Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

14. Amani! Amani

Kutoka siku ya ufunguzi wa Hekalu, uanachama wa Makabila Kumi na Mbili (idadi iliyokuwa 144,000) uliweza kudidimia. Kwa ghafla ilikuwa ni vigumu kushawishi na kutafuta wafuasi, kama ilivyokuwa kabla ya kutiwa sahihi kwa makubaliano ya Hekalu.

Rayford na Chaim walikuwa wamejitayarisha kukabili hali hii. Walibadili himizo lao baada ya kufunguliwa kwa Hekalu la kuhubiri ndani na wala sio nje. Vikao vilihamishwa kutoka mahali pa kulipa kodi hadi kuwa maskwota kwenye nyumba zisizotumika; tarakilishi sogevu ziliweza kuunganishwa na simu ili kuwasiliana kwa mtandao. Katika miezi saba na nusu ya kwanza, wachache kati ya wanachama 144,000 waliweza kupata fursa ya kusoma jarida la digest, ukweli halisi uliokuwa umetayarishwa na kuandikwa na Chaim na Rayford. Sasa walikuwa na nafasi ya kujadili yale yaliyokuwa yameandaliwa hususan kuwahusu na nafasi yao katika historia.

Wale waliokuwa na jukumu la kutafsiri walikamilisha jukumu hilo, na Neville pamoja na Rayford waliweza kuboresha ukurasa wao kwenye mtandao, na kuanda maelezo katika lugha tofauti kwenye tuvuti. Kanda za CD na zile za mziki zilitayarishwa, kwa pamoja na mamia ya tani za makala.

Marekebisho na haja ya kuhariri makala hayo ilikuwa ni lazima, kwani walikuwa wakienda kutoa ujumbe uliotofauti baada ya tukio hili ukilinganisha na ule wa hapo awali. Rayford alieleza katika makala aliyoita "Kutia mhuri na Ng'ambo". aliandika:

"Enyi watu mmetiwa mhuri au kuchaguliwa spesheli na Mungu ili muweze kuwa nguvu yake katika kueneza ujumbe wake wa mwisho katika miaka mitatu na nusu iliyobaki katika historia ya Kanisa."

"Msishangae kwamba hamuwezi kuona dhibitisho la mhuri kwa nje. Mhuri huo unatambuliwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe. Lakini kuja kwetu pamoja na kuunganika kama jamii moja kutoka mbali na mbali, ni dhihirisho kwamba alituchagua."

"Mungu ataweza kujaza nafasi endapo mmoja wetu atakufa au kukata kufuata mwana kondo. Licha ya hayo idadi yetu haitaongezeka kamwe. Mwaweza kusema kwamba hatima yetu imefungwa. Lakini kama mnavyotambua, bado tuko na uamuzi wa kibinafsi. Tunaweza kuchagua kukana wito huu na tupotee. Usijipeleke kumjaribu Mungu kwa kuamini uongo kwamba hawezi kuchukua uridhi wako (kama alivyofanyia Wayahudi, na jinsi alivyofanyia taasisi ya kanisa); kwani ukifanya hivyo, nafasi yako itachukuliwa na kutolewa mtu mwingine"

"Vile vile Mungu anayejua kutofautisha mwanzo na mwisho, anajua kwamba angalau wengi wetu tutaendelea mbele na hatutarudi nyuma. Aidha pia anafahamu kwamba, wengi wa wale walio kataa kumfuata na hawajajumuishwa kwenye uanachama wetu, watamuasi, hata nini ifanyike.

"Kilichobakia sasa ni juu yetu kuelekeza umati mkubwa ili usiadhiriwe na adhabu ya wasiomfuata Yesu. Lakini ili kufanya hivyo tutahitaji kujenga Huzuni Kubwa. Nitafafanua:

"Kama mnavyojua, watu kila siku wanakubali Alama ya Mnyama, na wafanya hivyo kwa mamilioni. Wameambiwa na wakuu wa madhehebu yao wafanye hivyo kisha kusingizia kutojua, au kutaka msamaha kutokana na huruma ya Mwenyezi Mungu punde tu Yesu atakaporudi, na kuokolewa. Itakuwa ni jukumu letu kuhubiri kinyume na hayo, na wakati huo kuwapa mabilioni ya watu waliopokea alama fursa ya kuungama na kuokoka."

Makabila Kumi na Mbili yalishangazwa sana na maelezo ya Rayford kuhusu kuokolewa kwa watu ambao tayari walikuwa na Alama ya Mnyama. Lakini Chaim alimuunga mkono.

Hawakuelezwa jinsi ya kuwahubiria au kuwatolea ujumbe wale waliokuwa na Alama. Waliambiwa tu itadhihirishwa na kufunuliwa baada ya miaka tatu na nusu ya mwisho. Kwa sasa walipaswa kufundisha kwa bidii kama kwamba hakuna fursa kama hiyo.

