Waathirika by Dave Mckay - HTML preview

PLEASE NOTE: This is an HTML preview only and some elements such as links or page numbers may be incorrect.
Download the book in PDF, ePub, Kindle for a complete version.

22. Safari ya Yerusalemi

Katika kipindi cha miaka mitatu na nusu iliyopita, vifo na uharibifu yalikuwa mambo ya kawaida kote ulimwenguni. Maisha mengi yalikuwa yamepotezwa kutokana na vita vya kikatili katika kipindi hicho kuliko ilivyowai kutokea katika historia.

Nchini Uingereza Miji kama vile Swansea na Plymouth ilikuwa imeoshwa kutokana na wimbi kuu la bahari. Miji kama vile Liverpool pia ilikuwa imeadhiriwa na kupoteza maisha ya watu. Uingereza ilikuwa imejaribu kufanya ukarabati kuliko mataifa mengine (Hasa katika Afrika na Amerika ya Kusini na Kati) mataifa ambayo yalikuwa yameadhirika kutokana na mawimb; lakini hayo hayakutoa maelezo mengi. Kuzika mabaki ya watu ndilo lililokuwa jambo la dharura. Shughuli za marekebisho ziliwekwa kando.

Miji ya pwani iliyowachwa ilionekana kwa wingi kama dhibitisho la Msukumo wa Mahangaiko, huku watu wengi wakitafuta hifadhi. Watu waliokuwa katika maeneo hayo waliweza kutafuta samaki, hata ikiwa hawakupata mabaki ya vyakula kama ilivyokuwa katika miji mingine.

Umoja wa Mataifa ulitangaza Uingereza Kama "Nchi ya Ulimwengu" punde tu baada ya kuanguka kwa Amerika, kuonyesha kwamba ilikuwa chini ya Umoja wa Mataifa. Majeshi wa umoja huo walitii amri. Maazimio yote ya Umoja huo yalifanywa kulingana na uamuzi wa Katibu Mkuu Levi Xu Dangchao.

Uingereza ilikuwa imewapoteza watu milioni kumi kutokana na mauaji yaliyotekelezwa na Umoja wa Mataifa.

Yote haya yalizidishwa na kujifanya viziwi kutokana na idadi ya mauaji. Kwa wale waliomfuata Dangchao, ilikuwa ni dhihirisho la wazi kwamba mioyo yao ilikuwa migumu, hata kwa vilio vya watoto waliokuwa wakiuawa au kufanyiwa ukatili. Wakati wapenzi wao wakiuawa, walizidi kumkasirikia Mungu.

Kujifanya kiziwi ili kumtumikia Mungu, ilimaanisha kwamba walimtukuza Mungu na maadili yake--kitu ambacho hawakutilia mkazo wakati maisha yalikuwa ni rahisi. Mauaji hasa yale yaliyokuwa ya papo hapo kama kwa kisu kile chenye makali, ilikuwa ni tiketi ya kuelekea mbinguni moja kwa moja. Hatukuwepo na matumaini kwao katika ulimwengu, ila tu kuwashawishi wenzao kujiunga na imani yao kwa Mwenyezi Mungu na kukataa yote yaliyokuwa katika utawala wa Dangchao.

Lakini ilikuwa kama kwamba kila mmoja--wabaya na wazuri--walikuwa wakiishi katika hali ya masikitiko.

Jambo la kuhuzunisha sana lilikuwa mauaji ya watoto. Wazazi walipaswa kushikilia watoto wao mbele ya mashine ile ya kunyonga na kukata koo kwani nafasi iliyokuwemo ilikuwa kubwa kuliko vichwa vyao vidogo. Watoto wale bila shaka hawakuwa na Alama. Lakini sharti lilikuwa kwamba mayatima kutokana na Msukumo wa Mahangaiko walipaswa kupata alama kwa lazima na kisha kutunzwa katika makao ya Kiserikali.

Utawala haukutaka kuwatunza watoto wengi, lakini walichukua jukumu la kikatili kuwauliza wazazi iwapo walitaka watoto kukatwa na ile mashine au serikali iwachukue. Wengi walichagua mashine.

