Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

21. Apollyon

Vita kati ya Dangchao na Wakristo vilipamba moto, na vikaendelea huku miaka tatu na nusu ya Huzuni ikikaribia kukamilika.

Katika kipindi cha miaka miwili tangu Dangchao kusitisha kutoa kwa kafara, na kuingia kwenye Hekalu kule Yerusalemi, pande zote zilihesabu mamilioni waliokata Alama, na mamilioni zaidi waliochinjwa kumfurahisha Dangchao.

Ingawa Pius alikuwa mwenye akili timamu kuliko huyo muasi wa Yesu, alikuwa anaendelea kuadhiriwa. Ilikuwa ni tamaa, iliyowavutia, lakini ilikuwa ni tamaa iliyotawaliwa na maovu na kufanya uongozi wao kuwa wa kikatili.

Hata ingawa Dangchao na Pius walikuwa wakiua watu wengi kuliko vile Rayford na Chaim walikuwa wakipokea watu walio zaliwa upya., hakika Wakristo walikuwa wakishinda vita vya kiroho. Idadi ya watu waliokuwa wakiomba kuwa wanachama wa msukumo wa huzuni ilikuwa ikiongezeka kila siku licha ya mauaji.

Kuanguka kwa nyota kuliwacha maafa na mamilioni ya watu walioaga dunia. Sio shirika la umoja wa Mataifa au Serikali za umoja huo zilikuwa na uwezo wa kukabili maafa yaliyokuwa yakitokea. Dunia ilionekana kurudi katika nyakati za giza. Watu kila mahali walikuwa wameteseka. Dangchao bila shaka alikuwa akipoteza umaarufu.

Lakini kuchoka na serikali za kilimwengu haikuwa sababu ya watu wengi kujiunga na Ukristo. Watu waliojiunga na ule Msukumo walikuwa wakifuata shuhuda za wale waliotangulia. ushuhuda uliodhihirika hata walipokuwa wakiuawa. Hakika kulikuwa na kitu bora baada ya maisha haya, na hawa wafuasi wa Yesu walikuwa wametambua!

Mbali na wale mashahidi wawili kuwindwa na Dangchao pamoja na Pius, walikuwa wamehutubia waandishi wa habari mara kadha kule Sydney na mkutano mmoja kule London.

Matokeo ya mikutano na wanahabari yalidhihirisha kwamba, Dangchao hakuwa na uwezo juu yao. Wanajeshi waliokuwa na silaha walitumwa kuwashika au kuua Rayford na Chaim; lakini kila mara, kundi hilo la wanajeshi ndilo lililoangamia, wale Mashahidi wawili waliongea tu neno moja na kundi la wanajeshi kuanguka, na matumbo yao kuliwa na funza.

Wakati Rayford na Chaim walikuwa wakiufunga mkutano na waandishi wa habari, waliongea mara moja na waliohudhuria mkutano ule walikuwa vipofu kwa muda. Katika heka heka hizo wale mashahidi wawili waliondoka kutoka eneo lile bila kuonekana.

Mikutano na waandishi wa habari ilifaulu sana hasa kwa shughuli za Kikristo.

Wale mashahidi wawili waliongoza vita hivyo kwa ufasaha na kujibu maswali na maojiano kwa njia iliyowavutia na kufurahisha ulimwengu mzima. Chochote walichosema kutoka upande mmoja yalikuwa haki ule upande mwingine. Walitumia lugha nyepesi kuwaeleza watu kwamba nia ya Mwenyezi Mungu ni kutaka watu kuishi vizuri huku wakimtambua kama Muumba wao. Walieleza kwamba Dangchao, Pius na wengine wale waliwekwa duniani kama vibaraka kujaribu imani ya watu. Walimaliza kwa kutoa wito kwa watu kuwacha mienendo mibaya, kukoma kuwafuata waasi wa Bwana na kutozingatia Alama ili waweze kupata uponyaji wa milele kwa kumti Mungu na Yesu mwanawe kabla ya kila mmoja kupata laana. Hawakuweza kufafanua aina ya laana itakayowakumba.

"Utatamani kufa ili uepuke," Rayford aliwahakikishia. "Sitataka kumuombea yeyote apate hayo. Lakini itatendeka. Mniamini. Mko na muda mchache kuungama. Tafadhali, kwa faida yenu, mbadilike hivi sasa. Kuukata mkono wako hakuwezi kulinganishwa na yale yanayotarajia kutokea iwapo hautaungama sasa hivi."

Mkutano huo wa waandishi wa habari uliletwa moja kwa moja kutoka eneo hilo na kusikika dunia nzima, na ukapelekea watu wengi kujiunga na Msukumo uliokuwa umewakumba Wakristo. Watu walikuwa wengi kwa yale makabila Kumi na Mbili kuweza kuhudumia kivyao; hivyo basi watu ambao tayari walikuwa wamejikata mikono waliitwa kusaidia.

Haikuchukua muda mrefu kwa Ulimwengu mzima kutambua na kuunga mkono Ukristo.

