Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

19. Msukumo wa Mahangaiko

Wanachama kumi na watano wa tabaka lile walijikusanya kwenye ukumbi wa nyumba ya mafunzo kule Sao Paulo. Fanicha ziliondolewa ili kuwepo nafasi kwao, na pia sehemu ya juu ya Meza isiyo na matende-guu katikati ya ukumbi ule. Ilikuwa na kamba za ngozi zilizofungwa kila upande.

Luis alikuwa amewasili kutoka Rio asubuhi ile. Kule Rio alikuwa amemuona muuguzi akitenda hayo mara mbili, kabla ya kutwikwa jukumu la kutekeleza mwenyewe. Sasa katika muda wa wiki mbili alipaswa kuwafundisha wenzake, jinsi ya kufanya. Kulikuwa na orodha ndefu ya watu waliokuwa wakisubiri kule Sao Paulo, huku watu wengi wakijaribu mtandao na kuomba msaada wa kuepuka Alama.

"Uko na kauli mbili tu," Luis alimueleza mgonjwa wa kwanza kumtembelea asubuhi ile, huku wengine kumi wakimskiza. Wote walikuwa wameletwa pale bila hiari yao na kwa kidota. "Tunaweza kutoa ngozi ya mgongo, au kuuchukua mkono wote. Tuna uhakika wa kupachika chembechembe kwa asilimia tisini kwa kutoa ngozi, na yaweza kufanya bora hata chini ya misuli"

"Tafadhali hapana, amogo! Toa yote!" mgonjwa yule aliomba, mkulima maskini wa umri wa miaka 40 hivi, kwa jina la Joaquin.

"Mashetani, wako kila mahali," aliendelea. "Siwezi kulala. Siwezi kufikiri. Tafadhali iondoe yote. Mungu, nisaidie!" na macho yake kuangalia mbinguni.

Sasa Joaquin alikuwa akivuliwa chini ya sakafu, kama mfungwa kwenye msalaba.

Mlango wa mbele ulifunguliwa kidogo na Fransisco kuchungulia. "Nimewapata," alisema huku akiingia kwenye chumba na kuufunga mlango nyuma yake. Alichomoa visu vya aina ya Stanley kutoka kwa mfuko. "Niliviiba. Mungu anisamehe." kichwa chake kikaegemea kama kwamba kuomba msamaha.

"Natumai kwamba katika hali kama hii Mungu ataelewa," Luis alisema kwa kumshawishi.

Fran aliinua kichwa kwa furaha. "ninafurahi kwamba umetazama mambo haya hivyo, luis," alisema, "Kwani sikuona hatia kwa kuchukua. Nilijihisi bora kabisa!"

Wale wengine walicheka kidogo. Mahali hapo palikuwa pa utesi kiasi cha kutocheka.

Joaquin aliyekuwa amepewa vidonge vya kuzuia uchungu dakika kumi zilizopita, alikuwa amenyatwa pale chini. Wanaume wawili waliinama, na kupanua miguu yake. Wanawake wawili walisongea karibu na kichwa. Hao pia walipiga magoti huku wameshikilia Bibilia. Wangepokezana kwa zamu huku wakiimba nyimbo za kiispania, huku Luis akitekeleza tambiko.

Walipokuwa tayari kuanza, kipande kizito cha ngozi kiliwekwa kwenye mdomo wa Joaquin, ili aweze kukiuma. Ilikuwa ni muhimu wasiweze kutambuliwa na majirani, kutokana nahayo, Jouquin hakuwa na budi ya kunyamaza kimya licha ya uchungu.

Kitita cha viraka kiliwekwa kwenye mkono wake wa kushoto. Aliambiwa kushikilia mkono wake wa kulia bila kusongesha hadi mwisho wa tambiko hilo.

"Bwana ni mchungaji Wangu. Sitapungukiwa," Felicadad alianza kwa kiispania. Aliendelea kusoma huku Joaquin akiwaza juu ya maelezo hayo.

Kisu cha kwanza chenye makali kilikuwa kimesafishwa kwa kileo. Luis alimwagilia tone fulani la dawa, kunyakua mkono wa Joaquin, na kuukata kwa kutumia kile kisu cha makali. Mwili wa Joaquin ulitingisika huku akiuma ile ngozi.

"Ijapokuwa nitapita kwenye bonde la kivuli cha kifo, sitaogopa ubaya; kwani Yu nami," Felicidad aliendelea. Fimbo yako, hunikinga na kuniliwaza."

"Twapasa kutoa nafasi kwa ngozi kutoka kwa mkono." Luis alieleza, huku akichukua uzi na shindano kushona mshipa wa damu. "Tukimaliza tutahitaji ngozi kufunika kiduta, na kuunganisha kwa sehemu ya juu."

