Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

13. Alama

Wengi wa wafuasi wa Uropa waliojiunga na tabaka la Maria Teresa (lililo jumuisha Afrika Kaskazini), walikuwa na utajiri mwingi, ambao haungaligawia tu watu maskini kutoka Afrika, bali pia tabaka zingine katika mataifa yanayostawi. Lakini kupata msaada kutoka sehemu moja hadi nyingine haikuwa rahisi.

Uropa iliongoza mataifa mengine kupokea "Alama", chembechembe ndogo iliyokuwa ikipata umaarufu kote ulimwenguni, kutokana na utendaji wake hodari. Makabila Kumi na mbila, kama Jesans kabla yao, hawakutaka matumizi ya kadi za pesa, kadi za kukopa na kadi nyingine zinazotumiwa badala ya pesa, na hasa matumizi ya Alama. Jambo hili lilifanya shughuli za kibiashara kuwa ngumu kwa makabila yote, na hasa wanachama wa Uropa.

Msimamo uliochukuliwa na Makabila Kumi na Mbili ulitokana na utabiri na laana inayojitokeza katika sura ya 13 na 14 ya kitabu cha Ufunuo wa Yohana:

"Yeye (asiyemfuasi wa Yesu) husababisha wote, wakubwa kwa wadogo, tajiri na maskini, walio mateka na walio huru, kupata alama kwenye mkono wa kulia, au kwenye paji la uso ili mtu asiuze au kununua, ila tu yule aliye na Alama, au jina la mnyama, au nambari ya jina lake." (Ufunuo wa Yohana 13:15-16)

"Yeyote atakaye abudu mnyama huyo au sanamu yake, na kupata Alama kwenye paji la uso au mkono wake, atapata kuonja divai ya ukali na adhabu ya Mwenyezi Mungu, itakayo mwagwa kwenye kikombe chake pasipo kuyeyusha; na kisha kuchomwa kwa moto mbele ya malaika watakatifu, na mbele ya mwana kondoo. Moshi kutoka humo utaelekea juu milele na milele, na hawatapata kupumzika usiku wala mchana, kwa wale wanaoamini mnyama huyo na sanamu yake, na yeyote atakaye pokea Alama ya jina lake." (Ufunuo wa Yohana 14:9-11)

Bila Alama, haikuwa rahisi kwa Chloe dada Maria au yeyote aliyekuwa katika tabaka lao kununua chochote. Rayford na Chaim hawakuwafundisha kwamba kadi hizo zilikuwa muhimu, lakini walifundisha kwamba mfuasi wa kweli alipaswa kukosea kwa kuwa muangalifu badala ya kutoa radhi na kuelekea kupokea alama. Ukweli ulioumiza ulikuwa kwamba mengi yalifanyika kwa kutumia kadi hizo. Dada Maria alianza kujihusisha na biashara za magendo, ambazo zilihitaji pesa nyingi ili kuhusika.

Hata ingawa Waingilisti wa awali waliapa kupinga matumizi ya Alama ilipokuja, punde tu walipoona inawasonga, iliwabidi kuchukua mwelekeo mwingine ili kuitumia, kama walivyo fanya kadi hizo za ubadilishanaji. Mabishano yao ya mara kwa mara yalikuwa kuhusu iwapo Mwenyezi Mungu angewaadhibu watu kwa kutekeleza kitendo kisicho na hatia kama kununua na kuuza.

Njia moja ya kufikiri ilikuwa kwamba Wakristo wangalichukua Alama bila kuabudu shetani, na hasa bila "kuuza roho yao" kwa shetani, huruma ya Mwenyezi Mungu ingaliwarudhuku kwa matendo hayo. Katika hali ya uhalisi walicho sema ni kwamba, hata iwapo wangali abudu sanamu au kuuza roho zao, wangalisema swala la "Kumuomba Yesu moyoni mwao" kabla ya kuuza, Mungu angelazimika kuwasemehe. Fundisho hilo lilidhihirisha ubinafsi, kujipenda, tamaa lutokuwa na uaminifu, na kila aina ya dhambi ungalifikiri kwa karne nyingi kabla ya Alama, hivyo basi ilikuwa ni kawaida kuchukua mwelekeo huo wa kukaidi.

Alama ilichukua miundo tofauti. Kwa umbali, ilikuwa ile alama ndogo, nyuma ya mkono wa kulia. Teknologia ilikuwa imefaulu kutengeneza chembechembe ndogo (au kitu kisicho na uzito) kilichokuwa kidogo sana hata kisionekane kwa macho makavu. Kilikuwa na nambari ya kujitambulisha ya kimataifa isiyo lingana na aina yeyote. Kwa alama hiyo mtu angaliupunga mkono wake wa kulia kwenye miali fulani iliyotumia nguvu za radio ili kutambua kiasi cha fedha za kuongeza au kutoa kwenye akaunti ya benki. Hii ingalifanyika kila mara unapohitaji kununua au kuuza chochote.