Dangchao aliyekuwa ameumia sana tangu kuanza kwa mikutano na waandishi wa habari, alikuwa tayari amerukwa na kichwa.

"Sisi ni vibaraka?" alipaza sauti, wiki kadhaa baada ya kuripotiwa kwamba Rayford na Chaim walimuita hivyo. Alitupa gazeti baada ya kusoma sehemu hiyo.

"Vibaraka? Wamedhubutu!" Alipunga mikono yake kwenye hewa huku akitingisa kichwa kwa masikitiko huku akiongea kwa sauti ya juu. Wanahabari walikuwa wamechukua neno hilo moja na kulitumia katika habari zote zilizohusu Makabila Kumi na Mbili.

Dangchao alishikwa na kichaa ndani ya chumba chake, huku akipiga fanicha na kujigonga huku na huku na kurusha vitu. Alitupa chungu kikubwa cha maua kwenye kio. Pius alikuwa kadhalika na uso wenye wasiwasi. Alikuwa ameanza kuzoea hali ya Dangchao.

"Nitawaonyesha vibaraka ni akina nani, na ni nani anayesukuma nyuzi za kuongoza vibaraka! Nitawaonyesha!" Dangchao alisema.

"Apollyon! Amka hapa! Apolioni!"

"Naam, bwana!" Na mara moja upande wa mkono wa kulia wa Dangchao kulisimama kiumbe cha ajabu na cha kutisha na chenye nguvu za kishetani. Uso wake ulikuwa wa kutisha kuliko kitu chochote ambacho Pius alipata kuona. mbali na ile sura nyingine ya Dangchao. Pius kwa uoga alijificha kando akidhani kwamba kiumbe hicho hakimuoni.

“Apolioni, leta jeshi lako!"

"Yaani niwalete hapa juu?" Apollyon aliuliza kwa mshangao.

"Ndio walete hapa juu!" Dangchao alisema kwa sauti. Na uso wake ukabadilika katika sura iliyomtisha Pius. "Nataka ulimwengu kufahamu nguvu nilizo nazo. Nataka waonje ninachoweza kufanya. Ninataka kuwafundisha adabu wale Wakristo."

"Lakini wataumiza watu wetu. bwana," Apolioni alisema. "Twahitaji kufanya hivyo leo? Kabla ya wakati?"

"Najua ninachofanya!" Dangchao alisema. Iwapo siwezi kuwapeleka jehanamu, basi nitawaletea jehanamu!" Alifurahishwa na jinsi alivyotamka usemi huu, na kuangua kicheko chake cha kishetani. "Wanachukua wafuasi wangu. Nina fursa ya kuwahangaisha hivi sasa.kabla wakufe!" Na kicheko kikarudia tena.

Pius hakuwa na hekima kuhusu kuangamiza watu wao, lakini iwapo matendo ya Dangchao yangalisababisha mahangaiko kwa wakimbizi.(Jina la pius kwa wale mashahidi wawili; hakutumia neno Wakristo, kwa sababu lilimkumbusha dhehebu lake la hapo awali.) Iwapo mipango ya Dangchao ingaliweza kusababisha mahangaiko kwa Makabila Kumi na Mbili, basi ilikuwa bora "kufanya maafa makuu" kama alivyosema Dangchao.

"Sasa, Apollyon! Fanya hivyo sasa!" Dangchao aliwika, na sura yake ya kishetani kuwaka akitazamia kuona yatakayo tendeka.

Sakafu ya chumba kile ilipasuka katikati na kurarua kile kitambaa kilichokuwa kimetandikwa pale huku sakafu iliyokuwa imepambwa ikiharibiwa. Moshi ulitoka humo ndani.mwingi, moshi wa rangi nyeusi, na kujaza kile chumba, kujaza ikulu, na kuingia mitaani, na kujaa kote Yerusalemi. Watu walishindwa kupumua.

Kisha baadaye ndani ya ule moshi, kulisikika sauti kama ya kikosi kilichokuwa na silaha na makelele. Mwanzoni haikusikika kisha kuendelea. Watu waliokuwa na eneo lisilo na moshi mwingi ndio waliotazama mahali kulikotokea sauti, na kisha kugeuka na kukimbia.

Lilikuwa ni wingu la nzige. au viumbe waliokuwa kama nzige. Lakini walikuwa na sura ya ajabu. Miili yao iliyokuwa na silaha na mabawa yao ya chuma yalitoa sauti kama ya askari walio na farasi. Kwenye mkia kulikuwepo chenete iliyo kuwa kama ya kisusuli.

Nzige hawa hawakuvamia miti, nyasi au mimea. Badala yake watu ndio walioshambuliwa. Viumbe hao walikuwa na meno yaliyouma kabla ya kuwachilia chenete zilizokuwa na sumu. Uchungu huo haukuwa wa kuvumilia. uchungu kushinda ule wa kujifungua. Ile sumu iliwafanya waadhiriwa kupooza na kuguna kwa uchungu na kujikokota chini kwa saa mbili au tatu kabla ya uchungu kupoa. Dawa za kupoesha uchungu hazikuweza kufanya kazi, aidha hatukuwa na dawa.