Kwasababu ya kukosa vifaa vya upasuaji. Alitumia tu kipuli aina ya pliers kushikilia ngozi ile. Mishipa ya ndani ilipaswa kuchomwa kwa waya iliyokuwa moto .uchungu zaidi.

Tone la dawa ile lilizuia kuvuja kwa damu, haikuwa rahisi sasa kutambua iwapo uzi au waya ile ilifanya kazi. Luis alikuwa na picha mbele yake iliyomuonyesha mahali pa kupata mshipa.

"Kufunga kwa bandeji kulipaswa kutunza sehemu za mishipa ya ndani," alisema.

Macho ya joaquin yalijawa na machozi, na sehemu za mkono ulioshikilia ngozi, nusra zionyeshe mfupa kwa kushika kupita kiasi. Sehemu zote za mwili zilisonga kiasi cha kuepusha kutingika kwa mwili.

"Majonzi yaweza kuwepo usiku, lakini furaha huja asubuhi." Maria alisoma, huku Felicidad akitafuta wimbo muafaka.

Luis alisukuma wembe ndani na kukata, mwili wa Joaquin ulijiinua kutoka kwa meza. Wale wanaume wawili walimshikilia kwa nguvu. Aliguna kwa uchungu huku kijasho kikimtiririka.

"Hapo! Tumekata mishipa ya kila aina," Yule mkufunzi alikuwa akiwaeleza wanafunzi wake.

Mahali pa kutatanisha pamekamilika sasa, Joaquin," alimuambia mgonjwa.

Luis hakusema mengi, huku akijifanya kuwa na kazi nyingi. Wale wanafunzi wake waliokuwa na mshangao walisonga karibu kujionea.

Ilikuwa ni dhamu ya Felicidad kusoma baada ya kukamilisha tambiko. "Heri yule aliyesamehewa dhambi zake, dhambi zake kufichwa. Heri mtu aliyepokea upako wa Bwana, na asiye na kikwazo rohoni mwake," alisoma.

Joaquin aliinua shingo lake na kumtazama Felicidad. Machozi yalimtoka, kulingana na maandiko yaliyo somwa, kama kwamba ni sawa na uchungu aliokuwa akihisi.

Kilichobaki ni minofu iliyoshikilia mifupa na mkono. Luis alisukuma ndani na Kile Kisu aina ya Stanley, kukata misuli iliyokuwa kubwa, na kuwacha mifupa.

Macho ya Joaquin yalijifunga na akazirai. Alikuwa amezimia.

Wakati tambiko lilikuwa limekamilishwa, na mwili wa Joaquin kufungwa, Luis aliwaarifu wanafunzi wake kwamba atafanya jambo moja, kabla yao kutekeleza kivyao. Walitarajiwa kuhudumia angalau mgonjwa mmoja kabla ya siku kuisha. Nakuwahudumia wengi hapo baadaye.

Aliwapatia maelezo kuhusu vile watakavyowatunza wagonjwa baada ya kupitia upasuaji huo.

Tukio hilo lile liliwaadhiri sana wale wanagenzi; hata kabla ya jereha kuanza kupona, wakati Joaquin alirudia hali yake, alitabasamu katika uchungu, alibadilika sana na kuongea juu ya amani aliyokuwa amepata.

Luis alimuonya kwamba angaliweza kupata matatizo. Maambukizi ya kipindupindu yalikuwa kawaida, na baadhi ya watu waliokatwa mikono walikufa kutokana na maradhi yaliyosababishwa sehemu ya jeraha kuoza.

"Hiyo sio shida," Joaquin alisema. Nina furaha kufa hivi sasa kwa kumpigania Mwenyezi Mungu vita. Moyo wangu ni huru. Ahsante Mungu! Wajua ndugu, nina furaha kufa kwa niaba ya Yesu sasa hivi. haki furaha."

Jaquin hakuwachwa nyuma miongoni mwa wale waliokuja kuondolewa Alama. Kote Ulimwenguni tofauti kwenye imani ilikuwa ikitukia. Watu ambao walikuwa hawajawai kuchukulia kazi ya Mungu kama ya dharura, walikuwa wakipokea amani, upendo, na motisha wakati huu wa kutazama amri ya Yesu. Ilikuwa mojawapo ya njia ya tambiko kwa wale walio teuliwa.ubatizo katika hali ngumu aliyopitia Yesu. Ilwakilisha tohara ya moyo, kwa kutoka katika uongo na kuingia kwenye Imani ya kweli ya Yesu na yote aliyofundishwa.

Lakini hata hivyo, kukatwa kwa mkono ili kuondoa Alama, ilikuwa ni mwanzo tu wa huzuni na mateso kwa watu hawa. Kukosa kuwa na mkono ilikuwa ni dhibitisho kwa ulimwengu mzima kwamba wamekata Alama. Mahali popote walikoenda, watu walisimama na kuwaangalia. sio tu kwamba walikuwa tofauti, lakini kwa sababu idadi ya watu wasio na mkono wa kulia ilikuwa inazidi kila siku. Lazima kuna jambo lililokuwa likiendelea na watu fulani walisimama kuwauliza.

