Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

KITABU CHA TATU

15. Mauaji ya Siri?

"Nitafanya. Sitaogopa! Nitafanyia Mwenyezi Mungu."

Neville alikuwa akiwaza na wenzake kuhusu barua-pepe aliyo pata sio iliyotanguliwa kutoka kwa Mike aliye Ankara. Mike alisema kwamba lile kundi lililokuwa Yerusalemi lilipita mita mia moja kutoka eneo alilokuwa Dangchao mara nyingi, katika shughuli zao mjini humo. Alisema kwamba usalama wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa haukuwa wa hali ya juu kama alivyodhani.

"Yuko na walinzi," Mike aliandika. Lakini iwapo mtu angalikwenda mbio na kumkaribia huku amevalia bomu, sidhani kama wataweza kumsimamisha."

Ujumbe wa Mike ulisababisha mjadala katika makao makuu ya Guildford, kuhusu iwapo itakuwa bora, huku wakifahamu mengi kuhusu Dangchao, kufanya mipango ya kumuua.

"Huyu sio kama binadamu," Neville alieleza. Ikiwa yeye ni Ibilisi, nini mbaya kwa kumuua?"

Rayford hakuwemo humo, lakini Irene ndiye aliyeuliza fikira yake kuhusu hayo. "Zaidi na hayo, je iwapo ni kiongozi bora kama vile dunia nzima inavyo dhani?" wote walimtazama Irene kwa mshangao. Je, alikuwa amedanganyika? Aweza kuwa alikuwa akiongea kuhusu kumtetea aliye muasi Yesu?

"Sisemi kwamba hawezi kuja kuwa shetani aliyezaliwa upya," alieleza. "Lakini tazama aliyofanya hadi hivi leo. Amewaleta watu pamoja kama vile ulimwengu haujawai kushuhudia. Amesaidia mataifa maskini kwa njia ambayo hayajawai kusaidiwa. Ameleta uwiano baina ya dini na madhehebu mbalimbali jambo ambalo limetufaidi." Mshangao ulikuwa unaibuka, hivyo basi Irene alianza kufafanua.

"Ninayo sema ni kwamba anaweza kuwa akifanya mazuri haya yote kwa nia mbaya." na akakimya. ".ama kwa kweli anaweza kuwa akitenda mema haya na kisha baadaye kutawaliwa na shetani hapo baadaye. Je vita vyetu ni kati ya Xu Dangchao aliye binadamu au ni shetani atakaye chukua mwili wa Dangchao wakati ujao?"

Matayo kama hakimu wa ukoo wa Yusufu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumuunga mkono Irene.

"Hatujui kwa hakika iwapo Dangchao ni binadamu, na ni kama mimi nawe kwa wakati huu." alisema. "Lakini kama ni Ibilisi nasi ni wapatanishi!"

Maelezo hayo yalikuwa na maana ikikumbukwa yalikuwa yanatoka kwa aliyekuwa mbatizaji, aliyeamini kwamba majeshi yangalitumiwa kutekeleza mapenzi ya Mungu. Lakini hiyo ilikuwa kabla ya kukutana na Jesans.

"Wakristo hawaangamizi maadui zao," Matayo aliwakumbusha wenzake. "Na hiyo inajumuisha hata adui wetu mkubwa. waasi wa Yesu. Malipo ni kazi ya Mungu, wala sio yetu. Iwapo tumefahamu Bibilia Vyema, Dangchao atapata jeraha kubwa hatimaye. Labda ndio wakati atakopoingiliwa na shetani. Na labda yeye kwa wakati huu hana hatia kama vile mimi nawe."

"Labda ni sisi ndio twapasa kumpatia jeraha hilo," alipendekeza Neville. Twapasa kumpigania vita Mwenyezi Mungu kule Magedoni. Sasa iwapo twaweza kuua watu kwa niaba ya Mungu, mbona isiwe hivyo?"

"Iwapo waweza kumuua Dangchao kwa kusema tu neno, basi muue," Matayo alidhihaki. Neville kumbuka kwamba silaha yetu kule Magedoni yapasa kutoka kinywani mwetu. Silaha yetu ni ukweli. hakuna kupunguza hakuna kuongeza. Wanelewa?"

