Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

20. Maafa

Reinhard alitembea kwa kukwawa kwenye barafu. Moscow nzima ilikuwa katika hali ya kusikitisha. Hakuna jumba lolote lililobaki

Kwanza tulikuwepo na mawe kutoka kwa nyota yaliyokuwa yametapaka kote Uropa, Afrika ya kaskazini, mashariki ya kati, na sehemu za Asia. Alama ilibakia mahali yalipoanguka, na kuanzisha moto kwenye misitu katika sehemu nyingi za dunia. Wingu la ukiwa lilikuwa limeutanda ulimwengu, huku likifunika mwangaza wa jua. Hewa ya moto kutoka kwa miali ya moto ilijaa kote na kuyeyusha unyevu wote uliojikusanya na kugeuka mawimbi yaliyonyesa mvua ya barafu, mawe hayo ya barafu yalikuwa hadi uzani wa kilo moja kwa kila kigae. Maelfu ya watu yalikufa kwa kunyeshewa na mawe hayo ya barafu. Miji yote iliwachwa bila paa. Mamilioni ya magari yaliharibiwa kiasi chakutoweza kurekebishwa. Mizoga ya wanyama ilitapakaa kila mahali.

Basi ikafuata na ile nyota kubwa asteroid. Ikaunguka upande wa katikati mwa Atlantiki, na kufanya maji kujaa na kuruka hadi mamia ya mita kutoka baharini, na kuosha miji yote iliyokuwa kwenye ukingo au pwani. Mamilioni yalipotezwa kwenye pwani ya Mashariki mwa Amerika ya Kusini na Kati, na pwani ya Magharibi mwa Afrika na Uropa.

Idadi ya nyota zilizoanguka katika awamu ya pili zilisababisha maafa mengi kuliko ilivyokuwa awamu ya kwanza, hata ingawa zilikuwa tu mojawapo ya nyota zilizokuwa zikiruka mfano wa garika. Huko Urusi waliita maafa hayo "Chernobyl" kutokana na miali yake. Miali hiyo iliadhiri theluthi moja ya mikondo yote ya maji kote ulimwenguni, aafa haya yalizidi na kuwapelekea watu kunywa yale maji yaliyo na sumu, huku wakifahamu adhari ya kupata saratani, matatizo ya kizazi, na vifo vya mapema. Ilikuwa ni kuyanywa maji hayo au kufa kwa kiu.

Rayford na Chaim walikuwa awali wamesha tabiri, na Dangchao pamoja na baba Mtakatifu Pius walifanya yote waliyoweza kupambana walipofahamu kwamba nyota zina kuja. Wataalamu walisema kwamba msukumo wa nyota ile kubwa hautagonga dunia. Walisema uwezekano wa kugongana na dunia ulikuwa mara moja kwa milioni, hata baada ya zile nyota ndogo kuanza kuanguka, walianza kusema kulikuwa na nafasi ya moja kwa kumi ya uwezekano wa ile nyota kubwa kulenga dunia. Kwa wakati garika hiyo ya ajabu ilikuwa inasababisha maafa, watu walichelewa kunusuru miji. Na sasa dunia ya Dangchao ilikuwa imekumbwa na maafa kupita kiasi.

Ilikuwa ni sababu ya kuchikia Msukumo wa mahangaiko. (aliodhania Dangchao kuwa baadhi ya wanachama wa tabaka 144,000) kwamba hii ilitukia mwanzoni.

Ilianzia na tangazo kutoka kwa Rayford na Chaim kwamba ukame utatokea Israeli, hadi pale Dangchao atakoma kuwadhulumu wafuasi wa Mungu. Mvua ilipotea kwa miaka mitatu. lakini haikukomesha dhuluma dhidi ya wafuasi wa Mungu.

