Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

17. Dangchao

Levi Xu Dangchao alikuwa akijadili mipango na Baba Mtakatifu Pius XIII, aliyekuwa amehudumu kwa miaka mingi kuliko Dangchao aliyekuwa Katibu wa Umoja wa Mataifa. Walikuwa katika makazi ya kibinafsi ya Baba Mtakatifu Yerusalemi.

"Kichwa chatarajiwa kuwekwa kwa sanamu iliyo mbele ya kanisa kuu la jimbo la Askofu Kesho asubuhi. Ni kweli?"

"Ndio hasa," alijibu Pius. "Jana kilimiminwa kwa kalibu, na kitawasilishwa leo"

"Nina kichwa cha badala kwa sanamu" Dangchao alisema kwa kiburi.

"Kichwa kingine?" Baba mtakatifu aliuliza kwa mshangao. "Wamaanisha nini? Kwanini tuhitaji kichwa kingine?"

"Ninamaanisha kwamba niko na kichwa kingine kilichoandaliwa kwa sanamu, nataka kitumiwe badala."

"Lakini mbona? Nini mbaya na kile tulichonuia kutumia?"

"Nini mbaya?" Dangchao alijiuliza kana kwamba anatafuta jawabu. Aliangalia nje ya dirisha kwa muda, Kuongeza sarakasi kwa yale yatakayotokea, aliongeza tena kimzaha na kwa upole. "Nini mbaya na kichwa kilichoidhinishwa na Pius?"

Aligeuka na kumuangalia Baba Mtakatifu Pius. Uso wake ulibadilika na kukunjamana. Sauti yake ilikuwa nzito na ya kukwaruza.

"Nini mbaya kwani sio mimi!" aliguna.

Pius alirudi nyuma kwa uoga. "Xu! Nini kimetendeka kwako?" aliuliza. " Uso wako.!"

Dangchao alipoa na uso wake kurudia hali yake nzuri ya upole.

"Wapenda hiki zaidi?" aliuliza.

"Ulinishtua," akasema Baba mtakatifu, akijiliwaza kwa kuona Dangchao akirudia hali ya kawaida.

"Hilo ndio lengo langu," Dangchao alijibu. "Watu wengi huniamini, Pius. Wewe waniamini au sio?" Pius alitingisha kichwa kukubali shingo upande bila hakika.

"Ningalipenda wewe uniogope," alisema Dangchao. "Ningalipenda wote waniogope.

Na itakuwa hivyo, " aliongezea baadaye.

Pius alijaribu kurejelea mazungumzo ya awali. "Haya yote yanahusu nini sanamu ya Bikira Mtakatifu?" aliuliza.

Dangchao aliongea kwa unyenyekevu, kama kwamba anamuongelesha mtoto. "Yote ni kuhusu sanamu, Pius. Waona, sio sanamu ya Bikira Mtakatifu bali ni sanamu yangu."

"Sijui kama hiyo itafaa, Baba Mtakatifu alijibu. Kanisa halioni shida kwa kutengeneza sanamu za mitume; na Dangchao atatunukiwa hivyo siku moja. Lakini sanamu hii ingelikuwa mojawapo ya sanamu kubwa iliyowai kutengenezwa na kanisa, ilikuwa haki kumtunuku Malkia wa Mbinguni, na wala sio katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, hata ikiwa ni kiongozi anayetambulika na kuheshimiwa hapa ulimwenguni.

"Wataka kuiona sura yangu nyingine tena?" Dangchao aliuliza, Kwa mara nyingine akiongea na Baba Mtakatifu kama kwamba anamkaripia mtoto. "Fahamu sijakuuliza. Ninakuambia.

"Wewe umepata kanisa kuu la kiaskofu na makao hapa Yerusalemi. Hata hivyo nahitaji makao hapa vilevile; na itakuwa jinzi nitakavyo."

