Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

18 INJILI

Alipokuwa amerejelea hali yake ya utulivu, akipanguza machozi yaliyokuwa yakimbubujika, wakati aliangua kicheko, Dangchao alizungumza zaidi kwa Baba mtakatifu.

"Nitahitaji usaidizi wako na jambo jingine dogo", alisema.

Tunalo dhehebu ambalo limekuwa likisema vitu vibaya kunihusu miye na serikali yangu. Tumejaribu kuwaandama kwa Mtandao, lakini waliharibu nyumba nzima iliyokuwa na hifadhi ya mtambo wa mtandao kabla ya kunakili anwani yao. Wanajiita Jamii ya koo kumi na mbili. Una habari gani kuwahusu?"

Kanisa liliweka rekodi kubwa kuhusu makundi yote mapya ya kidini, katika afisi zake kule Roma, lakini mbona, aliwaza Pius, amsaidie Dangchao? Je, iwapo watu hawa wangesaidia kumsimamamisha huyu mtu mbaya? Wangalifanya hivyo, basi angaliwasaidia kuliko kumsaidia Dangchao.

Katibu mkuu alipumua kwa ndani huku akichukua muelekeo mpya ambao Pius angekuwa akifikiria. Angalilazimika kucheza mchezo wa Pius kwa mara nyingine, kama alivyokuwa amefanya mara nyingi miaka iliyopita, ndiposa ana uwezo kwa Baba mtakatifu.

"Lolote lile unaloweza kufikiri kunihusu", alisema kwa ukarimu.

"Ukweli wa mambo ni kwamba hili ni dhehebu baya sana."

Tayari wamewaua watu tisa ambao tunajua na tuna habari kuwa kuna wengine ambao wameuawa kule Australia pia. Pius tafadhali! Ungekuwa unasaidia ulimwengu huu iwapo ungalitusaidia kuwasimamisha"

Pius alifikiria kwa muda kisha akaamua kuwa ikiwa angalikuwa anaelekea kuwa bingwa, hii isingalikuwa sababu nzuri au wakati mwafaka kuchukua hatua. Angalimsaidia Dangchao mara hii, angeshinda kwa kumpendelea. Basi angeweza kutumia hayo mapendoleo kupata uzuri zaidi wakati mwingine.

Dangchao alitabasamu. Uwezo wa kufurahisha tangu kitambo haukukosa kufaulu. Mfanye aendelee kuchelewa na angeweza kumkabili milele.

Kwa muda wa saa moja na nusu, Pius alikuwa na habari kamili kuhusu ndugu kumi na mbili kupitia kwa barua-pepe kutoka Roma, lakini alikuwa na usaidizi mdogo kwa wote wawili.

Wadadisi wa Kikatoliki walikuwa na jarida ndogo kutoka siku za Jeseni ambalo lilikuwa na jina la Reinhard. Hata hivyo, karibu habari yote waliyokuwa nayo kuhusu vuguvugu la koo kumi na mbili, ilikuwa inapatikana kwa Mtandao wa koo kumi na mbili.

Licha ya majaribio ya kamati mpya ya kanisa kuhusu makundi, kuwashawishi wa Jesani halafu koo kumi na mbili kutoa habari zao za ndani, hatukuwa na majibu kutoka kwa Reinhard, Rayford au Chaim. Hata majina yao hayakujulikani kwa sababu Rayford na Chaim walizoea kutoweka sahihi kwenye barua. Kamati haikuwa imepata kitu chochote hatari katika yale waliyokuwa wakifunza, kwa hivyo kamati haikufafanua zaidi. Tulikuwa na waliosema kuwa vuguvugu lilikuwa kubwa, kufikia idadi ya mamilioni, lakini kuna wengi walioamini kuwa hii ilikuwa ni ndoto, iliyosababishwa na watu waliotaka kutoa wazo kuwa kundi hilo lilikuwa kubwa kuliko lilivyokuwa. licha ya hayo hapakuwa majengo, hatukuwa na anwani za posta, hapakuwa kumbukumbu za mikutano, hapakuwa majina ya viongozi au wafuasi kando na Reinhard na wachache waliokuwa wafuasi mbeleni. Ilikuwa ni ukweli kuwa walitengeneza maandishi mengi, lakini maandishi yao yalipeana tu anwani ya mtandao.