Basi wale Mitume wawili wakatangaza kwamba maji katika maeneo yaliyowaua wateule wa Bwana yatalaaniwa. Maangamizi ya wateule yalianzia kule Amman, Yorodani, huku zaidi ya wateule mia moja wakiuawa siku ya kwanza. Hata hivyo, kima wawili walipatikana wamekufa ndani ya bohari la maji ya kusambazwa mjini, wakijaribu kukimbia. Lakini uchunguzi ulibaini kwamba walikufa kutokana na maradhi ya ebola, na kisha janga la ugonjwa huo likazuka kule Yorodani, na watu hawakuruhusiwa kuingia au kutoka kule. La kustaajabisha ni kwamba mauaji yalikoma, hatukupata kushuhudia ukatili huo kwa miaka mitatu ya mwisho Lakini hata hivyo hapakuwa mahali salama pa kujikinga kwani virusi vile vilisababisha vifo sawa na eneo lililo shuhudia mauaji.

Lakini Dangchao alikuwa na mvukuto kutokana na kukasiriishwa na wale wafuasi wa Mungu hata baada ya tukio la Amman. Mauaji ya halaiki yalianza kote duniani baada ya siku chache. Katika kipindi cha mwezi mmoja, zaidi ya wafuasi milioni moja waliokuwa na mkono mmoja walikuwa wamekatwa vichwa.

Na hapo ndipo wale Mitume wawili walionya kwamba nyota kuu itaangukia dunia. Dangchao na Pius walikataa kutazama mtandao wa makabila Kumi na mbili, kama kwamba waliogopa itaadhiri fikira zao, walipata tu ujumbe kupitia kwa washahuri wao. Waliposikia kuhusu nyota ile, walitawanya wataalam wa kusoma nyota kote duniani. Wataalam hao waliambiwa kuweka habari hizo kwa siri na wasizitoe kwa vyombo vya habari au raia. Wanahabari walipata ripoti ya nyota kubwa kuanguka siku tano kabla ya tukio. Hata hivyo, haikuwa mapema kwa uma kufanya lolote kuhusu hali hiyo.

Hapa tulikuwa na Reinhard akipata shida kutembea katika barafu kule Moscow, akijaribu kutafuta mahali salama, nyumba nyingi zilikuwa zimeharibiwa na garika kuu. Lilikuwa ni jukumu lake kuona vile kazi ya marekebisho itatekelezwa. Sheila Armitage alikuwa mzee sana kutekeleza jukumu kama hilo, hivyo basi majukumu kama hayo yaliwachiwa Reinhard.

Mwanzoni alikuwa ni Rayford aliyefundisha, na kisha baadaye kulichukua jukumu la kuwaongoza Jesans. Reinhard alifanya kila juhudi kukubali, lakini halikuwa jambo bora kuenda mitaani kuuza majarida huku Rayford akifundisha kama kwamba yote aliyosema yalikuwa yakitoka kwenye akili yake. Hatimaye akawa ni Sheila. Watu walihiari tu kumuendea Sheila kwa mawaidha kuliko yeye, kwa sababu alikuwa na umri mara mbili kumliko. Na karibuni akawa Jerry, mmoja wa wahitimu wa kwanza wa kabila la Asher, aliyekuwa akipewa heshima sana kuliko Reinhard.

Kwa hakika alipowasili Jerry, mwanaume wa mapambo yaliyopendeza, mwenye umri wa miaka sitini, nywele nyeupe na kidevu, aliingia tu na watu wakaanza kufanya kazi kwa bidii ili kurekebisha jengo lile. Huku majirani waking'oa paa ili kuuzeka kwa chuma au vifaa vilivyonunuliwa katika maduka ya serikali, wafanyikazi wa Jerry waliingia mitaani kuokota kutoka kwa vifusi vilivyokuwa vya majengo, ili kuvitumia kurekebisha nyumba yao. Vifaa vilikuwa vikiingia, na utakuwa ni muda mchache kabla ya kukomesha barafu kuingia kwenye makaaazi yao.