Watu wengi walishambuliwa mara kadha licha ya kujaribu kuepa janga hilo.

Viumbe hao walizidi kutoka kwenye ule moshi mweusi siku ile. Walitoka Yerusalemi na kuelekea sehemu zote za dunia. Viumbe hao walitarajiwa kuadhiri ulimwengu kwa miezi mitano huku wakishambulia yeyote waliyempata mbele yao.

Isipokuwa tu wafuasi wa Makabila Kumi na Mbili. Labda kile chembechembe kilichopachikwa ndicho kilicho wavutia viumbe hao. Au ilikuwa ni upako wakuepusha wale 144,000. Kwa viwango vyote, haikuchukua muda kabla ya Rayford na Chaim pamoja na vyombo vya habari waliona jinsi Dangchao alivyojikejeli.

Rayford na Chaim walitabiri hali ya ukiwa kote duniani.maumivu ambayo yangaliwafanya watu kutamani kufa. Walikuwa wameeleza kuhusu laana, lakini Dangchao mwenyewe ndiye aliyekuwa "kibaraka" na ilidhihirika wazi wazi. Viumbe wake wa mabawa ya chuma, meno makali na chenete za sumu, yalikuwa ni kinjo jinsi jehanamu ilivyo. Mwenyezi Mungu aliwaepusha waja wake kutoka kwa shambulizi la Dangchao!

Msukumo wa mahangaiko haukuwa kama Makabila Kumi na Mbili yaliyochanjwa kutokana na nzige, lakini uchungu kwao ulikuwa tu kama kuumwa na nyuki na sio kama vile wale wengine walivyokuwa wakiumia.

Wakati Wakristo kutoka kwa Makabila Kumi na Mbili au kutoka kwa msukumo ule, walipowakaribia wenzao walioadhiriwa, waliweza kuwaliwaza, kuwaombea na kuwapatia aina yeyote ya msaada wangalitoa. Uchungu haukuondoka lakini ukabaki kama shuhuda, sio tu jinsi Mungu alivyo na uwezo wa kuwatunza wajaa wake, lakini pia jinsi Wakristo walivyo na upendo, hata kwa maadui.

Sehemu zingine za dunia.wale ambao hawakuwa wamemfuata Yesu. walikuwa wakiendelea kukaidi. "maadui" wengi wa Mungu na wale wafuasi wake. Upendo wa aina yeyote kutoka kwa Wakristo ulizidisha chuki.

Hata ingawa mamilioni yalibadili na kumfuata Mungu, wengi wa watu duniani waliendelea kumfuata Dangchao. Waliamini uongo wake kuhusu wale Mashahidi wawili, kwamba ndio waliokuwa chanzo cha maafa yote duniani., na kwamba walidhihirisha ukatili kwa Mungu.

Miaka mitatu na nusu ya Msukumo wa Mahangaiko ilikuwa imesalia mwaka mmoja kufikia ukingoni wakati janga la nzige lilipofikia kikomo. Miezi mitano baada ya kuwasili, nzige walirudi Yerusalemi, kila mmoja akiwa amezunguka dunia. Wingu lingine la moshi mweusi lilikumba mji ule, viumbe hao waliruka ndani, na kisha wingu hilo la moto kupungua na kutokomea kwenye shimo la makaazi ya Dangchao, kwa pamoja na viumbe wale.

Zion Ben-Jonah Aandika

Maelezo kuhusu "nzige" yametolewa kwa upana katika Ufunuo wa Yohana (9:7-10) waweza kuwa wadudu wa kizazi kisicho cha kawaida, mashetani (malaika waliasi) au viumbe katili vilivyonaswa kwenye mashine, kama sura yake ya uharibifu inavyoeleza.

Kwa ulimwengu unaochukulia jehanamu kama hekaya, na kwamba shetani ni mzaha, sura hii yaweza kuwa ya kutatanisha. na hata kuhangaisha.

Lakini fikiri jinsi ingalichukuliwa miaka mia mbili iliyopita, kama tungaliongea juu ya simu za rununu, tarakilishi, roketi, mabomu ya atomiki, na miali ya Laser. Miujiza ya mungu ni miaka kama mwangaza mbele yetu, hivyo basi kuna mengi kuliko vile sisi tunaoishi katika karne ya Ishirini na Moja tunavyoweza kutambua na kuelezwa na sayanzi kuhusu maisha, dunia na kila kitu

Tunaamini kwamba Mungu hufanya kazi kwa utaratibu wake . Aidha tunaamini kwamba Mungu anao utaratibu wa sheria zote. Kwa hivyo kuna sehemu ambazo hatujaanza kugusia.

Uchawi, hekaya, vyombo visivyotambulikana angani (UFO) na mambo mengine ya kutisha yanachukuliwa kwa umuhimu sana siku hizi. Mbona tusiamini kazi za malaika, shetani, laana na uponyaji wa kiroho, hasa tunapo pata ujumbe huu kutoka kwa maandiko matakatifu kama Bibilia?