Maria na Elaine walisikiza kwa makini, bila kusema lolote. Walikuwa katika zile nyakati za jadi ambazo wanawake hawakupaswa kusema lolote, ila kukimya.

"Unafikiri vita hutoka wapi?" Matayo aliuliza, akisukuma wazo lake mbele zaidi.

"Kutoka kwa serikali zilizo na tamaa ya mafuta na utajiri," Neville alijibu kwa ujasiri. Alikuwa amesoma makala ya Rayford kuhusu mambo hayo.

"Hasaa. Kweli." Hilo sio jawabu alilokuwa akitaraji Matayo, hivyo basi alijibu mwenyewe. "Lakini wanapata wanajeshi kupigana kwa kushetanisha wapinzani." alisema. "Iwapo unaamini kwamba mpinzani wako ni nusu-binadamu, basi utajihisi umetosheka kufanya lolote. lakini Mungu hafanyi hivyo Neville. Yeye yuko na njia za kuwakabili wapinzani wake."

Mjadala ulimalizika punde tu Rayford alipoingia na gazeti mkononi.

"Mmesikia habari?" aliuliza.

Bila shaka hawakuwa wamesikia kwani jukumu la kupitia magazeti na kuleta habari lilikuwa la Rayford, ambaye alienda kila asubuhi kwenye mkahawa, na kisha kurejea na nakala ya bure. Lakini kwa wakati mwingine walifunga na kuitegea idhaa ya BBC, na alikuwa akjiitegea kabla ya kuongea.

Alitupa gazeti lile kwenye meza, ambapo kila mmoja angaliona kichwa chake:

Dangchao Auawa

Ripoti hiyo ilieleza jinsi Dangchao alikuwa amedungwa kisu na mshangiliaji alipokuwa akikagua ujensi wa sanamu kubwa ya Maria, Malkia wa Mbinguni, iliyokuwa ikijengwa mbele ya kanisa kuu la jimbo la askofu kule Yerusalemi. Jeraha la mduara wa sentimita tatu lilikuwa limedunga moyo wake.

"Alikufa alipofikishwa katika hospitali ya Chuo kikuu cha Hadassah," msemaji wa hospitali ile alitangaza.

Ripoti hiyo ilikuwa na maelezo kumhusu muuaji wa kujitolea, ambaye baadaye aliuawa na maafisa wa usalama baada ya shambulizi. Habari hizo pia zili dadisi kuhusu nani angalitwaa mamlaka ya Dangchao. Risala za rambi rambi zilizidi kupokelewa kutoka pembe nyingi za dunia, risala hizo zilimtambua Dangchao kama kiongozi mashuhuri na mkuu ulimwenguni, dunia ilikuwa imempoteza kiongozi mashuhuri kuliko mwingine yeyote.

"Je hilo sio jawabu kwa swali lako?" Matayo alimuuliza Neville, waliporejelea hali ya kawaida kutoka kwa mshtuko huo. "Iwapo Mwenyezi Mungu anataka kumzuia mtu, anaweza kufanya hivyo, bila kuzuiwa na wewe au mimi."

"Sasa ni nini kitatukia?" aliuliza Neville?" aliuliza Neville. "Je atapata uhai tena?"

"Ataweza iwapo yeye ni muasi wa Yesu," Rayford alisema. "Twapaswa kungoja. Hivi sasa tuombe kuhusu kile tunataraji kufanya. Leo ni siku ya 1,260 tangu kutiwa sahihi kwa ule mkataba."

Kundi hilo liliomba asubuhi ile na kujadili kuhusu muelekeo wa mambo. Hawakuona lolote jipya au mwelekeo usio wa kawaida. Rayford hakupata habaari sahihi?

Walitazama barua-pepe kutoka pembe zingine na hawakuona lolote likiendelea huko.

Irene alikuwa na shughuli kule London, kwa hivyo alipanda gari moshi mchana. Jioni alirudi na uso ulio guna.

"Je mlitazama barua-pepe asubuhi hii?" aliuliza Rayford kwa mshangao.

"Yeah. Mbona?" alijibu.

"Mmerudia tena tangu hapo?" aliuliza.

"Saa moja iliyopita nilituma bara-pepe kwa Chaim na kutazama mtandao," alijibu. "Mbona?"

Wasiwasi ya Rayford haikuwa kwa swali bali ni hali ya kutatanisha jinsi alivyouliza.