"Karibu! Karibu!" Jerry alisema kwa ukarimu, wakati alipomfungulia Reinhard alipobisha mlango. "Ivan mletee ndugu yetu kikombe cha kahawa," aliyekuwa wakati mmoja Muamerika alisema kwa lugha fasaha ya Kirusi.

"Sitaki kahawa," Rainhard alijibu kwa haraka.

"Nimekuja hapa kufanya kazi."

"Bila shaka," Jerry alisema kwa ukarimu. Kisha kutazama uso wa Reinhard: "lolote limekukera?"

"La, hakuna lolote linalo nisumbua" Rainherd alimjibu. "kuna jambo linalokusumbua wewe?"

Kwa hakika ndio, natumai lipo," Jerry alisema. "Je twaweza kuingia katika chumba cha nyuma tukajadili?"

"kwani nini mbaya tukijadiliana hapa?" Reinhard aliuliza kwa lahaja huku akizama kwenye kiti kile, na kuweka mikono yake kwenye sehemu za kuegemeza mikono.

"Sitaki nikuhaibishe," Jerry alijibu, kwa upole. "Nafikiri haujafurahia jambo fulani, nilitaka kujadili nawe faragani. mimi nawe tu."

Reinhard aliamuka na kuelekea katika chumba kilichokuwa nyuma. Sikutaka nikuhaibishe alifikiri. Kwa kuwaza juu ya maongezi ya upole ya Jerry Anthony. Alifikiri tu hana dosari na wenzake wangalifuata amri yake.

"Je inakukera kwamba mimi ni kiongozi hapa?" Jerry aliuliza. Alikuwa ameona hayo yapasa wiki kadha zilizopita, na ulikuwa wakati wa kutatua.

"Labda," Reinhard alisema, kwa kutingisa mabega, macho na mdomo, kuonyesha hali isiyo ya kujali.

"Tafadhali, naweza kujadili kitu fulani nawe? Jerry aliuliza.

"Ni juu yako," Reinhard alijibu, kwa kujifanya kama kwamba hana haja, huku akiinama kwenye meza katika chumba hicho, na kuangalia kwenye sakafu.

"Kabla ya vita.kule Amerika.Nilikuwa na kazi niliyo dhani ni bora. Nilijiona kama kiongozi bora. lakini ilichukua vile vita na mauti ya halaiki kuona kwamba fikira zangu zilikuwa potovu. Cheo fulani hakimfanyi mtu kuwa kiongozi.

"Nilifika hapa Moscow kama mtu aliyepotea. Lakini nilipokutana nawe, Reinhard," (Jerry alikimia kwa sababu fulani). "Nilipo kutana nawe, nilijua kwamba nimekutana na kiongozi wa kweli. Haukutambuliwa kulingana na malimwengu, bila mshahara, bila cheo, lakini ulijua ulipokuwa unaelekea. Ulijua jinsi ya kutambua vitu vidogo na mambo makubwa, ulinipa changamoto kujaribu.kuwa kiongozi wa kweli.

Reinhard alijipata katika mashaka. Alitaraji shutuma kutoka kwa huyo mtu aliyemzidi umri. lakini badala yake alitiwa maneno ya kubembelezwa. Ilifanya zaidi ya shutuma. Ilikuwa ni kitambo sana tangu Reinhard kupata sifa kama hizo, na alifahamu kwamba yale Jerry alikuwa akisema yalikuwa ni ya kweli kuhusu kiongozi bora. Kuwa kiongozi bora sio kupokea sifa kila mara. Ilimaanisha ule uwezo wa kuweza kuona mbele kuliko wenzio.

Yale aliyosema Jerry yalitosha kumletea matumaini yule ambaye alikuwa amepoteza. Reinhard alikuwa ameona baadhi ya viongozi katika Makabila Kumi na Mbili wakipoteza matumaini, na maono ya milele, na mbingu na hata kurudi kwa Yesu, na wote walikuwa wamerudi nyuma. Baadhi yao walikuwa viongozi bora kabla ya kurudi nyuma. Hakutaka kujiona kama mmoja wao kwa kurudi nyuma. Alisimama na kumkumbatia yule mzee.