Kwa walemavu wasio na mkono, au wale wasio na uwezo wa kutumia mkono wao wa kulia, tulikuwa na Alama ya kibadala. Watu hawa wangalipata Alama hiyo kuwekwa kwenye paji lao la uso. Wangaliweka kichwa chao mbele ya kifaa hicho cha miale ili kuidhinisha uuzaji au ununuzi.

Aina nyingine ya tatu ilikuwa kuhusu watu (hasa wale wenye utajiri mkubwa) walioogopa kwamba wangaliuawa kisha kile chembechembe kuondolewa na watu wakora. Mamlaka iliwahakikishia kwamba chembechembe hiyo ilikuwa ni ndogo sana, na haitakuwa rahisi kuipata baada ya kudungwa, na kwamba kile kifaa cha miale kingalitambua mtu aliye na chembechembe mbili na kukata kutoa huduma.

Kwa wale wasiotaka kudungwa na kupachikwa chembechembe hiyo walikuwa na fursa ya kuwekwa tu alama iliyoonekana kwenye mkono wao ili kuonyesha rasmi kwamba "Wamekubaliwa kihalali kutopachikwa chembechembe" (Declared and Certified Legally Exempt from Verification Implant) iliyo kuwa kwa kifupi kama DCLXVI, au 666 katika herufi za kiRoma!

Watu wasio kubali kupachikwa chembechembe wangaliruhusiwa kuweka nambari ya kujitambulisha kwenye mashine ya miale, kama ilivyofanywa hapo kabla ya Alama.

Labda Dangchao peke yake ndiye hakupaswa kupata aina yeyote ya Alama kwani jina lake lilikuwa ni Alama.

Chloe na Maria waligundua kwamba, kutokana na matumizi ya Alama yalivyoenea kule Uropa, wanachama wapya walikata kutiwa ile alama au kupachikwa chembechembe kwa sababu moja au nyingine. Kwa wengi lilikuwa ni jambo la ajabu tu kwani hawakuelewa yaliyokuwa yakiendelea kwenye benki. Mshangao huu ulidhihirisha kwamba Mungu alikuwa akiwakinga dhidi ya Alama.

Hata hivyo Rayford na Chaim walifanya juhudi kuwaelimisha wanachama kuhusu yaliyokuwa yakiendelea, na haja ya kujianda kufa kabla ya kukubali Alama.

Wachache kati ya wanachama wao walikuwa na kadi hizo za kukopa au kulipia. Hii ilikuwa hakika kwa wale waliotoka Uropa. Lakini daima walijaribu kutumia pesa kwenye biashara. Kwa muda kadi hizo ziliaribiwa.

Benki zilianza kuweka masharti mapya kwa watu waliokuwa na pesa nyingi. Malipo ya nauli ya ndege, kodi, kuchapisha, magari na hata vyakula na mavazi kwa kutumia pesa yalicheleweshwa, na hata kuwapelekea watu kulipia juu zaidi kuliko kawaida.

Rayford na Chaim waliomba makabila kumi na mbili kujitayarisha kwani itafika wakati hawatakuwa na uwezo wa kutumia kadi hizo au pesa. Chloe alikuwa amejifunza mengi kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu aliokuwa pamoja na Jesans na kutayarisha mwongozo juu ya kuishi bila kutegemea usaidizi kama huo. Mbinu zake tatu za kuishi zilikuwa "Omba, Badilishana au Iba." Kuomba na kuiba kuliwashangaza wanachama wenzake hadi pale alipofafanua.

"Ni fahari ya kidini tunayokumbana nayo," Chloe aliandika. "Tunaongea juu ya kuiba vyakula vilivyotupwa kutoka kwa maduka ya jumla au kuomba wakulima kuturuhusu kuokota matunda yaliyosalia baada ya mavuno. Kizingiti kinacho tushikilia sio kwamba tunafanya maovu. Ni hali ya kujivuna."

Kule Uingereza Rayford alikuwa ametafiti kwa pamoja na wale viongozi wengine na kisha kumaliza na kundi lililotembelea duka moja la jumla lililokuwa mashuhuri kwa Jesans kule London Magharibi. Kila kiongozi alipaswa kuingia kwenye pipa na kuchakura chakula au bidhaa zingine za dhamani. Ilipowadia zamu ya Irene, aliingia kwenye pipa moja kwa kusita huku Rayford akishika doria nyuma ya gari karibu naye.