"Tumeweka baadhi ya watafiti wanaotumia Tarakilishi walio bora ulimwenguni kwa kazi hiyo, na wao wote wamekwama".

Dangchao alilalamikia Pius walipokuwa wamemaliza kusoma ripoti kutoka Roma.

"Kila kitu kinaonyesha kwamba mtandao unashangaza, mtambo wao haupo lakini mtandao wao unafanya kazi. Ni kama hatuna maarifa ya kusimamisha.

Hata hivyo wanamgambo wa koo kumi na mbili walikuwa wamezunguka kwa kasi sana. Kasi hii iliongezeka kwa miezi michache iliyofuatia. Kila wakati, habari nyingine kuhusu Dangchao kutoka kwa vyombo vya habari ilijitokeza, Maelfu zaidi wangalitembelea mtandao wa koo kumi na mbili ili kupata habari motomoto kutoka kwa wale mashahidi wawili kuhusu yaliyokuwa yakiendelea.

Je, Dangchao alikuwa ameonyesha ujasiri kupita kiasi? kuashiria kwamba vyombo vya habari havikujua jinsi ya kuitikia kwa ripoti kuwa Dangchao alikuwa mbabe, au jambo jingine lolote jeuri kuwa yeye na Baba mtakatifu Pius walikuwa wanaelekea Yerusalemi.

Ile sanamu ya kuogofya na kile kichwa cha gargoyle na kiwiliwili cha kike, ikidaiwa ni sanamu ya Dangchao, ilishangaza ulimwengu, lakini ilikuwa tu mwanzo wa maajabu na mishangao mingine.

Dangchao alirarua patakatifu pa utakatifu kutoka kwa hekalu, na akajiwekea pale kiti cha enzi akalie huku akiabudiwa na kutamaniwa na uma. Aliwaalika watu wa dini zote na wale wasiokuwa na dini waje kumuabudu, kwa hivyo aliharibu uhusiano wake na viongozi wa kiyahudi waliotarajia kuwa angekuwa mkombozi wao.

Alisisitiza kwa kutoa burudani kwa wageni wake na chaguo lake la burudani lilikuwa la kufukuru waziwazi. Kwanza ilikuwa nyimbo ya kumsifu yeye kama mkombozi wa ulimwengu, kisha nyimbo hizo zikaanza kumkejeli mungu halisi. Wachezaji waliletwa, ambao walizidi kuashiria ngono katika shughuli zao. Madawa kali ya kulevya yalitolewa bure kwa wageni. Katika muda wa miezi chache tu, Dangchao alikuwa amejumuisha vitendo vya ngono hadharani na matendo mengine ya kutia najisi katika mpangilio wa hekalu la kiyahudi.

Lakini jambo la kushangaza kwa yote ni kwamba, watu walikuwa wanaikubali. Kwa mfano alikuwa ametabiri kuwa hata wale waliochukia matendo yake walikuwa wadhaifu sana kwa tabia na hawangeweza kumpinga.

Kulikuwa na wale walioenda kumuabudu kwa wingi na kushiriki katika sherehe zake zilizojaa kelele na ulevi, kwa furaha iliyokuwa wazi. Miongoni mwa watu walio hudhuria walikuwa wanadiplomasia, na watu walioheshimiwa sana kuonekana katika mojawapo ya sherehe najisi za Dangchao.

Ilikuwa imeripotiwa kwamba katika baadhi ya matendo makuu yaliyoendeshwa kwenye hekalu, umbo lake lote lingalibadilika kisiri na watu wangalifahamu mara moja kwa hofu baadhi ya nguvu za kiajabu alizokuwa nazo.