"Danke", alisema kwani Jerry alifahamu Kijerumani.

"Danke, Jerry! tafadhali nisamehe kwa tabia yangu mbovu."

Reinhard hakuwa na nafasi tangu kuingia Moscow, zaidi ya miaka minne iliyopita, lakini haikuwa kisingizio cha kushahuriana na mtu huyu mwenye busara, na jukumu kwa muungano kwa zaidi ya miaka mitatu, na aliyeongea ukweli uliomtoa Reinhard katika upembe wa kupotea.

"Nieleze zaidi kukuhusu," Reinhard alisema, katika juhudi za kuficha dhambi zake. "ulikuja aje huku Moscow?"

"Hatukuwa na chaguo," Jerry alieleza. Nilijificha kule Amerika kwa wiki kadha; lakini wakati elkopta ilikuja kuwanusuru wahanga, ilikuwa ni ile ya Urusi. Tuliletwa hapa na tumeishi hapa tangu hapo."

"Na je familia yako?" Reinhard aliuliza.

"Nilikuwa na watoto wawili, msichana na mvulana, wote wakiishi New York. Walikuwa karibu na eneo la mlipuko. Wangalikufa papo hapo."

"Na bibi yako?"

"Bibi yangu?" Jerry aliuliza. " Mi.Yeye." Alisita. "Sijawai ongea juu yake."

"Labda huu ndio wakati bora kuanza," Reinhard alisema kwa ukarimu.

Jerry alisita kwa mara nyingine. Ilikuwa dhairi kwamba alitaka kuongea, lakini kulikuwa na kitu kilichokuwa kikimzuia. "Nitahitaji kuongea juu ya hilo," alisema. "Na uliweke hilo kati yangu nawe?" aliuliza. "Ni muhimu sana."

"Bila shaka," Reinhard alikubali.

"Mke wangu aliuawa, sio kutokana na mlipuko. Aliuawa na muaji wa kujitolea, mbele ya macho yangu." Sauti ya Jerry ilianza kukatika, lakini alitaka kumaliza masimulizi yake. Bila shaka lilikuwa ni jambo ambalo alijiwekea kwa muda. "Alinuia kuniua miye pia!" alilia. "Hank.Hank Greenhorn. mmoja kati ya walinzi wangu, alijirusha mbele yangu. Hakuwa na nafasi."

Jerry aliketi chini ya sakafu na kuweka uso kwenye mikono yake, akidondokwa na machozi huku akisimulia.

Reinhard alisikiza kwa makini. Walinzi? Muaji wa kisiri? alikuwa akiongea juu ya nini?

"Mlipuko ulinifanya kiziwi kwa muda. Nilihangaika sana kiasi cha kushindwa kuongea. Hakuna yeyote aliyetoka mle ndani akiwa hai. Wakati Warusi walipowasili, Nilijua singalitumia jina langu la kweli. Nilitumia jina langu la kati. Gerald Anthony. Ndevu zangu zilikuwa zimeanza kumea na nikawacha. kwa pamoja na nywele zangu ndefu.

Rainhard alijiunga naye kwenye sakafu na kumkumbatia. Kwa yale aliyokuwa akiongea, alionekana kama aliye sumbuliwa.

"Mungu angalinisamehe kwa njia ipi?" alilia, huku akipanguza mapua kwa kitambaa.

"Ningalikuwaje mtu asiye na huruma? Niliwacha tamaa zangu za kisiasa kuwa muhimu kuliko maisha ya watu wale. Nilichelewa kugundua kosa langu. Singali nusuru Amerika; lakini nashukuru Mungu, sikubwenyeza chochote kuwaangamiza."

