Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

16. Mashahidi Wawili

Alhamisi asubuhi, Rayford aliamua kwenda kujionea eneo la Web Wonders. Alipanda gari la moshi kuelekea makutano ya Clapham na kisha kutembea hadi eneo alilofahamu kwamba ni afisi za Web Wonders. Polisi walikuwa wangali kwenye eneo hilo, ingawa vifusi vilikuwa vimeondolewa. Watazamaji wachache walikuwepo, wakijadili kilichotukia. Rayford alijongea karibu ili kusikiliza habari kuhusu kilicho sababisha.

Watazamaji hao walijua machache kuhusu kilichokuwa kinaendelea. Lakini punde tu alipofika mahali hapo, Rayford alimuona mtazamaji mmoja akiongea na askari huku akitoa ishara. Hakutaka kuwatazama moja kwa moja, lakini ilionekana kwamba mtu yule pamoja na Askari walikuwa wakielekea upande wake, na yule raia alikuwa akionyesha kidole kumuelekeza. Rayford alichagua kutulia. Aligeuka na kuenda.

"Wee! wewe hapo! Simama hapo ulipo!" Bila shaka walikuwa wakimuambia Rayford, lakini kwa kuwapa mgongo alijifanya kama kwamba hasikii, na kuendelea kutembea. Hapo tu askari wawili walitokea mbele yake. Alikuwa ameshikwa.

Aligeuka na kuinama huku akijinyoshea kidole, huku akitafuta maneno yakusema, "Mnaongea nami?" kwa mudomo wake.

"Ndio, tunaongea na wewe, jinga!" mmoja wa wale polisi alisema huku akimchukua kutoka nyuma kwa kiburi.

Alisukumwa karibu na yule mjulishaji, na Rayford akamtambua kama Nuhu, aliyekuwa mwanachama wa kabila la Yosefu. Nuhu aliama baada ya mabishano zaidi ya mwaka mmoja uliopita. Alikuwa amekiri kwamba kundi hilo lilikuwa dhehebu lisilo la kawaida, na kwamba viongozi wake walikuwa a kiimla. Rayford alikuwa awali akimuona Nuhu kule Liverpool yalipokuwa makaazi ya idara ya ugawaji. Idara hiyo iliamishwa, na huo ndio uliokuwa mwisho wa kumsikia Nuhu, au kumuona Nuhu. hadi leo.

"Ndio, ni yeye!# Nuhu alisema.

"Mnaongea juu ya nini?" Rayford aliuliza.

"Je una kitambulisho?" afisa wa polisi aliuliza.

"La, kwa hakika sina," Rayford alisema kwa uhakika.

Hakuona haja ya kubeba kitambulisho kwa wakati huo. Hawataweza kumpata Irene na wenzake iwapo hawakujua alipoishi.

"Unajua lolote kuhusu kulipuliwa kwa jengo hili?" afisa wa polisi aliuliza

"Mimi? La," Rayford alijibu, kwa kushangaa na swali hilo. Mbona walikuwa wakimuuliza yeye kuhusu bomu ilihali ni wao walio tekeleza?

"Nitakupeleka hadi kwenye kituo kwa maojiano," afisa wa polisi alisema.

"Nina shtakiwa?" Rayford aliuliza.

"Sio iwapo hautakuwa mkaidi."

"Sielewi. Nitajua nini kuhusu yaliyotendeka hapa?" aliuliza.

"Watu sita walifariki wakati wa mlipuko kwenye jengo hili siku tatu zilizopita. Tunaamini kwamba unazo habari kuhusu mlipuko huo. Unalolote la kuficha?"

Ilikuwa ni ajabu. Mamlaka hayo yaliamini kwamba Rayford Strait aliharibu Web Wonders? Ilionekana kama kwamba Nuhu aliletwa hapo kutambua wafuasi watakao fika pale. Rayford alikuwa amejiingiza kwenye mtego.