"Ulipoteza mkono kupitia njia gani? nimeona watu wengi kama wewe. Hii inaashiria nini?"

Na kutokana na hilo, ujumbe ulikuwa ukienea kupitia njia ya mdomo, kwa yeyote ambaye hakupata kuutazama mtandao. Wale waliopata ujumbe huu waliupitisha kwa uaminifu kwa wengine kama walivyopata, kwa sababu hakuna yeyote aliyekosa kupata uguso kutokana na yale waliyosikia.

Palikuwepo haja ya kuwaficha wanamhanga hao kabla ya kupona majeraha kutokana na kukatwa mkono. Wakati huo walipewa mafundisho ya kutosha, na baadaye kuwekwa pamoja na wanamhanga wengine waliokuwa wamekatwa mikono. Wangalichukuliwa kwa kufunikwa macho, kwenye giza, hadi pale watakapoishi utumwani, wakiishi kama watu wasiotakiwa kwenye jamii. Walijua kwamba haitakuwa muda mrefu kabla hali yao ya ulemavu kutumiwa kuwatia mbaroni. Lakini walikuwa wamefanywa uamuzi, na kama Joaquin, walikuwa tayari kupoteza maisha, kutokana na imani yao mpya.

Kwa sababu Alama haikuwa ikionekana, wale 144,000 kati ya Makabila Kumi na Mbili hawakuwa na tofauti yeyote na watu wa kawaida mitaaani. Kutokana na hili waliweza kuishi ile miaka tatu na nusu bila kutambuliwa.

Lakini wanamhanga waliokatwa mikono walikuwa ni alama ya wazi kwa uma. Walijulikana na wale waumini wengine kama Msukumo wa Mahangaiko. kile ambacho hakingaliwasilishwa kupitia kwenye mtandao uliotayarishwa na Rayford na Chaim katika ujumbe wao (licha ya ukweli ulio kuwemo), ushuhuda wa kudumu kutoka kwa Msukumo wa Mahangaiko. Watu wale walioshiriki tambiko na kujivunia utajiri na mafanikio waliyopata. kama kwamba wokovu wao haukugharimu chochote. ulikuwa ni shuhuda ya kweli kulingana na mapenzi ya Mungu.

Msukumo wa Mahangaiko haukuwa na matumaini ya maficho katika ukiwa kama wale 144,000. Waliamini hivyo, kama walemavu wa kiroho, siku zao zilikuwa zimehesabiwa. Haitakuwa kitambo sana kabla ya Dangchao na jeshi lake kuwavamia kisha kuwahukumu, iwapo kuelewa kwa Rayford na Chaim kuhusu utabiri kulikuwa kwa kweli.

Lakini ufahamu wa haya uliwafanya kutia bidii katika kuhubiri kuhusu habari njema ya Yesu. Walitaka wengine kuepuka laana iliyokuwa ikining'inia duniani, na ushuhuda wao haukuweza kulinganishwa na Makabila Kumi na Mbili. Maelfu zaidi walikuja kila kila siku, kujiunga nao. Dunia ilikuwa ikipokea kutoka kwa hawa, muamuko kuhusu kupokea imani halisi katika kizazi kisichomti mungu.

***

Kwa wakati huo huo kulikuwa na mabadiliko yaliyokuwa yakiendelea kule Yerusalemi. Baba Mtakatifu Pius aliyekuwa ameapa kufanya kitu cha kishujaa "siku moja" alikuwa akisonga mbali na kutekeleza. Yeyote yule aliyedhani kwamba haikuwa na "Uwezekano" kuchukua hatua dhidi ya watu waliomuasi Yesu (Kwa sababu ingalitishia cheo chake, heshima yake,,shirika lake na amani yake) alikuwa ameaibika na kukasirishwa na shuhuda ya wanachama wa mkono mmoja katika Msukumo wa Mahangaiko, aliodhani kwamba hawakuyataka Makabila Kumi na Mbili.

Pius alikuwa tayari kusahau ukweli wa dhambi za Dangchao kwa kuzingatia ukinzani wa kundi hili, na shida na uchungu aliodhani wanapitishia ulimwengu. Mkataba wake na Dangchao kuyawinda Makabila Kumi na Mbili lilikuwa jambo lililowakera, hadi kumpelekea kuamini kwamba wito wake ulikuwa ni kikinga dunia dhidi ya mkiuko wa dini.