Basi, baada ya muda, sura ya ukali na uchovu ikaonekana. Kulikuwa na hali ya kutatanisha chumbani humo, Baba Mtakatifu Pius alikumbwa na uoga kiasi cha kuona na kushika.

"Je waelewa?" aliguna kiumbe Dangchao.

"Ndio.ndio! Ninaelewa," Pius alisema kwa hofu tele.

Lakini hakuelewa. Angalielezea ulimwengu vipi?

"Utaona," Dangchao alisema, wakati swali lilipoulizwa baada ya kurejelea hali yake ya kawaida. "Watakubali, jinsi ulivyokubali. Labda hawatafurahia, lakini watakubali. Na watakubali mengi kabla ya hatujamaliza."

Dangchao aliendelea mbele kumuelezea Baba Mtakatifu jukumu la Pius katka utawala mpya.

"Lengo kuu la dhehebu kwa kawaida ni kutilia mkazo uhalali wa mamlaka ya utawala," Dangchao alieleza. Na jukumu lako sio kinyume.

"Kitu ambacho kimetendeka kwa wakati huu wa mpito ni kwamba nitatoa vazi. Nimechoka na ukafira. Nataka watu wanione jinsi nilivyo, na pia nataka waniogope".

Ndio mwanzo ilikuwa inamfikia Pius kwamba anaongea, ana kwa ana na yule asyependa Kristo. Kanisa halijatilia mkazo mambo kama haya. Hawataki kutafakari juu ya wanautamaduni. Kwa sasa Pius alikuwa akikabiliwa na ukweli halisi; hakuwa tayari kukabili tukio kama hili.

Kwa hivyo alikuwa amedanganyika kuelekea Yerusalemi. Alikuwa huku kwa minajili ya kuweka wakfu utawala wa mtu huyu mkatili. Iwapo Dangchao kweli alikuwa mwanaume.

Lakini Pius hangerudi Roma. Hata akijaribu, je Dangchao atamuachilia? Alikuwa amehisi sekunde chache za hofu ambayo Dangchao alikuwa amemtia kwa kuwepo hapo, na kufahamu kwamba jitu hili halingalimwachilia kwa urahisi. Alikuwa mtumwa wa Dangchao, na hatukuwa na njia yeyote.

Kwa sasa hivi hakua na namna bali kufanya vile ilivyotakikana.

Kile kichwa cha sanamu kiliwasili, na Pius akasumbuliwa sana kuona sura hiyo ilikuwa uso wa Dangchao na wala sio ule alionuia. Ama uso huo wa kijificho ulikuwa wa hakika?

Dangchao alijibu swali hilo baadaye siku iliyofuatia walipokuwa na Pius.

"Ili kufikia mahali nilipo hivi sasa," alieleza, "Nimeweza kuvaa barakoa za kila aina. Na zote kuonyesha mtu mzuri.

"Lakini mimi sio mtu bora. Sitaki hata watu kufikiri mimi ni mtu mzuri. Nataka waniogope. Nataka niweze kuwaongoza. Na ninataka kutekeleza hayo bila kujifanya mimi ni mzuri.

"Waona Pius, huo ndio ukweli halisi wa kuwa katika mamlaka. Mtu yeyote anaweza kuongoza watu wanao muamini. Lakini nataka kuwatawala watu wanao niogopa. Waniogopa, au sio?"

Pius hakuwa na lakusema, ila kukanganya azimio lake la awali la imani yake kwa Dangchao na kutikisa kichwa kuhafiki uhusiano mpya na kiongozi wa dunia.

"Ndio waniogopa," Dangchao alisema kwa tabasamu. "Watafuta njia ya kuepa. Lakini bila shaka hakuna, au sio? Utaenda wapi? Nina tawala ulimwengu, niko na uwezo huo hata ikiwa watu kama nyinyi hamtaki.

"Nimeweza kufaulu kufanya haya kutokana na alama. kutokana na alama," alijivuna.