Kulikuwa na mengi yasiyo leta maana sawa. Polisi hawakuwa na anwani yake, ambayo ingalikuwa katika mojawapo ya orodha zilizokuwa Web Wonders. Na iwapo kulikuwa na afisi nyingine kwengineko, basi aidha hawangalitambua. Hata hivyo wangali pata maelezo kutoka kwa nakala za orodha. Rayford alikuwa mashakani, lakini maskani ya Neville na Maria yasije kuvumbuliwa.

"Kwenye gari, gaga wewe!" mmoja wa polisi aliamuru, na kumsukuma kutoka mgongoni.

"Eee, pole pole bwana!" alilalamika, akianguka chini na kujipanguza.

"Hii sio sarakasi, rafiki!" askari alijibu "Fanya tunavyokuelekeza."

"LA!"

Ilifanyika tena. Hatukuwepo na tahadhari wakati huu. Rayford hakuhisi njaa. Neno lilimjia tu kutoka kinywani alipokuwa ameketi.

Aliposema lile neno "La", miale ya moto iliwazingira wale polisi watatu. Miali ilikuwa kali sana na kuwajeruhi kushinda ilivyokuwa kule Neville.

Rayford alijiona kama aliye mashakani asipokimbia. Punde tu baada ya kutamka neno hilo aliruka na kukimbia. Alikuwa amefikia kona kabla ya umati kuona yaliyotendeka, hata hivyo hawakutaka kumkimbiza mtu anaye pumua miali ya moto.

Wale maafisa wengine wa polisi walikimbia kuwanusuru wenzao waliokuwa wakiteketea, lakini walichelewa. Askari watatu walikuwa wameuawa na mwanakombora. Askari hao hawakutaka kujumuishwa kwenye orodha ya Rayford, basi hawakuona haja ya kumfuata. Walipiga simu kuomba msaada.

Rayford alikuwa amefika katika makutano ya Claoham na kuchukua gari moshi kuelekea Guildford. Alikuwa na hofu, huku akiofia kwamba anaweza kuwa anaandamwa. Alikuwa pia akisumbuliwa na aliyowatendea wale askari watatu. Na sasa ilikuwa pia habari ya wale watu sita waliokufa kule Web Wonders. Nini ilikuwa ikiendelea? Alikuwa ameshiriki kuwaangamiza?

Ndani ya nafsi yake alielewa jibu. Alikuwa najibu yapasa miaka tatu na nusu iliyopita, lakini hakutaka kufikiri juu yake. Wakati wengine waliongea juu ya hayo, alibadili mazungumzo.

"Siwezi kumudu," angalisema. "Siwezi kufanya hivyo sasa, nitangoja hadi nifike mbinguni kupata maelezo." Alikuwa akiongea juu ya ule mlipuko uliotokea kwenye sebule ya Neville miaka tatu na nusu iliyotangulia.

Bibilia inaarifu kwamba wakati mwisho wa kipindi kile cha miaka tatu na nusu, tutakuwa na "Mashahidi Wawili" ambao watawindwa na utawala wa wakati huo kote duniani. Mitume hao wawili watakuwa na uwezo wa kuwakabili maadui zao kwa miale ya moto kutoka kinywani mwao. Watu wengi walitamani na kutumai kuwa manabii hao, lakini Rayford alionekana kuwa na sifa walizokosa wale wengine. Askari watatu katika makutano ya Clapham walikuwa tayari wamekufa kutokana na ushahidi wa sifa hiyo.

Rayford alipowasili kule Guildford, aliwasukuma wenzake na kuelekea moja kwa moja kwenye tarakilishi, alipomtumia Chaim barua iliyokuwa na alama "Dharura". Ndani yake alimuarifu Chaim kukatiza mawasiliano kupitia kwa huduma za tuvuti zingine ila tu kuunganisha na mtandao wa Web Wonders.