Watoto wakubwa (wale wenye umri wa miaka zaidi ya saba) walipaswa kutoa uamuzi wao. Wengi walichagua kufuata mamlaka, na hilo lilisababisha maafa zaidi kuliko mashine.

Watakatifu walikuja kuona iwapo ilani aliyotoa Yesu, ikiwaarifu wateule kuomba kwamba wasipate mimba au kuwa na watoto wadogo katika kipindi kitakachofuatia Msukumo wa Mahangaiko.

Vitendo vya ngono havikukoma miongoni mwa wafuasi, lakini sio kwa wingi kama ilivyokuwa kabla ya dhiki kuu. Hakuna aliyetaka kupata mtoto nyakati hizo za majaribio, mpango wa uzazi ulikuwa ni ghali kwa wale wateule kukidhi. Hali ya umati mwingi wa watu pia ilipunguza kuwepo kwa siri.

Wale waliokuwa wakitaraji kuuawa walifikiri sana. Na Makabila Kumi na Mbili yaliidhinisha hali ya kutooa, au kushiriki katika vitendo vya mapenzi. Wawili waliotaka kuoana walipewa kazi nyingi na kuwa pamoja na manyapara kila mara. Iwapo uamuzi wa kuoana uliafikiwa, ulifanywa bila kubusu au kukumbatiana. Sherehe fupi ilifanywa baada ya uamuzi kama ule.

Watu waliooana miongoni mwa Makabila Kumi na Mbili, walitengwa kwa muda mrefu; lakini walipaswa kukumbuka jinsi maisha yalivyokuwa magumu.

Kulikuwa na wachache kati ya wanachama walio kwenda kinyume. Lakini hilo liliwapa nguvu waliobaki.

Tulikuwa halikadhalika na majeruhi miongoni mwa Makabila Kumi na Mbili. Hata ingawa hakuna yeyote ambaye alikataa Alama alipata maafa kutokana na wale wadudu, kulikuwa na baadhi ya wanachama walioshikwa na polisi, wakati walipokuwa wakisaidia walio jeruhiwa kutokana na Msukumo wa Mahangaiko, na hata kulikuwepo na ulegevu wa kiusalama na kusababisha maafa. Vifo kutokana kwa njia hii, havingaliepukika, lakini mamlaka ilisita kuwatesa wale waliokosa alama, huku wakitumai kwamba walikuwa na maelezo zaidi kuhusu walipokuwa vviongozi wao.

Wengi walikuwa wamejisalamisha kwa mateso, na kusababisha kukamatwa; lakini njia kama hii haikuwa kawaida sana.

Wafuasi wapya katika mwanzo wa miaka ile tatu na nusu ya mwisho (wale ambao hawakuwa na Alama) wangalijaza pengo kutokana na wale waliohama kutoka kwa muungano wa Makabila Kumi na Mbili, ili katika mwaka mmoja uliobaki walikuwa karibu 144,000.

Lakini mwishoni mwa mwaka, idadi yao ilipungua kiajabu. Ndio waliobaki. watu waliokuwa duniani waliokata Alama. Kwa haraka walikuwa wakinyauka.

"Nini kilikumba ulinzi wetu?" Chloe aliuliza kupitia barua-pepe ya dharura kwa Rayford, pale Maria Teresa alipigwa risasi na kuuawa kule Roma.

"Ulinzi sio hakikisho," Rayford aliandika kwa kujibu wafuasi wote. "Mungu huwachilia mvua kunyeshea wazuri na wabaya. Jeshi lolote lililoshinda vita halikosi majeruhi, na tumewapata pia. Lakini tazama mbali tulikotoka. Hakika Mungu yuko nasi.

"Neno `waathirika' linamaanisha `Yule anayeishi juu'. Tunaweza kuwa hai katika mwili, na hiyo ni njia moja ya kuishi. Lakini kuna ushindi mkuu baada ya kupambana na adui wa mwisho--kifo--na kisha kuibuka kama mhanga. Ujumbe wa ufufuo ni kwamba kifo sio mwisho. Hufanya tofauti.