Reinhard alikuwa akijaribu kumuelewa Jerry. Ni vipi Jerry Anthony au Jerry fulani alisababisha kuanguka kwa Amerika? Alisukuma nywele za huyu mzee kutoka usoni mwake, kisha kumtazama. Nywele zake zote zilikuwa za kijivu, labda kutokana na yale aliyopitia, lakini kutoka kwa kidevu Reinhard alidhani angalimtambua.

"Fitzhugh?" aliuliza.

Jerry alitikisa kichwa.

Reinhard hakuamini. Alikuwa ameketi kwenye sakafu akimbusu aliyekuwa Raisi wa Amerika. Mtu huyu alikuwa amezeeka, mwenye nywele ndefu na kidevu, lakini alikuwa Rais.

Muaji wa kujitolea (labda mmoja kati ya askari wake) lazima aliingia kwenye Ikulu ya White House, pamoja naye na mkewe.

Yule Rais wa Amerika alimueleza Reinhard kwamba alikuwa ni Reinhard aliyemfundisha maana ya kuwa kiongozi. Na alikuwa amesema baada ya kufanya kazi chini ya Reinhard kwa zaidi ya miaka tatu. Sifa gani hizo za kufurahisha! Na alikuwa mjinga kiasi gani kutotambua kwamba hakuwa anatambuliwa na kuheshimiwa!

Hakika, wito na kumuita Mwenyezi Mungu lilikuwa jambo muimu kuliko kuwa Rais wa taifa lenye uwezo mkubwa. Rais Gerald Fitzhug alikiri hayo. Waliyokuwa wakifanya yalikuwa muhimu hata ingawa Reinhard hakuwa akitambulikana katika ufalme wake huo. Reinhard aliomba kupata nguvu ili kupata nguvu na kubaki mwenye imani, na kumshukuru Mungu kumuwezesha kutekeleza jukumu kama lile.

***

Kinyume, Dangchao na Pius walikuwa wamehangaika, kwa kupoteza mwelekeo katika juhudi zao za kuongoza ulimwengu. Pius alikuwa ni ibilisi tu kama Dangchao wakati huu. Huku akiwa amejifunza kutekeleza miujiza ya kishetani kutoka kwa Dangchao. Pius kwa aibu alikuwa akitembea karibu na ile sanamu iliyokuwa katika eneo la hekalu, huku akisujudu na kumuinamia Dangchao na kumuita majina ya heshima na hadhi, huu ulikuwa ni ushahidi kamili jinsi alivyokuwa akimuabudu binadamu/mnyama.

Sanamu ile ilikuwa imenusurika kutokana na garika, lakini hekalu zote zilikuwa zimeharibiwa kutokana na garika. Nyota iliyoanguka iliharibu makao ya Pius punde tu nyota zilianza kuanguka. kwa bahati hakuwemo ndani wakati huo.

"Lazima tuwakomeshe," Dangchao alisema alipokuwa akila maankuli ya mchana. "Lazima tuyatafute makao yao makuu. tuwaue wale Mashahidi Wawili, jinsi wanavyojiita. Tusipofanya hivi wataendelea kunawiri. Mateso yatawafaa. Lazima kuna mtu anayejua. Watatuarifu yalipo makao hayo."

"Lakini, Mwadhani," Pius alijibu, "Maumivu huchukua muda. Itadidimiza mauaji. Kila mmoja anahitajika kusaidia kujenga upya. Itahitaji mengi sana kuanza kutekeleza. Kuna mahojiano na wasemaji, wadadisi, maafisa wa kuweka kumbukumbu, maafisa wa kuwakamata, wauaji. Na hata vyumba vya kuhifadhi maiti vimejaa kutokana na maafa ya hivi punde."

"Laani maafa! Wacha walale walipo! Iwapo hatutawakomesha Wakristo hawa, kila kitu kitapotea. Vuka utepe mwekundu. Iwapo wapelelezi watashuku au kufikiri mtu ni mfuasi, nataka mtu huyo auawe. Sijali kama atakuwa na Alama au la. Lazima kuna watu humu ndani wanao wasaidia. lazima tuwatafute na kuonyesha mfano."