Mtakatifu Pius alionekana kama aliye zuzuliwa, lakini hakudhubutu kuuliza swali lake. Hata hivyo, Dangchao alibahatisha alichokuwa akifikiri.

"Swali lako iwapo alama ni yangu?" aliuliza. "Ni sababu unaona tu alama na kusahau ukweli ulio nyuma yake. Uso wa Dangchao sio sura yangu, Pius. Umeona mimi halisi. Je ninafanana na Dangchao? La hasha. Nilichukulia mafao ya mwili wake.

"Oh, kwa hakika alishirikiana nami vizuri kabla ya kufa kwake, kama wewe, na waliokutangulia, mmefanya hivyo tangu jadi. Ilikuwa tu baada ya kifo chake cha ghafla ndio nilichukua mwili wake.

"Lakini alama. Nimekuwa nikifanya kazi zaidi ya miaka elfu. Ni ishara ya utu kunitegemea, na inaelekea kukamilika. Ndio Pius, ni alama yangu na, ninatawala ulimwengu kwa alama hiyo."

Dangchao alimlazimu baba mtakatifu kukiri kwamba ulimwengu mzima unamuabudu, na kwamba waweze kuabudu sanamu yake. Ile sanamu ya Maria mbele ya kanisa kuu la jimbo la askofu ilitakiwa kubadilishwa na kuwa sanamu ya Dangchao au mnyama aliyekuwa Dangchao.

"Usijifanye mtakatifu," Dangchao alisema, wakati Pius alisema kwamba hivyo ni kumtukana Mwenyezi Mungu. "Mmekuwa mkimuabudu Maria kwa karne nyingi, na yeye sio mtakatifu jinsi nilivyo. Misa haikunung'unika kuambiwa kwamba Maria ni mamake Mungu? Iwapo uliwafanya kuamini hivyo, mbona usiwaambie kwamba umepata Ufunuo wa Yohana kwamba mimi ni Babake Mungu?"

Kwa hayo Dangchao aliangua kicheko cha kishetani kilicho mugandamiza Baba mtakatifu Pius XIII kwenye mifupa.

Zion Ben-Jonah Aandika

Ufumbuo kuhusu `Joka la mabawa' kufukuzwa kutoka mbinguni. (Ufunuo wa Yohana 12:7-9) Joka hilo laja ulimwenguni na kuanzisha vita kati ya Kanisa, au "Bi arusi" wa Yesu. (Ufunuo wa Yohana 12:12-13) "Joka" hili kwa hakika ni shetani, aliyekuja kupiga Mungu vita na wote wanaomuamini Mungu. (Ufunuo wa Yohana 13:5)

Joka hilo litachukua umbo la mwanadama aliyepata "Jeraha la kutisha". Mwili huu ulio na shetani ndani yake huitwa "jitu". (Ufunuo wa Yohana 13:3)

Ibilisi huyu anasaidiwa na "Manabii wa Uongo" (Ufunuo wa Yohana 16:13), wanaopelekea ulimwengu wote kumuabudu ibilisi na sanamu zote alizojenga. (Ufunuo wa Yohana 13:11-14)

Kama vile tutakavyoona kanisa lisilo la kweli likiwa sambamba na Kanisa la Mungu ndani ya miili ya wateule, ndivyo hivyo tutakavyoona manabii wa uongo wakiwa sambamba na kufanya kinyume na Manabii wa kweli siku za mwisho.

Huku waamini wa hakika wakimuamini Mungu wasiye muona, wale wasio wa kweli wataabudu miungo na sanamu, na kuweka imani yao kwenye alama (au pesa) kukidhi mahitaji yao. (Waefeso 5:5)

Jambo la kujivunia kuhusu wale wasiomuamini Yesu, ni kwamba, yote hayo yatafikia kikomo. watu watalazimishwa kuchukua muelekeo, upande mmoja au ule mwingine. Hakuna mapatano, masikilizano au kutokuwa na hakika. Hakuna kuita uovu wema na kuita wema uovu! Shukuru Mungu kwa hayo.