Kama alivyosema Mtume Paulo, kama hakuna ufufuo, basi sisi ni watu tulio taabani. Lakini kwa sababu kuna kufufuka, tutaishi--hata baada ya kuuchukua uhai wetu. Tutanusurika! Tutaishi zaidi ya hayo yote!"

Hata hivyo yeyote kati ya wale wahanga wa Makabila Kumi na Mbili aliyekuwa hai, alikuwa akihesabu siku katika miezi ile ya mwisho.

Ilipokuwa imebaki wiki mbili, Rayford na Chaim waliona ni bora waanze safari ya kuelekea Yerusalemi. Wote walifahamu kwamba ingaliishia kwa kufa, hivyo basi walipowaaga wenzao, ilikuwa ni kwa uzito kutoka ndani ya mioyo yao.

Jambo la kushangaza ni jinsi Irene alivyokuwa na amani kuhusu kuondoka kwa Rayford. Yeye ndiye aliyemjulisha ya kwamba walikuwa wameishi pamoja kwa miaka mingi kuliko wachumba wowote walio wajua. "Hesabu siku" alisema kwa kukumbatiana kwa mwisho. "Hesabu siku"

Mashahidi wale wawili waliwacha nyuma tarakilishi zao--chombo cha kipekee cha mawasiliano kati yao na Makabila Kumi na Mbili. Walichukua nguo chache za kujibadilisha na vifaa vingine vya usafi-- hakuna la ziada.

Rayford alikuwa na mbinu za kufika huko, lakini Chaim alipaswa kuabiri ndege ili kutoka kule Australia.

Chaim hakuwai kupata kuooa, na labda kutokana na hilo alikuwa na uhusiano wa karibu na waja kazi wake. Machozi yalimtoka alipowaaga. Alikuwa ni mkubwa kwa umri ukilinganisha na Rayford, na mwenye nywele ndefu za hudhurungi zilizokua kwa sababu ya kukosa wembe. "Ilikuwa ni hali ya kimaumbile kuziwacha nywele zangu kukua," alisema.

Mwishoni mwa mwezi wa Novemba jumapili moja jioni, Chaim alienda kwenye uwanja wa ndege wa Kingsford Smith kule Sydney. Hakuwa na uhakika jinsi ya kutoka nchini humo. Hakuwa na tiketi, pasipoti, visa, pesa, na wala kitambulisho, na muhimu zaidi, hakuwa na Alama. Alipita katika vitengo vya ukaguzi bila kizingiti.

Mamlaka ya uhamiaji nchini Australia yalikoma kukagua stakabadhi za wasafiri miaka kadha iliyopita.

Aliweza kupata ndege ya shirika la El Al kuelekea Tel Aviv kupitia Bangkok. Wakati wasafiri waliitwa, Chaim aliingia kwenye safu. Mwanamke aliyekuwa mbele yake alikuwa na kisulusuli cha kuanguka cha ajabu tiketi yake ilipokuwa ikikaguliwa. Huku wahudumu wa shirika lile walikuwa wakimhudumia mwanamke yule, Chaim alinyenyekea na kuingia ndani ya ndege. Ilikuwa ni rahisi tu kiasi hicho. Ndege ile haikuwa na wasafiri wengi, hivyo basi Chaim alingojea katika chumba cha mapumziko kwenye ndege ile hadi pale wasafiri wote walikuwa wameketi, na kisha kuchukua kiti ambacho hakikuwa kimekaliwa.

Kwa utaratibu ndege ile iling'oa nanga kuelekea Bangkok. Ilifikia kiasi chake na kisha kuanza mwendo. Chaim alikuwa akimshukuru Mungu jinsi mambo yalivyomuendea sawa, wakati mhudumu wa ndege alikuja alipokuwa akainama na kumuambia "kiti hiki hakijaorodheshwa kama kimelipiwa." alisema kwa upole. "Umesonga kutoka kiti kingine?"

"La, hiki ndicho kiti ambacho nimekalia tu," Chaim alimuambia yule mwanamke kwa kutabasamu na kuvinya jicho.

"Tafadhali waweza kunionyesh pasi ya kuingia?" yule mhudumu aliuliza.

"Nasikitika kwamba sina," Chaim alimuambia huku akitabasamu.