"Ulipata shida yeyote?" aliendelea.

"Yote haya ni ya nini?" Rayford aliuliza. "Kuna shida yeyote?"

Irene alieleza. "Nilisimama ili kulipia akaunti yetu pale Web Wonders. Polisi walikuwa kila mahali, bila kuwepo Web Wonders."

"Unasema nini, hakuna Web Wonders?" Rayford aliuliza.

"Hakuna kitu," Irene alisema. "Hakuna wafanyi kazi, hakuna afisi, hakuna jengo. Mabaki ya jivu tu, na yaliyokuwa matofali."

"Haiwezekani. Una uhakika ulienda mahali panapohitajika?" Rayford aliuliza, huku akisonga karibu na tarakilishi ili kujaribu anwani yake kwenye tuvuti.

"Hakika nina uhakika," Irene alisema. "Mimi huenda pale kila mwezi."

Neville alichagua huduma ndogo ya tuvuti kwa sababu ilikuwa ndio taasisi ya kipekee ya huduma za mtandao iliyokuwa ikikubali malipo kwa kutumia pesa mjini London. Irene alilipia akaunti zao kila mwezi.

Rayford alibonyeza ili kupata barua. "inaunganisha," alisema, huku wakijikusanya kando ya tarakilishi, na kusikiza mlio wa kawaida wa tarakilishi.

"Inajibu," Irene alijibu kwa mshangao. Walisikiza huku hayo makelele ya kuunganisha mitambo yakilia, na kadhalika kuashiria kwamba tarakilishi ilikuwa ikiunganika na mtambo mkuu kule Web Wonders.

"Wako na afisi nyingine mahali kwengineko?" Rayford aliuliza.

"Labda sifahamu," Irene alijibu. Mike ndio mwenyewe, na anafanya kazi hapo kwenye afisi iliyo makutano ya Clapham. Sijapata kumsikia akiongea kuhusu afisi nyingine."

Hapo tu, Neville aliwajulisha kutazama tarakilishi, ilikuw sasa inapokea mawasiliano na kiunganishi cha tuvuti kisichokuwepo!

"Tazama hapa!" alisema huku akigusa kio.

Ratiba ilionyesha kwamba Rayford alikuwa anapokea zaidi ya barua 200 katika ukurasa wake.

"Nimeangalia tu ukurasa huu saa moja iliyopita!" Rayford alishanga, Hatujawai pata kiasi kama hicho, hata wakati wa miezi sita." Alikuwa akiongea juu ya yale waliyopitia baada ya mkataba wa Hekalu kutiwa sahihi.

"Ni kweli tena!" Neville alieleza. Alitazama kila aina ya anwani zikichezacheza kwenye kio huku barua zikiingia kwenye ukurasa wa Rayford.

"Lakini zinatoka wapi?" Rayford aliuliza. Nini kilitukia kule Web Wonders? Unafikiri mamlaka inatukabili?"

Maswali hayo yalikuwa tu kebehi. Hakuna yeyote ndani ya chumba kile aliyekuwa na jawabu.

Ilichukua muda wa nusu saa kukusanya barua zile, huku hayo yakijiri, Neville alikuwa akiwaza jinsi ya kukabili barua nyingi kiasi hicho siku za usoni, iwapo zingaliendelea kuingia kwa kiwango hicho.

Rayford kwa upande mwingine alikuwa akiwaza iwapo wangalikimbia. Kulingana na wote, Huzuni Kuu ilikuwa imeanza. Ulikuwa ni wakati wao kukimbilia "Jangwa". Kilichotokea Web Wonder, kilikuwa ni dhihirisho la wazi kwamba utawala au mamlaka yalikuwa yamewapata.

Lakini waende wapi? Wapi mabawa ya kimiujiza kuwawezesha kupaa na kuepuka shida hii? Au ilikuwa tu kwamba walikuwa karibu kunaswa? Huduma yake ilikiwa imefikia kikomo?

Iwapo hitimisho lilikuwa limewadia, basi Rayford alikuwa tayari kupigana, sio kwa bunduki, lakini kwa ukweli. Kulikuwa na mengi yaliyokuwa yamejadiliwa kati ya wanachama wa makabila yale miaka tatu na nusu iliyopita. Sasa ulikuwa wakati wa kusambazia ulimwengu mzima.Iwapo angalisikizwa.