Kwa bahati utawala haukuweza kupata njia ya tuvuti aliyotumia Chaim. Akikatiza mawasiliano kule Australia, hawataweza kumpata huko. Watu hao wawili watakuwa wakiyaweka mayai yao kwenye kapu moja, lakini lilikuwa ni kapu lililotunzwa kimiujiza.

Lazima kulikuwa na afisi nyingine za Web Wonders ambazo hazikuweza kutambuliwa na mamlaka, au Mwenyezi Mungu aliandaa tuvuti yake kuwaunganisha makabila kumi na mbili. Rayford aliamini hivyo.

Kisha akarejelea dhamira kuu ya barua-pepe.

"Lazima nijue," aliandika, "Iwapo umepata kuona miale ya moto kutoka kinywani mwako unapoongea. Kuashiria iwapo wewe yu anayedhani yu, utajua ninacho sema."

Saa chache Rayford alitazama ukurasa wake kwenye tarakiliahi na kupata majibu.

"Ndio nimepata," ilisema. "Sasa tuende wapi kutoka hapa?"

Tuende wapi? Rayford alifikiri. Alikuwa amejiuliza hhivyo yapata wiki moja sasa. Orodha ya maswali ilikuwa ikongezeka kwa haraka kuliko majibu.

Walakini, iwapo yeye na Chaim walikuwa wale Mashahidi wawili, basi hawangaliweza kunaswa kwa urahisi. Kulingana na Bibilia, walikuwa na wakati mwema katika hiyo miaka mitatu na nusu, ili kuwafanya wasikike ulimwengu mzima, na kutumia wakati huo bora.

Kitu cha ajabu, kama alivyofikiri Rayford, ni kwamba watu wengi walitaka kutekeleza jukumu hilo (Hospitali za Akili punguani zilijaa watu kama hao) na kwa karibu, kazi ya "mashahidi wa nyakati za mwisho" haikuwa na kiinimacho walicho husisha watu wengi. Kwa sasa Rayford alikuwa akitambulika kama jitu linalopumua miali ya moto.

Chakutia hofu ni kwamba utambulizi huo ulikuwa karibu na ukweli.

Zion Ben-Jonah Aandika

Marejeleo kuhusu "Mashahidi Wawili" au Mitume (nyakati za mwisho) Wawili, yanaweza kupatikana kutoka kitabu cha Ufunuo wa Yohana 11:3-2. Wamelinganishwa na Elija na Musa, katika Agano la Kale. Yoyote atakaye kuwa miongoni mwao, bila shaka watakuwa na nguvu au uwezo wa ajabu, ili kutimiza mamlaka yao. Katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana tunaelezwa kwamba Mitume hao wawili watatabiria ulimwengu kwa siku zile 1,260 za mwisho (Miaka mitatu na nusu au miezi 42) wa miaka ile saba kabla ya kurudi kwa Yesu.

Kwa sababu ni kawaida kwa watu wendawazimu kudai kwamba hao ni "Mashahidi", makanisa mengi yamekatisha maongezi ya Mashahidi Wawili. Lakini wale halisi hawapaswi kudanganywa na wasio wa kweli. Kuwepo au kokosa kwa wenye akili punguani, tutakuwa na mitume wawili nyakati za mwisho wakieneza ukweli kwa walimwengu.

Ni dhahiri kwamba ni mashahidi wawili na manabii wa uongo nyakati za mwisho wataendesha shughuli zao bila ushirikiano.kwa sababu tamaa zao na kujitakia makuu hakutaruhusu kushirikiana na kusikiza wenzao.

Kuna usemi mmoja katika Bibilia kwamba kila kitu cha kiroho kuweza "kudhibitishwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu", (Matayo 18:16, Wakorintho wa pili 13:1, Timotheo wa kwanza 5:19, na Wahebrania 10:29)

Iwapo itatendeka kwamba mmoja lazima atekeleze kibinafsi, basi kutakuwa na dhibitisho kamili kwamba nguvu za ajabu zitajulikana kama "shahidi" wa pili. (Yohana 5:36)