Vyombo vya habari, ingawaje viliduwaa, havikuwa na nguvu au uwezo wa kufanya chochote ila kutangaza yaliyoendelea kama kwamba ilikuwa tabia ya kawaida kutoka kwa kiongozi wa ulimwengu. Dangchao aliyeonekana kuwa na uwezo wa kufanya kazi siku nzima na kusherehekea usiku kucha, alikuwa na benki na washiriki muhimu wa umoja wa mataifa mfukoni mwake. Kati ya hizi jumuiya, aliumiliki ulimwengu na wala hakuna yeyote aliyedhubutu kumpinga.

Hata, hivyo, msimamo wake wa hadharani kumpinga Mungu na majaribio yake ya kuchukiza kwa wepesi, ndio iliwafanya mamia ya maelfu ya watu kutafuta wasia wa koo kumi na mbili na maelezo. Hapakuwa na taashishwi yoyote zaidi kuhusu alikotoka Dangchao. Alikuwa mpinga Yesu kamili aliyedhihirisha uovu. Neno lilisambaa kote ulimwenguni kuhusu mtandao wa kumi na mbili. Anwani yake ilipakwa (chini ya giza) katika kuta na mabango popote pale waumini 144,000 wangepata nafasi ya kujaa.

Kwa hivyo, watu walipoona yaliyokuwa yakitendeka Yerusalemi wangaliwageukia Rayford na chaim kuwafafanulia. Kwa muda mfupi, hakika mamilioni ya watu walikuwa wakitembelea tuvuti au mtandao ambao ulikuwa kiwasilishi rasmi cha mashahidi wawili wa Mungu wa siku za mwisho.

Watu wachache walikuwa wamegundua ishara ya siri katika anwani pepe ya Neville na walikuwa wameweza kuwasiliana kwa barua moja kwa moja na koo. Watu hawa walikuwa wanashugulikiwa kibinafsi. Wengi wao walikuwa hawajapata alama kwa hivyo wakachukuliwa haraka kwa ushirika, kwa dhana kuwa mungu alikuwa amewakinga kutowekwa alama na pia alikuwa amewezesha kuwasaidia kugundua ishara ya siri ya anwani-pepe. Kwa kuzingatia dhana hii, watu hawa hawakuwa tisho kwa usalama.

Kati ya ishara ya siri ya anwani-pepe na kukosa jina kwa mtandao, wale 144,000 hakika walikuwa wametorokea 'jangwani' mwa usalama kutoka kwa watawala. Mungu mwenyewe alielekeza wale wangaliowafikia, na ulimwengu uliosalia ulifungiwa nje.

Mbali na wachache waliotawanyika na wengi katika mashambani na wasiostarabika vijijini mwa ulimwengu wa tatu, hakika, kila mmoja ulimwenguni alikuwa amepolea alama hadi wakati huu. Ilikuwa vigumu kufanya biashara bila alama hiyo. Wale koo kumi na mbili ambao hawakufaulu kupata kodi ya bure kutoka kwa marafiki binafsi katika jumuia, walikuwa wakilazimishwa kukaa kwa njia katika mitaa au kwenye mahema na kwa makaazi mengine ya dharura. Lakini kwa jumla walikuwa wakiishi bila matatizo yasio ya lazima, kwa kutumia sheria ya kuomba, kubadilishana na kuiba mahitaji ya kimsingi ya maisha katika huu mpangilio mpya wa dunia ulio muovu na wazimu.

Watu waliokuwa katika shida kuu ni wale waliokuwa wakiwasiliana na koo kumi na mbili kwa kukosa matumaini. Yale waliyokuwa wamesoma kuhusu ile laana juu ya wale waliochukua alama ilikuwa hakika imewaweka katika hali ya kukosa imani kiroho. Walikosa mbinu yoyote ya wokovu, na walikuwa wakiishi katika dunia iliyokuwa inakua haraka katika uovu kila siku.

Dangchao alirudisha michezo ya kitambo ya waRoma, ile ya kupigana hadharani na watu wengine au wanyama ambapo wapiganaji walipigana hadi kifo.

Pia alikuwa amepanga kuonyesha mateso ya hadhara na mauaji huko Yerusalemi kupitia kwa kama burudani. Lakini watu wengi ambao hawakuwa wamemfikiri Mungu kwa dhati awali, walikuwa wanachukizwa na haya yote na hawakutaka.