Baadaye usiku huo alikaa mbele ya tarakilishi. Hakufikiri sana kuhusu yale aliyoamini kuhusu Levi Xu Dangchao na utawala wake wa ulimwengu. Rayford alieleza kuhusu idadi ya herufi za jina la Dangchao, na kutabiri kwamba kiongozi huyo atafufuka, lakini watakachoona sio mwili wa binadamu. Itakuwa ni zombi.mzoga uliozingirwa na kukaliwa na Shetani mwenyewe.

Alitabiri kwamba utoaji wa kafara utakoma, na kwamba Dangchao atachukua mamlaka ya Hekalu, akijitangaza kwamba yeye atadumu. Baba Mtakatifu atatoa ombi kwa ulimwengu mzima kumuabudu Dangchao kama Masia wa Ulimwengu.

Yalikuwa ni matumaini ya ajabu, lakini Rayford alihisi kwamba hakuna muda wa kutosha, na alitaka kueleweka vyema kabla ya kunaswa. Ungalikuwa ujumbe wake wa mwisho duniani, na hata ikiwa alikosea katika maelezo yake mufti, alipaswa kupata ujumbe wake kuwafikia wale ambao angalishawishi: yaani iwapo Dangchao angalifufuliwa, angalikuwa yule Muasi wa Yesu aliyetabiriwa. Hakuna shaka. Angalikuwa ibilisi. Yeyote aliyemtumikia atakuwa ni shetani, iwapo walitaka kuona hayo au la.

Rayford aliona haja ya kumtumia Chaim makala yake kabla ya kuyachapisha kwenye mtandao. Alimuuliza Chaim kuweka kwenye ukurasa wake kwanza, ili ujumbe huo uweze kupatikana, endapo yeye angalinaswa au kukumbana na janga sawa na lilie lililopata wafanyi kazi wa Web Wonders. Chaim alitoa mapendekezo kadhsaa aliyoyakubali Rayford kabla ya kuchapisha.

Neville muda huo alikuwa akitazama msururu ule. Iwapo kulikuwepo afisi nyingine ya Web wonders na barua kuzidi kuingia kwa kiwango kile, basi walihitaji mashine ya kuchambua na kujibu. Alianza kwa kutunga barua ya kueleza watu kwamba hakuna haja ya kujibu, na kwamba wangalipata ujumbe wote walio hitaji kwa kuangalia kwenye mtandao. UKurasa utahaririwa kila siku bora tu ubakie kwenye tuvuti.

Iwapo watu walitaka kupata ushahuri kutoka kwa makabila kumi na mbili, basi walipaswa kumuomba Mungu ili awaelekeze jinsi ya kupata kuwasilisha barua zao. Hii ilikuwa ni kama kamari, na Neville akaomba Mungu kuwawezesha watu wanaostahili kuufikia ukurasa huo. Neville alitayarisha tuvuti ili barua zote zilizoanza na 7 kama herufi ya kwanza ikifuata na barua, ndizo zitakazo wafikia wanachama wa makabila kumi na mbili.ikitoa mojawapo ya herufi kumi na mbili zilizo sawa. Mbili kati ya tabaka za makabila hayo zilianza na J: Mike na Martin (tabaka la Kiyahudi) Matayo na Rayford (tabaka la Yosefu) watu waliotaka maelezo ya ukweli walipaswa kuandika Ju kwa Mike na Martin na Jo kwa Rayford na Matayo.

Barua ya Neville haikutoa maelezo kuhusu kile watu walihitaji kufanya ili kufaulu, iwapo utaratibu haungalizingatiwa, basi barua zao hazitapata kuwasilishwa. Ili baki kwa Mwenyezi Mungu kuwaelekeza watu walio na haki kile cha kuandika. Neville alielekeza watu kwenye ukurasa uliowafundisha jinsi ya kumtii na kumsikiza Mungu.

Hakuna aliyejua iwapo barua zitaeendelea kuwajia kwa kiwango kile, au iwapo wangalikuwepo kuzipokea.