Irene aliyekuwa ameepa kutekeleza mambo kama hayo walipokuwa wakiishi na Rayford kwenye vyumba vya Guildford, alikuwa na wasi wasi. Alijipinda nyuma ya pipa la kiwanda, ili kukanyaga ua lililokuwa karibu, kabla ya kupanda ndani.

Lakini kabla ya kujiinua, aliona kitu kikisonga ndani ya pipa, na kuingiwa na hofu. Mbele yake alimuona mwanamke mkongwe aliyekuwa amevaa matambara, nywele zisizo laini na uso mweusi kwa uchafu. Wanawake hao wawili walitazamana kwa mshtuko.

Lakini alikuwa mwanamke yule dhaifu wa matambara aliyeongea kwanza.

"Irene!" aliita kwa sauti na mshangao, na kisha kujifunika mara moja kama kwamba ni aibu.

Irene hakuwa na la kusema. Ni vipi huyu mwanamke mkongwe na mchafu aliweza kujua jina lake? Kisha aliona kitu fulani usoni mwa mwanamke yule alichokitambua.

"Elaine? ni wewe? Elaine!"

Irene aliinama kumkumbatia yule mwanamke dhaifu, aliyekuwa ameanza kulia, kwa hofu na kuokaka.

Wakati Rayford alikuja kuona mbona amechukua muda, Elaine alikuwa amesimulia yote yaliyompata. Yale aliyowacha yalikaririwa kila mara walipokuwa wamemaliza shughuli hiyo ya kuchokora.

Elaine Billings aliweza kutumia gari na pesa za Tom na Betty kununua mafuta, na kujiendesha pamoja na mmewe hadi kule Montana, walipomuacha Irene kule Dakota Kaskazini; lakini Vernon alikufa kutokana na miali ya jua wiki moja baada ya kuwasili.

Wale wanahiji walikuwa wamesambaratika walipokuta kwamba hakuna Masia kule Montana. Baadhi ya watu kadhaa walijifanya kuwa Yesu, ili hali wengine waliona wampatie Mungu muda, na ndoto zao zitakuwa kweli. Kwa jumla lilikuwa kundi la wanahiji waliosikitika. Wengi wao kama Elaine walipotewa na imani huku wakishindwa la kufanya. Wengi walikufa walipokuwa kule Montana kabla ya helikopta kuwanusuru baada ya wiki kadhaa.

Ilikuwa ni bahati tu au utaratibu uliokiukwa ndio uliomfikisha Elaine Uingereza. Alikuwa ameelewa kwamba alikuwa na binamuye kule Uingereza ambaye angalijali maslahi yake. Lakini kwa kuchanganyikiwa, mamlaka ya wakati huo (wengi walikuwa wa kujitolea) walifanya machache kudhibitisha madai yake. Alipowasili, Elaine alipata maskini binamu wake aliaga dunia baada ya kukumbwa na mshtuko wa moyo mwaka mmoja kabla. Alikuwa peke yake katika nchi ya ukiwa pasipo msaada wa aina yeyote.

Elaine hakufanya juhudi zozote kuomba kutunzwa au kupata msaada kutoka kwa kanisa lolote au shirika lolote la kibinadamu. Na kuchagua kujitafutia tu katika vitongoji vya miji. Licha ya hali yake hiyo ya kushangaza na kutisha, Elaine alikuwa na tabia timamu iliyo muwezesha kuishi katika maisha hayo ya ukiwa kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.

Elaine kwa utaratibu alianzakurejelea hali yake kutoka kwa hayo masaibu. Kwa sababu wote walikuwa wamepitia kwenye njia hiyo ya hiji, yeye pamoja na Irene walikuwa pamoja kuliko dada wa aina yeyote. Irene alimuona mwenzake huyo kama baraka kutoka kwa Mungu, kwa niaba ya mwanawe wa kike na kiume alio waaga miezi kadhaa iliyopita. Elaine alikaribishwa na kukubaliwa kwenye tabaka la Yusufu kama mojawapo wa waasimamizi wa kundi la Guildford.

Tukirudia maelezo ya Chloe kuhusu kuishi bila Alama. "Kuiba" kilikuwa kitu cha hapo awali ambacho Elaine alikuwa hodari, baada ya mwaka mmoja na nusu kwenye vitongoji vya mji. Alikuwa na ujuzi wa kuchokora na kuishi kwa kutumia vyakula vya mapipa. Lakini bila shaka alikuwa hodari katika ubadilishanaji. Alikuwa amejifunza kuokota vito vya dhamani, na kisha kubadilishana na kwa vyakula, nguo na hata mahali pa kujikinga usiku. (ingawa alitegemea kuomba kujikinga).