Kwa hivyo, Chaim na Rayford walitoa mpango wa wokovu uliokuwa umegusiwa katika ujumbe kwa wale 144,000. Ulikuwa ndio ujumbe tangulizi kwenye mtandao na kushtua ulimwengu.

Haya ndiyo aliyoyasema:

"Mpango wa Mungu wa wokovu si tofauti na vile ilivyokuwa. Unahitajji kumpokea Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu na pia kama tegemeo la pekee la wokovu".

"Tofauti (Kwa wale wanaojua kitu fulani kuhusu yale yaliyokuwa yakichukuliwa kuwa Ukristo) ni kwamba hatuzungumzi kuhusu kujisingizia katika imani, wakati huu. Kumpokea Yesu ni maana ya kupokea kila alilosema. Mafundisho yake ni sehemu muhimu ya mpango wa Mungu wa wokovu kwako. Soma mafunzo yake na utagundua kwamba anatarajia imani kamili. Kanuni zake ziko juu lakini anachopeana ni uzima wa milele. Hakuna gharama iliyo juu kwa hayo."

Rayford alieleza kwamba kusulubiwa kwa Yesu msalabani, kulipelekea kutoa wokovu kwa yeyote aliye hitaji; lakini haikumpasa Yesu kuchagua yeyote. Alikuwa akiangalia viwango fulani.

"Mengi ya madhehebu yenu yamefundisha kwamba Mungu wa Upendo hawezi kuweka viwango, kutaka kwa lazima au kuweka "zawadi" kwa yale anayotoa," alisema. "Lakini wamewapeleka wapi? Wamewasukuma kwenye ukingo wa kuangamia. Yale waliyofundisha yalisikika kama 'habari njema' kwa wakati ule, kwa sababu ilikuwa rahisi. Lakini imebadili kuwa janga kuu.

"Kinyume na hayo, injili aliyofundisha Yesu ilikuwa ukweli halisi na habari njema, hata iwapo haikuwa rahisi. Ilikuwa ni habari njema kwa sababu ujumbe huo ulijaribu ulifanya yale tuliyo puuza katika maisha. Aliona upuuzi na udhaifu wetu. Aliona kwamba , kwa matukio yanayotokea hivi sasa au la, siku moja utaaga dunia, na kushtakiwa kwa kukosa kufuata Mwenyezi Mungu. Alijua kwamba zawadi aliyokuwa akitoa. msamaha, na maisha ya milele katika nchi ilyo nzuri, ya kupendeza na kutosheleza kuliko ulimwengu huu wa sasa.

"Je ni dhamana gani anayouuliza? Anauliza uwache yote, yaani utoe kila kitu ulicho nacho. utajiri wako, maisha yako, jamii yako na marafiki na hata maisha yako.

Uchukue ama uwache. Hiyo ndio dhamana. Imekuwa ni malipo yake, na itabakia gharama yake. Toleo hili lingali wazi kwako. Lakini hakutakuwepo udanganyifu wakati huu.

"Wengi mnaosoma ujumbe huu mtafahamu na kukiri alama ya mnyama, katika mkono wa kulia au kwenye paji la uso. Wengi wenu mnafahamu kwamba Bibilia inasema kwamba, yeyote atakaye pata alama atapokea adhabu ya Mwenyezi Mungu, na utachomwa na kusaga meno mbele ya Yesu na malaika watakatifu. Utatupwa kwenye ziwa la moto, na kuungua milele. Hivi ni vitisho vya kweli. Huwezi kufikiri kwamba huo ni 'upendo', lakini kumbuka. hautaweka sheria; Mungu ataweka. Kabla ya kukubali hayo hautapata kufahamu jinsi anavyotupenda.

"Sasa haya ndio maelezo ya habari njema ya Yesu Kristo kwenu nyinyi mliopokea alama ya mnyama. Ina maana kwamba ukubali kukatwa mkono wa kulia au kukatwa kichwa kwa ajili ya neno la Mwenyezi Mungu!