Makabila hayo yalisikia mengi kiasi cha kutenda angalau mawili. La kwanza lilikuwa ni kuomba uhakikisho kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwamba hawajadanganyika. Walikuwa wakiishi katika nyakati za uongo kama ilivyotabiriwa, na kwamba yale Rayford na Chaim walisema yalionekana kama uongo, mhali ambapo wameepuka.

Jambo la pili lilikuwa jinsi ya kuwachukulia wale walio kuwa na Alama. Ilikuwa rahisi kuwa mchoyo, kiasi cha kuto wapenda wale waliopotea. Lakini nini kingalitokea iwapo ulimwengu haujapotea milele? Na je iwapo wale 144,000 wangalikuwa wamepotea milele? Utatanishi kama huu kuhusu imani yao na ile ya wasio na imani ulikuwa bora; ulifanya kinyume na mwelekeo wa kujivunia dhehebu.

Huku wakingojea wakati huo wa kuhubiri kuwadia, Makabila hayo Kumi na Mbili yalishindwa kusadiki kwamba walikuwa wakiishi nyakati za mwisho. Ulimwengu kwa kimiujiza ulikuwa unapata marekebisho kufuatia mkasa mkubwa kuwai kutokea duniani, mkasa uliosababisha vifo vya watu milioni thelathini na tano huko Amerika. Baada ya maafa hayo, ulimwengu ulikuwa unastawi kwa haraka kuliko hapo awali. Uongozi wa Xu Dangchao ulileta mabadiliko ya kila aina, yote yaliyomnufaisha karibu kila mtu. Hata Makabila Kumi na Mbili yalikuwa yamenufaika kutoka kwa masikizano baina ya madhehebu.

Ilikuwa vigumu sana kuamini kwamba hapo usoni kulikuwa na maandalizi ya huzuni na kuhangaika kwa ulimwengu, ambao ulilinganishwa na kuangamia kwa Amerika!

"Itumie! Itumie!" Chaim alikuwa ameandika katika utaratibu wa matumizi ya wakati nyakati hizi za amani duniani. "Lakini usiamini hata kwa sekunde moja kwamba ni hakika," alionya.

Chaim na Rayford walifikiri kwamba kufikia sasa mamlaka yalikuwa yameanza kutambua kuwepo kwao na kwa kiasi kidogo yale waliyokuwa wakifanya, na ni muda tu kabla ya shoka kuwaangukia.

Utabiri wa watu wa Mungu kuhaidiwa "mabawa ya mwewe" ilikuepuka kusulubiwa, ulikuwa umewafikia. Kwa hakika ilikuwa ni ushairi tu. Hawakutarajia kumea mabawa. Lakini hata kama walipata ndege ya kuwasafirisha, walishindwa mahali pa kujificha ili wasitambuliwe na zana za kiteknologia zilizokuwa zikitumiwa na mataifa kuwinda na hatimaye kupata chochote au mtu waliyehitaji.

Usafiri wa ndege ulikuwa ni mgumu kutokana na hitaji la kuwa na Alama, ili kupata tiketi, aidha pia mamlaka yaliyo miliki ndege na viwanja.

Wataalamu wa Bibilia walifundisha kwamba mahali pa kujificha ni Petra, mji uliochongwa kwa miamba ya mawe, kule Yorodani. Lakini hatujui iwapo taaluma ya kisasa itakosa kuingia mahali kama pale, na iwapo palikuwa mahali pa siri, basi siri hiyo ilitambuliwa na wale walioandika na kueneza ujumbe kwamba ni mahali pa siri.

Maandiko yalieleza kama mahali pa kujificha "jangwa" au "mahali pa ukiwa" lakini hakuna yeyote kati ya viongozi hao wawili aliyesema ni mahali papi. Kwa sasa waliwasihi wanachama kuchukua mwenendo wa utaratibu, na kutamai kwa Mwamba Imara wa Milele, na mafundisho yake, tuliyoambiwa na Bibilia yatakuwa Mwamba usiotingika, na kuwakinga dhidi ya "mafuriko" na "dhoruba" (Matayo 7:24-25)

Wataalamu wengine wa Tarakilishi waliokuwa miongoni mwa kundi hilo walijiunga na Neville, na kwa pamoja wa kaanda mawasiliano kupitia kwa tuvuti hadi kwenye mtandao wao, ili iweze kuwa vigumu kuwafikia. Lakini walielewa kwamba baada ya muda fulani, mtandao wao utagunduliwa.

*.*.*

Ilikuwa yapasa miaka mitatu tangu kufunguliwa kwa hekalu kule Yerusalemi. Wakuu wa usalama wasiopungua nusu dazani walikuwa wamejikusanya kwenye sehemu isiyo na mwangaza mwingi, kuzunguka mashine ya kisasa ya tarakilishi na vifaa vingine vya mawasiliano katika afisi fulani kule Moscow, ilikuwa ni Jumatatu jioni mwishoni mwa Juni. Wafanyi kazi wengine walikuwa wameenda nyumbani jioni baada ya shughuli za siku nzima.