Kwa sababu hii Neville na Rayford hawakulala usiku bali walilala mchana na Matayo na Irene kushika doria. Irene alifungua Redio kusikiza habari. Ukweli halisi ulikuwa kwamba kwa miujiza Dangchao alikuwa "ameamuka". Ripoti kutoka kwa Umoja wa Mataifa lilidhibitisha kwamba habari ya hapo awali iliongezwa chumvi, na kueleza kwamba Dangchao alikuwa anaendelea vyema baada ya kupokea matibabu katika Hospitali ya Hadassah, na alikuwa anapata nafu. Picha ilionyesha akitoka hospitalini huku hajafungwa sana kwenye jeraha.

Wakati huohuo, Dangchao alitangaza kwamba hali duni ya usalama iliyopelekea majaribio ya mauaji ilipaswa kutazamwa upya, na kufanya mabadiliko makuu katika Umoja wa Mataifa. Alitangaza Yerusalemi kuwa chini ya Umoja wa Mataifa, na kusema kwamba atatumia Hekalu kama makaazi ya "muda" na kama Makao makuu ya shirika hilo la dunia., kwa sababu eneo hilo ndilo lililokuwa salama mjini humo. Waandishi wa habari na vyombo vya habari vilikubali tukio hilo na kuunga mkono, kutokana na hofu iliyosababishwa na "mauaji ya siri". Hakuna aliyeuliza mbona uhamisho upelekwe Yerusalemi.

Baba Mtakatifu alinukuliwa kuunga mkono, huku akisema ulimwengu ulikuwa unakaribia dini moja, na ilikuwa bora iwapo dinio hiyo ingeshirikisha shirika kuu kama vile umoja wa mataifa. Kuwepo kwa Dangchao kwenye Hekalu ni ishara ya ule umoja, alisema.

Kulikuwepo pingamizi kutoka kwa baadhi ya makuhani wa Kiyahudi; lakini ajabu ni kwamba, kulikuwa na sauti za kuunga mkono. Wengine walisema kwamba Dangchao ndiye Masia aliyesubiriwa kwa muda mrefu. Kwa kiwango fulani alikuwa Myahudi, na alidhihirisha uwezo wake wa kuleta amani. Ilikuwa ni haki tu "mji wa Amani" ufanywe makaazi yake. Kuani hao ndio waliosikitishwa, hata hivyo Dangchao hakuwa tayari kutambua ukuani wao, kutokana na jukumu lake kwenye Hekalu.

Kwa yale makabila kumi na mbili, mtazamo wao ulikuwa tofauti. Kufikia saa za maankuli ya mchana Jumatano , wote kwa pamoja na wasimamizi wao walikuwa wamechukua tahadhari. Huzuni Kuu ilikuwa, kwa hakika, imeanza; ulinzi wa kikabila ulikuwa umekiukwa; na hawakujua mahali pa kuenda au kujificha.

Zion Ben-Jonah Aandika:

Watu wengi wamekosea kwa kuamini kwamba, wakati fulani siku za usoni, Mungu atadhihirisha nguvu zake kiasi cha kumtambua na kutofanya lingine ila kumuabudu. Kwa bahati mbaya, ukweli halisi sio hivyo. Lazima kuna nafasi ya shaka; na utabiri haukosi. Tazama utabiri kuhusu Yesu katika Agano la Kale. Hata sasa, baada ya miaka 2000, hakuna uhakika kamili katika sehemu nyingi.

Wengi wa walimwengu hawatajua kinachoendelea kiroho nyakati za mwisho kabla ya kurudi kwa Yesu. Hata wale watakao elewa watashuku baadhi ya utabiri na kukosa kuelewa, kama ilivyodhihirika kwenye sura hii. Lakini hapo ndipo wapaswa kuegemea nafsi zao.

Anachohitaji Mungu ni watu watakao muamini, kumtumikia na kumtumaini hata ingawa hawana jibu. Wale wafuasi 144,000 wanawakilisha haya. Mtu mmoja kati ya 50,000 atakayefanya kitu kifaacho, kwa sababu ki sawa, na sio kwamba wamelazimishwa kutenda.

Hata hivyo kitu kimoja tusicho paswa kufanya, ni kujaribu kutosheleza au kuharibu yaliyo tabiriwa. Sio kwamba hatuna uhuru wa kuamua, lakini ni kwa utabiri unatueleza yale yatakayo tokea kutokana na uhuru wetu.