Yule mhudumu alionyesha sura ya ukali. "Waweza kunionyesha tiketi yako?"

"Ukweli ni kwamba sina hata tiketi," Chaim alimjibu kwa moyo wa mapenzi.

"Tafadhali ngojea tu hapo," yule mhudumu alisema akiondoka kwa haraka kutafuta wazo la pili kabla ya kuchukua hatua.

Sijui anafikiri nitaenda wapi huku juu, Chaim alifikiri huku akimngojea.

Katika chumba cha wahudumu, Hattie yule mhudumu alimuonyesha mhudumu mkuu alipokuwa ameketi Chaim.

"Wamuona yule mtu aliyeketi pale katikati kwenye safu ya sita kuelekea pale mwisho?" Hattie alimnong'onozea. "Hana tiketi".

"Kweli?" akasema mhudumu mkuu kama kwamba hilo lilitoa maelezo yote. "Nilimuona alipoingia. Nilidhani kwamba alifanana na mmoja kati ya wale mashahidi wawili. Uliwaona kwenye ?"

"Hakika ndio!" Hattie alisema huku akitazama maungo ya Chaim. Chaim aliona wawili hao wakimtazama na kisha kuwapungia mkono kama ishara ya salamu za kirafiki.

"Hii ni ajabu sana," Daudi alisema huku akielekea mahali Chaim alikuwa ameketi.

"Wewe ni mmoja kati ya wale Mashahidi, au sio?" Daudi aliuliza. "Nimeshautazama mtandao wenu."

Alimtazama Hattie, aliyempa matumaini kwa kusema, "Sio ajabu, Daudi. Kila mmoja ameutazama."

"Ahsante," Chaim alisema na kumsalamia Daudi.

"Sasa unafanya nini kwenye ndege hii?" Daudi aliuliza.

"Nasafiri kuelekea Tel Aviv. Kuna mambo fulani kule Yerusalemi."

"Lakini wahitaji tiketi ili kusafiri."

"Lazima muelewe kwamba siwezi kununua tiketi bila Alama; nami sina Alama,"

"Nitaongea na wakubwa wangu, na labda itabidi ndege ipinduliwe ili urudishwe Sydney. Hata iwapo watakuwacha, tutakuwa na askari wakikungojea kule Bangkok, unafahamu hayo?"

"Wadhani kwamba Mungu hawezi kunifikisha Yerusalemi?" Chaim alimuangalia Daudi na kumuuliza huku kichwa chake kimeegemea upande.

"Ndio, nimesikia hadithi. na hakika sitaki nikukasirishe!" alicheka. Lakini bila shaka hautatekeleza jambo baya, hasa kwenye ndege, ama?"

"Kusema kweli," Chaim alisema akimuashiria Daudi kuinama ili aweze kunong'ona, "Sina uwezo. Nafahamu tu muda mchache kabla ya tukio. Naamini kwamba Mungu ndiye anayefahamu aina ya kinga ninayohitaji."

"Nitaongea tu na Rubani kisha nikujulishe," kijana huyo alisema.

"Ahsante," Chaim alitabasamu, na kisha kurejelea kusoma gazeti alilokuwa akisoma walipo ng'oa nanga.

Katika chumba cha rubani kulikuwa na majadiliano ya faragha na kisha simu kupigwa Sydney.

"Anasema kwamba tutakuwa na hali ya makabiliano," Yule rubani alisema.

Maelezo yalitoka kule kwamba wasifanye lolote la kumkera Chaim, na kwamba waende tu Bangkok ambako mamlaka itajulishwa.

Lakini mtu mmoja katili aliyefanyia shirika hilo la ndege kazi, alipiga simu kule Israeli, na kutoa ujumbe kwamba habari ziwasilishwe kwenye makao ya ikulu. Wakati ndege ilipotua Bankok saa nne usiku saa za huko, mawaidha yalibadilishwa. Chaim alipaswa kubaki ndani ya ndege hadi saa sita za usiku kisha apelekwe Tel Aviv. Sherehe za kumkaribisha zilikuwa zaandaliwa katika uwanja Ben Gurion asubuhi itakayofuatia.

