makanisa. Hivyo basi majengo au jengo moja la kifahari, linalojumuisha madhehebu matatu makubwa na yenye nguvu duniani, daima machoni mwao ni kitu cha kuvutia. Lakini ni kwa sababu wanaamini na kutumaini kwenye mijengo, na sio kujitoa kwa moyo wao."

Kulingana na Rayford, kuungana kwa taasisi hizo za madhehebu ilikuwa ni muigo wa kuunganika kwa pamoja makanisa yasiyoonekana, kama ilivyokuwa ikidhihirika kwa kubuni Makabila Kumi na mbili. Madhehebu ya ulimwengu hu yameweka matumaini kwenye suluhisho la kisiasa, alisema, huku waumini wa kweli walikuwa ndani ya roho mtakatifu na mwenyezi Mungu, atakaye waunganisha kwa njia yake.

"Iwapo Mungu hatajenga nyumba, basi wanafanya kazi bure wale wanaojaribu kujenga," alinakili kutoka Agano la Kale.

Mike na Martin walikuwa wamerudi Ankara wakati wa ufunguzi rasmi. Lakini walitazama sherehe hiyo moja kwa moja kupitia kwa runinga pamoja na ulimwengu mzima.

***

Kanisa kuu la jimbo la Askofu halikuwa limekamilika wakati wa ufunguzi wa hekalu, mwishoni mwa kipindi cha joto mwezi wa Juni. Vyombo vya habari havikujishughulisha na yale yaliyokuwemo kwenye kanisa hilo kuu. Wangaliona Makanisa kama hayo wakati wowote na popote. Haja yao ilikuwa ni Hekalu.

Kulikuweko uwezekano tu wa Hekalu moja la Kiyahudi.

Ingawa jamii ya wahubiri ya Walawi (Levi) ilikuwa imekufa, chimbuko mpya la wahubiri lilikuwa limeanza kuibuka la vijana wa Kiyahudi chini ya masharti fulani. Kutoka kwa kundi hili, Kuhani mkuu alikuwa ameteuliwa ili kuongoza shughuli za Hekalu ikiwemo ufunguzi rasmi.

Watu mashuhuri kutoka jamii ya Kiyahudi walikuwepo pamoja na wanasiasa. Ingawa watu wasiokuwa Wayahudi hawakuruhusiwa humo ndani, Picha na michoro ya mpangilio wa humo ndani zilitolewa kwa waandishi wa habari. Solomon angalifurahia. Karibu kila kitu kilikuwa dhahabu au fedha, au jumla ya dhahabu na fedha. Sakafu iliyotandikwa mkeka nadhifu,, visawazishi vya hewa, na kipaaza sauti cha hali ya juu vyote kuonyesha tofauti kati ya hekalu la awali--lile lililojengwa na Solomon, au lile lililojengwa na Zerubbabel.

Hekalu za kwanza zilikuwa mfano wa Safina ya makubaliano, sanduku takatifu lilio kuwa na Amri Kumi na nyimbo zingine za utakatifu. Kuhani tu ndiye aliyepaswa kuingia "Patakatifu kwa Watakatifu" mahali pa safina, na kwamba ungaliingia tu mara moja kwa mwaka. Kuhani aliyeingia humo ndani alifungwa kwa kamba kiunoni, iliaminika kwamba angalipigwa dhoruba na Mwenyezi Mungu endapo alifanya dhambi na kisha kufa.

Hekalu jipya halikuwa na chochote kulinganisha na Safina au Amri Kumi. Lakini ulikosa makabadhiya Kiyahudi, kwa heshima ya historia, katika Agano la Kale na nyakati za kisasa. Makabadhi ya vitu hivi hayakuwa tu kwa utakatifu wa watakatifu. Yalonyeshwa kote katika Hekalu nzima.

Wakati Solomon alitakasa Hekalu, moto ulitoka mbinguni kumaliza kafara. Ule moto wa kimiujiza, ulikuwa umeendelezwatangu hapo ili kuendelea kuchomeka. Lakini hakuna aliyetaraji Mwenyezi Mungu kutoa ishara ya Uwezo na nguvu zake kwenye Hekalu hilo mpya. Mwanga wa miali ya kisayanzi (Laser beam) ulielekezwa kwenye mazibao na kuwasha moto wa milele, ili kutolea kafara.

Watu mashuhuri walitoa hutuba kila baada ya mwingine kwa matumaini kwamba Mungu alikuwa amewaelekeza watu wake katika nchi aliyowaahidi Waisraeli. Kafara zilizidi kutolewa mchana na usiku kucha, huku wale waalikwa wasio mashuhuri wakingoja fursa yao ya kutoa kafara baada ya takriban miaka 2000 kwa niaba yao na mababu wao.

Kulikuwepo machozi ya furaha na sherehe kwenye mji huo usiku wote. Ukuta wa majonzi ulibadilishwa na kuwa ukuta wa furaha, na jumuia ya dunia kufurahia kwa pamoja na Wayahudi, waliokuwa wameteseka kwa karne nyingi, na waliokuwa sasa wakiabudu kwenye Hekalu lao.au katika lile lililo tayarishwa na Katibu wa Umoja wa Mataifa Jenerali Levi Xu Dangchao kwa matumizi.

Zion Ben-Jonah Aandika

Pazia iliyokuwepo kati ya utakatifu na watakatifu iliraruka, kutoka juu hadi chini (Matayo 27:50-51), kwa wakati ule Yesu alisema "Yamekwisha", na akafa msalabani, yapata miaka 2000 iliyopita (Yohana 19:30). Yesu alikuwa ametabiri kuharibiwa kwa Hekalu (Matayo 24:2), utabiri uliodhibitishwa mnamo mwaka wa 70 A.D.

Hata ingawa hatukuwepo na maelewano kuhusu yale aliyoyasema, shtaka moja lililo mpata lilimwezesha kupata zaidi ya shahidi mmoja kukubali wakati wa mashtaka, ni kwamba ati Yesu alikuwa ametisha Hekalu lao la dhamani (Matayo 26:59-62). Kile alichowasilisha kilikuwa muhimu kuliko Hekalu (Matayo 12:6). Aliongea kuhusu wakati ambao umoja hautahusu mahali tunapoabudu, lakini kuhusu yale maadili ya kindani , kama vile uaminifu na imani (Yohana 4:21-24). Miili yetu sasa ni hekalu la Mungu (Wakorintho ya kwanza 3:16).

Ukristo wa kisasa umerudia ule wa Agano la Kale kwa kuabudu Kanisa, kiasi kwamba taasisi ya Kanisa la kisasa ni Uyahudi uliopakwa rangi nyingine.

Lakini ongea juu ya muungano au ushirika unao husu siasa na utaikosa ile alama. Ongea kuhusu mapenzi bila kumhusisha aliye na mapendo, bila shaka hautapata mavuno.