Kubadilishana ilikuwa njia muafaka ya kuepuka Alama, hasa kwa wanachama wa Makabila Kumi na Mbili waliokuwa wakitoa utajiri wao, na kutoona haja ya vitu vya ulimwengu kwenye maisha yao mapya. Katika miaka ya usoni walihitaji kufanya hivyo ili kupata mavazi na chakula. Iwapo walikuwa tayari kupata hasara yeyote, walitaraji kupata mtu wa kuwapatia walichohitaji kwa pupa.

Upungufu ni kwamba ubadilishanaji hautawezekana ili kupata tikiti za usafiri au gari, kwa sababu ya hati za makaratasi zinazohusishwa. Hivyo basi Makabila Kumi na Mbili yalionywa na msemaji wao kwamba watakumbana na nyakati ambazo watakosa vitu fulani kama hivyo.

Wafuasi hao walikuwa wamebaki na muda wa miaka mitatu na nusu baada ya kutiwa saihi makubaliano ya ujenzi wa Hekalu, na kisha kulazimishwa kuondoka kwenye mfumo wa kiuchumi; lakini kwa majaribio, walikuwa tayari wameanza, hasa wale waliokuwa wakiishi upande wa Magharibi.

Jesans na wengine waliokuwa nje ya mfumo huo kama Elaine hata kabla ya mkataba huo, walitambuliwa kama walio na umahiri wa kuishi katika nchi za utumwa. Walikuwa wamefaulu kwa kukata kutumia Kadi za aina yoyote--- na kipao mbele chaAlama.

"Hatuhitaji maelezo mengine kuhusu Alama zaidi ya yale yaliyo kwenye injili," aliandika Chaim Rosenberg, akiwa Australia "Alama haizungumziwi huko," aliendelea. "Lakini huko, kuma mafundisho yaYesu, tunahimizwa, kuwa kama maua au kama ndege, viumbe visivyo na kazi, hakuna kazi ya kulima, na hawana haja ya kufuma nguo. Mungu anawalisha, na atatulisha iwapo tutaweka kazi yake mbele. Laiti tungalitilia hilo maanani karne kadha zilizotangulia, , tungali kuwa tayari kukabili yanayotarajiwa kutukia."

Chaim alifundisha kwamba shida zitakazo wakabili wafuasi wakati wa mwisho itakuwa ni kutokana na kuasi au kutozingatia mafundisho ya Yesu.

"Wasio mfuata Yesu hawapaswi kutuwinda," aliendelea. Wale wasio na imani kamili wanajitayarisha kupokea Alama. Wengine walio werevu wako tayari kukana Alama, hivyo basi wataangamia na kufa. Itatendeka hivyo kwasababu hawajapata kumti na kumskiza Mwenyezxi Mungu kila mara. Hayo ndiyo tunayojifunza hivi sasa. Lakini wale wanao kimbia adabu kama hii watalipa kwa uchungu miaka michache ijayo."

Zion Ben-Jonah Aandika

Alama ya Mnyama ni karibu sana na kweli, wale wanaojadili na kudai kwamba sio utimilizo wa Ufunuo wa Yohana 13:15-17, wanajihusisha au kuelewa kiufundi. Hapana shaka kwamba tutakuwa na maendeleo katika taaluma ya kiufundi miaka michache inayokuja, Ulimwengu mzima utajiingiza kwenye mfumo wa biashara uliotabiriwa miaka 2000 iliyopita. Na Bibilia inatueleza kwamba uvumbuzi huo utatoka kwa wanao muasi Yesu. Waweza kutafakari kuhusu usemi huu au kumtupa Mwenyezi Mungu na Bibilia.

Kutokana na onyo kali linalotolewa na utabiri huu kuhusu kukubali Alama, itahitaji mtu aliyekufa kiroho kutozingatia na kuendeleza anasa na hali ya maisha ya vitu vya ulimwengu huu (wakiwemo waumini wa makanisa) pasipo kubadilika.

Hivi sasa wengi wa watu walio Magharibi, inaonekana kwamba hawako tayari "kuwa salama" na kuishi kama Wakristo wa jadi. Kuna utajiri mwingi katika jamii zetu, na kuna neti za kushikilia yeyote anayetaka kufanyia majaribio aina ya maisha ya kiroho kuliko jinsi ya kununua kabati mpya yakuweka nguo na magari mapya. Lakini wanaendelea kumuasi Yesu.

Bila au na Alama, dunia (tena yakiwemo makanisa) imeendelea kuweka imani yake kwenye mambo yasiyofaa, na kupoteza muda mwingi kujishughulisha na maovu wanayodhani yatawaletea furaha.