Dangchao aliendelea: "Watu watajenga upya baadaye. Nguvu zote zielekee kuwakomesha Wakristo. Tusipo fanya hivyo hatutakuwa na ulimwengu wa kujenga."

Na sasa, ulimwengu ulitazama kwa mshangao na kukosa kuamini kwamba, kiongozi wao mkuu-- mtu waliyemdhania yapata mwaka mmoja na nusu kama kiongozi maarufu ambaye hajawai patikana ulimwenguni--hakujali maslahi yao wala maumivu yao kwa ajili ya tamaa zake za kuwadhulumu Wakristo.

Dangchao alikuwa ameshawishika kwamba Wakristo ndio waliokuwa wakiangamiza ulimwengu, alitumia makarani wake na mojawapo ya waandishi mashuhuri kuhakikisha kwamba ujumbe huo unafikia wengi. Alifaulu kueneza ujumbe huo wa uongo dhidi ya Wakristo na kutoa taswira ya kwamba hao ndio waliokuwa wameapa kuangamiza dunia. Haya yaliwapelekea hata majirani kuanza kupigana na kuuana hata kwa visingizio visivyokuwa vya kweli. Maafa na mauaji yaliendelea, lakini watu wanane kati ya kumi waliokufa walikuwa ni wale wenye alama iliyo jikita katika mikono yao ya kulia!

Matokeo ya hasira za Dangchao, yalifanya hata idadi kubwa ya wafuasi wake kuungama na kumwacha. Walidhani kwamba, hata ikiwa ni mauti, heri wafe kwa njia ya haki na upande wa kweli.

Wale Mashahidi Wawili hawakuchoka kuwahimiza katika hekima yao "Iwapo tutakufa hatimaye," walisema, "Basi ni heri kufa kwa kutetea Mungu au kwa kumtetea shetani? Huu ndio ukweli na ujumbe ambao umekuwa ushuhuda wa injili karne nyingi zilizopita, iwapo dunia imetusonga au la."

Zion Ben-Jonah Aandika

Maafa yanayofuatia baada ya milio ya kwanza minne ya "tarumbeta" ya Huzuni Mkuu (Ufunuo wa Yohana 8:6-12) yameelezwa katika sura hii. Ni ajabu kwamba neno "Chernobyl" ni jina la Kirusi la mmea wa sumu ujulikanao kwa kimombo kama "wormwood" Maelezo yaliyo kwenye kifungu cha Ufunuo wa Yohana 8, yanatuarifu kwamba nyota itakayolenga dunia itajulikana kwa jina hilo.

Sura hii pia inatoa maelezo kuhusu uwezo watakao kuwa nao wale Mashahidi Wawili. Somas Ufunuo wa Yohana 11:6.

Funzo kuu hapo ni lile la uongozi. Udhalimu wa utawala wa Kilimwengu ni kuhusu heshima, utajiri, mamlaka na kutambulikana. Lakini hali ya unyenyekevu na kujitoa na hatimaye kufa kwa "Mwanakondoo" ndiyo inayosimulia juu ya ufalme wa mbinguni.

Ni aibu gani kwa Constantine kukosa nafasi ya kujifunza kama vile Fitzhugh anavyoelewa katika sura hii, nini maana yakuwa kiongozi wa kweli katika ufalme wa mbinguni! ni hadi pale watu watakapo fahamu ndiposa viongozi wa mataifa yenye uwezo wataelewa na kuwa wahudumu bora wasiotumia mamlaka yao kuwaangamiza au kuwadhulumu wenzao, na "kutumia nguvu zao" kuleta faida kwa Mungu na watu wake.

Pius anawakilisha hatima ya wale ambao watatumia mamlaka yao kwa njia zisizofaa na kumuasi Mungu kwa kuwacha yale tunayopaswa kutenda ili kuona ufalme wake.