Mmoja wa wale wataalamu, mtu mnene aliyejulikana kama Sergei, alivunja kimya huku wakitazama kio cha tarakilishi moja, huku wakitaraji kitu fulani kutokea. "Yeyote kati yenu aliyeuzuru ukurasa wa mtandao huu?" aliuliza., ili kutuliza uchovu wao.

Walitazamana tu, huku wakiofia kujibu. Sergei alidhani kwamba ameuliza swali la upuzi, lakini alijaribu kuendeleza swala hilo kwa mazungumzo zaidi.

"Ni stihizai, kweli. Wanafikiri kwamba watu wanaweza kuishi bila pesa. Wanasema chembechembe itakayopachikwa imetoka kwa shetani." Sergei alicheka sana. Hatukuwa na jibu. Waligeuka na kumtazama Sergei kama kwamba walitaraji aongee.

"Nili-nili niliutazama tu kwa sababu kijana wangu wa kiume aliniambia niutazame," alisema kwa kujitetea. Lakini hayo yalimuweka fikira zaidi. Macho yaliinuliwa, na moyo wa Sergei kuzama kwa kutatizika na yale aliyosema juu ya mwanawe ili kujiondolea lawama.

"Kweli, haku. na maanisha." aliaanza bila uhakika wa kumaliza aliyokuwa akisema.

"Ndio hiyo!" alipaaza sauti mmoja kati ya wale maafisa, ambaye alikuwa akitazama kio cha tarakilishi. Sergei na mwanawe kwa muda walikuwa wametengwa, hasa kwa muda.

"Ni Uingereza. Magharibi mwa London!"

Wale wanaume walifaulu kupata chimbuko la mtandao wa Rayford.

"Tutausimamisha mtandao huu wa wasaliti hawa sasa hivi!" alisema yule mzee, aliyeonekana kuwa msimamizi wao. "Lakini twapasa kujua kwanza ni nani aliye nyuma ya mpango huu. Oleg tafuta London kwenye simu!"

***

Wafanyi kazi wa Web Wonders, kule makutano ya Clapham, ndio walikuwa wakimaliza zamu yao kuingia usiku, ulipotendeka. Mlipuko haukutokea humo ndani bali kule juu, miale ya nguvu iliyopenya ndani ya jumba lile, na kisha kulipuka, na kuteketeza kila kitu humo ndani wakiwemo watu wale na kubaki jivu, na kwa wakati huo kuwacha tu yale majumba yaliyokuwa karibu na alama za moshi kwenye ukuta. Web Wonder nawafanyi kazi wake wote hawakuwepo tena.

Mwanzo wa huzuni kuu ulikuwa umewadia.

Zion Ben-Jonah Aandika

Wafasiri wengi wa Bibilia wanatafsiri kuhusu miaka saba ya huzuni mkuu kabla ya Yesu kurudi. Lakini Ufunuo wa Yohana unaeleza wasi kuhusu kuwepo kwa awamu mbili za nusu ya miaka hiyo saba ya mwisho. Imeelezwa kama miaka tatu na nusu, miezi 42, au siku 1260. (Ufunuo wa Yohana 11:2-3, 12:6 na 14, 13:5, na Danieli 7:25, 9:27) Ni nusu ya mwisho, yaani miaka mitatu na nusu ya mwisho iliyo jaa dhiki kuu. Nusu ya kwanza ndio hujulikana kama "amani ya plastiki".

Wengi wamesema kwamba vita ndiyo ishara ya siku za mwisho, Yesu alisema kwamba vita ni ishara yakwamba sio karibu (Matayo 24:6). Lakini, maandiko yanatoa onyo kwamba waasi na wasio mfuata Yesu ndio watakao tawala dunia na kuongoza `amani' au kwa tafsiri nyingine `Maendeleo' (Danieli 8:23-25). Mtume Paulo, akiandika kuhusu nyakati za mwisho, alionya kwamba `uharibifu wa ghafla' utafuatiwa na kila mtu kusema "Amani! Amani!" (Kitabu cha I cha Wathesolonika 5:3)

Ufunuo wa Yohana pia unaeleza kuhusu wanajeshi waaminifu 144,000 walio wafuasi wa mwana kondoo (Ufunuo wa Yohana 7:2-4, na 14:1-12), na wakati huo kuongea juu ya "umati mkubwa usio hesabika." (Ufunuo wa Yohana 7:9-17) Umati huu umeletwa mbele ya mwenyezi Mungu wakati wa Huzuni Mkuu. Wafuasi kadha kwa kimiugiza wamelindwa (Ufunuo wa Yohana 12:14), lakini wengine wamechinjwa kwa wingi (Ufunuo wa Yohana 13:7). Fumbo la kweli iliyo kama uongo!