"Hiyo ndio kweli halisi. Yesu alisema kwamba, iwapo mkono wako wa kulia utakukera, basi ukate. itakuwa bora kuingia ufalme wa mbinguni bila mkono, kuliko kuelekea jehanamu kwa maelekezi ya mkono wako wa kulia. Kwa miaka mingi watu wamechukulia usemi huo kama kwamba hakutaka tuuchukulie kama jazanda. Lakini sasa ni jukumu la kila muumini au mfuasi kila mahali kudhihirisha imani yake kwa matendo.

"Labda wengi wenu hamjapata kusikia ilani kuhusu Alama ya Mnyama. Lakini mmesikia sauti ya Mungu kupitia kwa nafsi zenu, na kisha kukaidi. Kwa sababu moja au nyingine muliamua kufuata njia zenu, kusonga mbali kutoka kwa maadili ya ujana na maadili ya dini zenu. Na ni kutokana na kukosa imani na muelekeo wa kuchanganyikiwa ndiposa mmejikuta mahali mlipo.

"Kumbuka Mungu hajauliza chochote kile ambacho hajawai kuuliza mtu yeyote. Tofauti ni kwamba sisi tunaoandika tulisikiza , ule moyo wa kiroho cha ndani kwa makini kabla ya kukubali Alama ya Mnyama, na kukataa kukubali. Tulimkubali Mwenyezi Mungu na mafundisho ya Mwanawe."

Kwa hakika tulikatiziwa na twazidi kukatiziwa kwa uamuzi wa kuweka Mwenyezi Mungu mbele. Lakini kwa jumla tumeibuka na kuwa mbele. Wewe unaye soma ulichelewa kutoa uamuzi, ukidhani kwamba ni vigumu au inakatiza mipango yako kwa kumuweka Mungu mbele, na kisha kujiletea haya yote."

"Tunaweza kuhitimisha kwa kukueleza kwamba uamuzi huu unafaa na ni kweli. Mbingu ni hakika. Yesu ni mwana wa mungu. Yale anayotoa ni hakika. Uzima wa milele. Upendo wa milele. Amani ya milele.

"Lakini mapatano halisi ya hayo yote yatahitaji kubadili hali yako ya maisha. Uamuzi ni wako.

Zion Ben-Jonah Aandika

Maelezo mengi na ufafanuzi kuhusu Alama ya Mnyama yazidi kutolewa na jinsi Wakristo wapaswa kuchukulia, na kisha kuepuka adhabu kwa kutenda hivyo. Yote huzungukia "Hisani ya Mungu", na jinsi Mungu wa Upendo hawezi kumtia adabu yeyote atakaye sema Bwana Bwana kwa Yesu. hata iwapo hawajapata kumtii au kujaribu kumfuata. Lakini fundisho kama hilo ni kinyume cha hekima ya Mungu, na kufanya stihizai kwa yote yaliyo kwenye Bibilia (na hasa Yesu) kuhusu imani.

Inaweza kuchukuliwa kwamba kukubali Alama ya Mnyama (kama inavyoelezwa kwenye kitabu cha ufungua) yatosha kumpeleka mtu kwenye ziwa la moto wa milele, bila matumaini yoyote. Lakini yale Yesu alieleza pale kwenye mlima kuhusu kuukata mkono iwapo umekuudhi (Matayo 5:30) yatoa ufafanuzi kuhusu gharama ya "nafasi" ya pili. iwapo kutakuwepo kitu kama nafasi ya pili.

Jambo la muhimu ni kwamba, iwapo unachukua muda mwingi kuweza kumuamini Mungu, ndiposa utapata shida nyingi. Nani anayeelewa kwamba hakuna fursa ya kuungama dhambi kule jehanamu? Lakini nani atataka kuingia huko ili ajionee?

Bibilia inasema,"Sasa huu ndio wakati, Wakati wa wokovu ni leo. Leo hii ukisikia sauti yake usifanye roho ngumu kama wale Waisraeli walipokuwa jangwani, na kumfanya Mungu akasirike." (II Wakorinzo 6:2 Wahebrania 3:7-8, na Wahebrania 3:15)