Ujumbe ulifika kule Tel Aviv, na habari kwenye runinga zilieleza kwamba Chaim alikuwa ameteka nyara ile ndege. Nusu ya wanahabari wote iliwasili katika ule uwanja wa ndege, kwa pamoja na kile kilichoonekana kama jeshi nzima la Umoja wa Mataifa.

Wakati ndege ilipotua kule Tel Aviv, ilielekea katika sehemu ya mapokezi ya raia wa nchi ambayo yalikuwa yamewekwa usalama. Chaim alikubaliwa kushuka kivyake huku ndege ikielekea mahali pa kupokea abiria wa kigeni pamoja na wale wasafiri wengine.

Chaim alipitia mlango ulioelekea chumba cha mapokezi huku mianga kutoka kwa wapiga picha ikiwaka. Alipungia mkono wale wanahabari, kisha kiongozi mmoja wa Umoja wa mataifa akaja mbele, akijaribu kuwa mjasiri kwa ajili ya wapiga picha, huku akijifanya asiyemuogopa Chaim kutokana na nguvu zake maalum.

"Nina kuarifu kwamba utaandamana nami" alisema huku akitaraji jibu.

"Bila shaka" Chaim alijibu. Alichukuliwa na kusukumwa kwenye gari la polisi.

Akachukuliwa, sio kwenye kituo cha polisi, lakini ndani ya jumba la kifahari kule Yerusalemi.

"Kwani! Hatimaye tumekutana! Dangchao aliwika huku Chaim akielekezwa kwenye chumba chake cha mamlaka. Kila mmoja aliinama na kusujudu mbele ya Katibu Mkuu, isipokuwa Chaim aliye simama wima.

"Wapi mwenzako?" Dangchao aliuliza.

"Sijui," Chaim alijibu.

"Labda nitakufungia hapa nione kama atakuja."

Chaim hakujibu.

"Tutakuwa na wakati mwema nawe hapa katika Hekalu," alisema kwa hali ya ukaidi machoni mwake.

"Halikadhalika Mungu atakuwa na wakati bora nawe," Chaim alijibu, kwa ujasiri jinsi alivyoongea mteka wake. Dangchao alihisi nguvu za tisho hilo na kunyamaza.

"Ni mzaha tu nataka kumuuliza rafiki yako maswali fulani tu. Twahitaji kufanya kazi pamoja. kwa wema wa dunia."

Kwa mara nyingine Chaim alinyamaza.

Habari ziliarifu kwamba Chaim alikuwa ameshikwa na kuzuiliwa katika ikulu. Dangchao alitumai kwamba hayo yangalimvutia Rayford.

Zion Ben-Jonah Aandika

Kufuatia mahangaiko makuu, Yesu alisema kwamba, Wakristo watasalitiwa na kuuawa kutokana na imani yao (Luka 21:16) na kisha kusema (aya ya 18) "Hakuna hata unywele wenu utakao angamia." Hali ya kukanganya inatokea pale Rayford anasema katika sura hii kwamba "Ulinzi sio hakikisho"

Twaweza kufa kutokana na imani yetu, lakini "hatutaangamia". Hiyo ndiyo maana ya "kuishi juu." Hakuna hakikisho kwamba hatutateseka. Kwa hakika mtazamo ni kinyume (Timoteo II 3:12) Bila shaka ulinzi wetu utakuwa wa kirohi na wa milele, na sio wa muda.

Hii ndio sababu kwamba maono ya "Mahangaiko" ni muhimu kwa yeyote aliyeamini, kwa kila umri. Tunapovumilia majaribio na hata kutazama mauti, tutajichagua kiroho. Maisha kwa wengi wetu yapaswa kuwa na utulivu na sio matayarisho ya mauti.

Bibilia inasema kwamba wakati wa Nuhu na ule wa Sodoma na Gomora, walikuwa wakifanya tu bidii ya kuoana na kuzaa tu bila kufikiri Mungu; na ni kwa sababu ya hayo kwamba (na sio tu mashoga na walawiti au wasio mtambua Mungu) waliangamizwa. (Luka 17:26-30)

Hata wale Mashahidi wawili watakuwa na upungufu, kama vile Chaim anavyoona katika sura hii.