Kuishi na kufanya Kazi kwa pamoja na Dangchao kulikuwa na madhara kwa Pius kama vile watu wanaoishi karibu na eneo la kusafisha maji-taka huadhiriwa. Kinachowakera wageni wanapotembelea eneo kama hilo huonekana na wanaoishi pale kila baada ya siku. Dangchao alikuwa na upungufu wake, ilikuwa dhahiri; lakini alikuwa akijaribu kuleta amani ulimwenguni wakati mgumu. Hali ngumu katika afisi yake labda ndio iliyomfanya kutenda vile. Jambo muhimu ni kwamba, kama alivyojiambia Pius ni kuimarisha muungano wa Kanisa, na umoja wa serikali. Shida chache njiani ilikuwa ni jambo la kawaida. Ilikuwa ni mojawapo ya gharama atakayolipia katika wakati huo.

Pius aliwaza kuhusu kufanya marekebisho kwenye sanamu mbele ya basilika. Kipaaza sauti kiliwekwa, pamoja na bunduki chini ya sanamu hiyo. Umati wa watu ulijitokeza pale kila siku, na sanamu hiyo kubwa ingali "zungumza" kwa umati ule katika zamu, kwa kusema, "Tuiname na kumuabudu mfalme wenu pamoja na Mungu!" Sekunde tano baada ya usemi huo, zile bunduki zilizokuwa mita moja kutoka chini, zingalifyatuka.

Watu wengi walikufa au kujeruhiwa wakati wa kwanza bunduki zilifyatuka. Hatukuwepo na tahadhari kuhusu litakalo tokea, Dangchao alikuwa amefanya mzaha kuhusu vile watu wataanguka na kulala kifudifudi, hadi pale watakapo hakikisha kwamba bunduki zimewachwa kufyatuka, wakati mwingine sanamu ile "itaongea"

"Lazima kutakuwepo na uharibifu wa vitu fulani katika shughuli za kivita," alisema, wakati watu walilalamika kuhusu kujeruhiwa kwa watazamaji wa kawaida au hata kuuawa. wale waliosujudu kwa kujua walichotarajiwa kufanya. "Sio ya ajabu vile ujumbe unavyoenea kwa wale wengine wasio na 'hatia'," alicheka. "Sasa tumefanyia majaribio na kuonyesha mfano, nani atajificha nyuma ya ujinga?"

Waliomuasi bwana hawakuwa na la kujali katika kuua ili kutoa maelezo. Lakini alilotaka ni kuungamiza Makabila Kumi na Mbili kote ulimwenguni, waliokuwa wakipata umaarufu kila kukicha. Ujumbe kuhusu kukatwa kwa mikono ulikuwa umemfikia, na kuamurisha kwamba vifaa vikubwa vyenye makali vijengwe kwenye miji yote kote duniani. Iwapo umati mzima ungalichinjwa, basi watu wengi wangaliogopa, alidhani hivyo. Ingaliwatisha wafuasi wenzake ambao walikuwa na nia ya kujiunga na imani hiyo.

Zion Ben-Jonah Aandika

Imani yenye nguvu huwaadhiri wale wote wanaokumbana nayo. Baadhi watajaribu kuiga waliyoona; lakini baadhi hukasirika tu kwa kuona imani kama hiyo. Hawawezi kudumu kwa ukweli kuhusu umaskini katika roho, hivyo basi kuwashambulia walio wahaibisha. Hao huwaita warithi, wendazimu, na wanatabaka lisiloeleweka. Na hujaribu kuwanyamazisha, au kuwaangamiza.

Kitabu cha Ufunuo wa Yohana kinaongea kuhusu umati mkubwa usioweza kuhesabiwa (kwa pamoja na wateule 144,000 walioteuliwa na Mungu kabla ya Mahangaiko au Huzuni Mkuu kutokea). Inaeleza kwamba watu hawa watavaa kanzu nyeupe wakisimama mbele ya Mungu, kanzu zilizosafishwa kwa "damu ya Mwanakondoo" (Ufunuo wa Yohana 7;9, 14-17)

"Damu ya Mwanakondoo" inamaanisha damu ya Yesu iliyo mwagika msalabani kwa ajili yetu. Lakini pia Yesu alitoa wito kwetu sisi kuubeba msalaba wetu na kufuata nyayo zake. Ufunuo wa Yohana unatueleza kwamba wakati wa Huzuni mkuu na mahangaiko, wafuasi wa Bwana watawaungusha waasi wake kwa "Damu ya Mwanakondoo, na kwa wito yakwamba hawakupenda maisha yao, hata usoni mwa mauti." (Ufunuo wa Yohana 12:11)

Haya yote ni kuonyesha kwamba umati mkubwa "unaojitokeza wakati wa Mahangaiko na Huzuni mkuu" watakuwa wahanga, wakimfuata Mwanakondoo hadi kifo chao. Ufunuo wa Yohana unatuarifu kwamba "Watakatwa vichwa" (Ufunuo wa Yohana 20:4)